Amecheza karata vizuri, ila angeleta ujeuri wa kutishia kuhama chama basi ndio ulikua mwisho wake kisiasa.
Ange danganyika kwenda CCM kisa Dk. Bashiru amemkaribisha au kinga walioahidiwa na Speaker pamoja na A.G, angekutana na fitna nyingi sana za wana CCM kindaki ndaki.
ILA BADO ninaamini serikali ndio imemshinikiza aongee hayo kwenye hii press ya leo. Baada ya kuona dunia na taifa zima limepokea "NEGATIVELY" kulazimishwa kwa Covid-19 kuapishwa bila ridhaa ya chama chao na Mwanasheria Mkuu Wa Serikali na Speaker kujigamba kuwatetea kwa nguvu zote.
Pia Covid-19 walishagawanyika, kuna waliotaka kurudi na kuomba msamaha, na kuna waliotaka waendelee na ukauzu wao.
CHADEMA NINGEPENDA KUONA wanatumia karata zao vizuri kukubali maridhiano ya kina Halima Mdee & Co LTD. Kwa kuwapa mashart umiza;
1) Ili kupokea baraka na msamaha wa chama, basi Covid-19 wafanye press kutoa muongozo wa nani alieshinikiza wao kuapishwa. Na vikao vilifanyika vipi na wapi.
2) Covid-19 waandike barua za kujivua ubunge wa kuteuliwa kwa NEC na SPEAKER (Japo kisheria baada ya kufukuzwa uwanachama wameshaondolewa).
3) Katika press hio Covid-19 watoe tamko la kuungana na wanachama wenzao sambamba na vyama vingine vya upinzani kutotambua uchaguzi mkuu 2020 pamoja na bunge hili.
4) Pia katika press hio "WAOMBE MSAMAHA CHAMA NA WANACHAMA" kwa kukubali kufanya hayo waliofanya ya kuapishwa bila ridhaa ya chama. Na wakiri walikosea sana.