Lema na Mbowe pamoja na Dr.Slaa sijui watamchukulia hatua yeyote Halima Mdee au kwa sababu ni wa nyumbani.
Ukweli ni ukweli tu Magufuli ni Jembe... Hana vinasaba vya ccm
Hakika Halima Mdee siku zako huko chadema zina hesabika! Hakika na jimbo lako sasa litachukuliwa na Josephine maana huu ni usaliti kusifia mawaziri wa Jk!
Katika hali isiyotarajiwa Mbunge wa Kawe Halima Mdee amemtaja Dk.Magufuli kuwa ni Jembe kwenye mkutano Goba katika uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi barabara ya Mbezi Mwisho kwenda Goba mpaka Tangi Bovu.
Aidha, wananchi wa Goba (Wote CHADEMA na CCM) wamempokea Dk.Magufuli kwa shangwe wakimwita "JEMBE JEMBE" Clip ya video inakuja.
Pia alikuwepo Mbunge wa Jimbo la Ubungo Mh.John Mnyika na wote kwa pamoja wamesema "MAENDELEO HAYANA CHAMA"
View attachment 221823
Dk.Magufuli (W/Ujenzi), Halima Mdee(MB-Kawe) na Madabida(M/Kiti CCM -Dsm)
View attachment 221825
Kutoka Kushoto Mkuu wa Mkoa Dsm, Dk.Magufuli, Madabida na Mh.Mnyika.
Kwani ni magufuri au ni wananchi kupitia kwa mtumishi magufuri? Hizo ni kodi za wananchi wali si hela magufuri. Kingine, hapo ametimiza majukumu yake anayoripiwa mshahara.