Halima Mdee: Porojo za Dodoma haziniumizi

Halima Mdee: Porojo za Dodoma haziniumizi

Wachache nilio wanukuu MJITAFAKARI NA KUCHUKUA HATUA, ili mrejeshe uungwana wenu. Lakini kwa kuwa mnaandika nyuma ya keyboard na ID feki, mnaona ni sahihi kuunga mkono upuuzi wa Halima na Esther. Lakini, naamini moyoni mwenu hao wabunge siyo tu wanajidharirisha, pia wanadharirisha CHADEMA na heshima zenu humu JF
Nadhani umendika bila kutafakari. Take time kidogo kunywa maji fikiri hivi nine lipo kwenye mstari?
 
Hivi hawa maspika hawanaga hata aibu?? . Maana kuna maisha nje ya bunge.

Mkuu aibu waipata wapi, maisha baada ya uspika wanapewa ujumbe wa bodi au wakuu wa vyuo vikuu. Kwa ujumla jinsi utakuvyojipendekeza na kufanya kile anachokitaka yule mwenye nguvu ya uteuzi hata baada ya uspika una uhakika wa kula kodi za wananchi kama fadhila.
 
Safi sana kamanda hizo porojo tu mapambano yanaendelea.
 
Ndugai kadri anavyozeeka ndivyo anavyozidi kuoza kichwani!! Hivi viwavi jeshi wana madhara gani kwenye ubongo? Maana tangu Wagogo waanze kula viwaji jeshi imekuwa kero. Ukimsikiliza Lusinde ndo utachoka kabisa, ukimsikiliza Simbachawene naye hivyo hivyo. Inahitaji research ya kujua madhara ya hawa wadudu kwa watumiaji!!
 
Bunge lile nalo bola wawachie waendelee kukaa kama kikundi cha wahuni tu eti ccm loh!
 
Wachache nilio wanukuu MJITAFAKARI NA KUCHUKUA HATUA, ili mrejeshe uungwana wenu. Lakini kwa kuwa mnaandika nyuma ya keyboard na ID feki, mnaona ni sahihi kuunga mkono upuuzi wa Halima na Esther. Lakini, naamini moyoni mwenu hao wabunge siyo tu wanajidharirisha, pia wanadharirisha CHADEMA na heshima zenu humu JF

Ni kweli ulio dhahiri kwamba Mdee na Bulaya hawakutenda kama ambavyo wewe ungetaka au mimi na wengine. Lakini kwa mtu mwenye kutaka kutoa hukumu ya haki ulipaswa uungwana wako ujielekeze kwenye kiini cha tatizo. Kiini cha tatizo kipo wazi na sehemu kubwa tatizo lilichangiwa na kiti cha spika ambaye ni dhahiri alikwepa kumuona muanzisha zogo kisa yuko chama chake. Na udhaifu huu wa upendeleo wa kiitikadi umekuwa ukifanywa karibia na maspika wote wa kipindi cha bunge la vyama vingi.

Hebu tujiulize leo kabisa kama watu wazima, kwenye kundi la wabunge chini ya 90 wa upinzani humo ndio kuna watovu saana wa nidhamu ambao kila siku kamati ya kina Mkuchika inaona makosa yao. Lakini bunge hilo hilo lisione watovu ndani ya wabunge zaidi ya 250 wa ccm. Hii inakuingia akilini kweli? Wewe mwenye unapita sana humu jukwaani, unaangalia bunge, ni kweli kama kiti kinatenda haki wabunge wa ccm wana nidhamu ya kiwango cha hata siku moja kutotiwa hatiani?

Wewe sema hivi cdm ni watoto wa kambo hivyo wanapaswa kujifunza kuishi na mama wa kambo na wala sio suala la kutuambia eti kina Mdee, Bulaya wana makosa saana ya kukosa bunge mwaka mzima. Nilichokiona kwa Ndugai na yeye anataka kumuiga Magufuli eti kwamba hachekicheki, anaogopa asije akaambiwa kama alivyoambiwa Mangu, " I wish if I could be IGP" Hayo yote ni kutaka kumuiga eti mkuu wa nchi kwamba hana mchezo na wapinzani kama alivyo mkulu kwa wapinzani. Pale kwangu naona Ndugai ni kama anaiga tembo kunya.
 
Ni kweli ulio dhahiri kwamba Mdee na Bulaya hawakutenda kama ambavyo wewe ungetaka au mimi na wengine. Lakini kwa mtu mwenye kutaka kutoa hukumu ya haki ulipaswa uungwana wako ujielekeze kwenye kiini cha tatizo...

Hebu tujiulize leo kabisa kama watu wazima, kwenye kundi la wabunge chini ya 90 wa upinzani humo ndio kuna watovu saana wa nidhamu ambao kila siku kamati ya kina Mkuchika inaona makosa yao...

Nakubaliana nawe kwamba si wabunge wa upinzani tu wanaongea hovyo, je hiyo ni tiketi ya mbunge mwingine kufanya hivyo!

Unasema Kiini cha tatizo kipo wazi na sehemu kubwa tatizo lilichangiwa na kiti cha spika ambaye ni dhahiri alikwepa kumuona muanzisha zogo kisa yuko chama chake...
. Mimi sizijui kanuni za Bunge lakini naamini kwamba Bunge ni sehemu nyeti na ya heshima ambako wabunge huitwa waheshimiwa. Hivyo maneno na matendo yao lazima yawe katika misingi hiyo ya uheshimiwa.

TULAANI KWA NGUVU ZOTE VITENDO VYA KIHUNI VYA BULAYA NA MDEE
 
siasa bana, na akili zetu watanzania zilivyo ndogo basi wanasiasa kwa kutambua hilo huwa wanatufanya kama mbwa koko akirushiwa mfupa anaenda tu bila kujua anaweza akawekewa sumu... Huyu Spika Ndugai si ndiyo wapinzani wakiongozwa na Lowassa walisema bunge linaendeshwa kienyeji na Naibu Spika Dk Tulia, kwa sababu ya kutokuwepo kwa Spika Ndugai kipindi kile alipokuwa anaumwa. Na kuna lugha kabisa ilitamkwa kwamba Spika Ndugai ni mtu makini, kipindi kile wanaomba apone haraka arudi bungeni.. Leo hii mbaya tena, shikamoo siasa.
 
Ni katika kujifariji tu. Hizo anazozitaa porojo ndiyo zilimuumiza kichwa kwenye adhabu ya kwanza zikamfanya akiri makosa yake na akaomba samahani. Tatizo kubwa la huyu dada anaamini kuwa bila kufanya hivi hawezi kuwashawishi wapiga kura wake.
 
Back
Top Bottom