Halima Mdee aibuka shujaa Kawe

Halima Mdee aibuka shujaa Kawe

Tabata kero hii ccm imekaa madarakani miaka nenda rudi,hali ndiyo kwanza inazid kuwa mbaya

hata maji ambayo ni uhai ccm mnaifanya iwe ni ajenda ya kisiasa??

Hatari sana,,hizi species za binadam hawa sijui zimedondoka kutoka sayari gani,,hawana huruma kabisa??
 
Ahsante kwa taarifa mkuu. Sijui gamba MAFILILI litaficha wapi sura yake?

Hii ni janja tu, Mdee kawapanga Clouds ili aonekane amefanya mazuri Kawe; Uhalisia Halima Mdee hauziki tena jimboni Kawe
 
Imekugundulika wananchi waliojipeleka Clouds TV na kutoa ushuhuda ni kundi la akina Chuwa, Masawe, Mramba, Mremi, Swai, Lema, Shayo, Shio & Co. Janja ya Mdee tumeigundua, 2015 ni mwisho wa Mdee na Chadema kwa ujumla jimboni kwetu tumewagundua hamna tija kwa wananchi
 
Imekugundulika wananchi waliojipeleka Clouds TV na kutoa ushuhuda ni kundi la akina Chuwa, Masawe, Mramba, Mremi, Swai, Lema, Shayo, Shio & Co. Janja ya Mdee tumeigundua, 2015 ni mwisho wa Mdee na Chadema kwa ujumla jimboni kwetu tumewagundua hamna tija kwa wananchi

Mkuu watu wa hilo kabila walikunyanganya nn hasa. Mbona unawachukia zaidi ya chenge,Lowasa,mkapa,Mramba,.............

Punguza Chuki Mkuu na kama kuna kitu unaona wamefanikiwa kushinda wewe fanya mpango uwaige na wewe utafanikiwa tu. Chuki na wivu ni mzigo mzito ambao mwisho wa siku itabidi uwaachie na watoto na wajukuu zako mzigo huo usio na maana yoyote kabisa.
 
Hii ni janja tu, Mdee kawapanga Clouds ili aonekane amefanya mazuri Kawe; Uhalisia Halima Mdee hauziki tena jimboni Kawe
Kuna sredi ya jamaa wa Mbezi akimlalamikia barabara za Mbezi.
Naona wakazi wa huko wamefumba maji vinywani wakimsubiri 2015.
 
Hakika leo clouds imeweka ushabiki pembeni
eti ushabiki pembeni ni kwa chadema tu. ujinga. halafu unatakiwa ujue kwamba suala la maji ni miongoni mwa ahadi za jk wa wana-dar wote tupate maji. full stop.
 
Mheshimiwa Mdee ni performer, siyo mpiga blah blah,endelea kupigania wana Kawe hadi kieleweke,
 
Hii ni janja tu, Mdee kawapanga Clouds ili aonekane amefanya mazuri Kawe; Uhalisia Halima Mdee hauziki tena jimboni Kawe

Kwasababu mmezoea kuwahada wananchi kwa kutumia tbc1 mnafikiri na wengine wanafanyahivyo.
 
safi sana mbunge wetu,njoo na huku mbezi juu,maeneo ya jogoo mabomba ya wachina hayatoi maji,tumefuatilia dawasco hadi tumechoka!karibu muheshimiwa

Pole sana ndugu zangu wa Jogoo shida ya maji imekuwa ya miaka yote hasa eneo la ukanda wa bomba la gesi kule juu kuteremka hadi kati. Jamaa zangu wanaishi huko kila wiki inawagarimu sh.45,000 hadi 55,000 kununua maji. Biashara ya maji huko imeshika kasi watu wanashangaa bomba kuu la maji la Ruvu chini linapita pale Africana kwenda masaki, Mikocheni, mjini n.k. lakini wao wanasota. Eti wanasingizia mwinuko pressure ndogo! iliwezekanaje Goba, Makongo na Wazo ambako mwinuko ni mkali zaidi ya ule wa Jogoo na maji yanatoka? wachina walioweka mabomba kabla ya kukabidhi mradi kwa Dawasco walitest kwa kutumia maji yao yakapita na kufika maeneo yote. Nini kiliendelea baada ya hapo! Zilitolewa pesa za mradi unaofadhiliwa na World Bank kupitia serikali ya mtaa ili kuchimba visima virefu kunusuru maisha ya wanyonge, M/kiti wa serikali ya mtaa na diwani walichokifanya Mungu ndiye anajua! shuguli ya uchimbaji ilianza kama ushahidi na gafla wakafunga virago wakaondoka. hakuna maelezo hadi sasa. Ila nyie wakazi wa Jogoo mmezidi kwa upole, ndiyo nasikia Huyo M/kiti mmemtimua lakini je huo ubadhirifu aliofanya kajenga nyumba ya kifahari mda mfupi, anajenga tena gorofa pesa kapata wapi kwa mshahara gani? Angalia barabara yenu toka Afrikana kwenda juu tunapata shida sana tunapokuja huko magari hawezi kupishana mpaka mmoja asimame kwanza pembeni apishe na mvua zikinyesha ndio basi tena magari mnapark! Mh. Halima Mdee, hili jukumu libebe pia. Tembelea africana panda na hiyo barabara mpaka nguzo za umeme mkubwa ujionee mwenyewe. kutana na wananchi wako watakujuza mengi
 
MAFILILI, haya yanaonekana katika posts zako.

1. Chuki mbaya sana dhidi ya CDM

Hii ni janja tu, Mdee kawapanga Clouds ili aonekane amefanya mazuri Kawe; Uhalisia Halima Mdee hauziki tena jimboni Kawe

Hima Hima wana CCM sasa ni wakati wa kuwa wagumu ili chama kibadilike muonekano wake miongoni mwa wanajamii. Kuzorota kwa CCM ni anguko la wazee, vijana na watoto wenye utashi na upendo wa dhati kwa Tanzania.

Nawashangaa wana CCM wenzangu wa mkoa wa Mtwara kubadilika na upepo wa msimu ambao mbeleni MTAJUTA, CHADEMA inataka kuwatumia ili waweze kutimiza kura TU.

Chonde chonde Wamakua, Wayao, Wamakonde na Wamwera kwa nini mnatutesa nyie ni CCM damu damu tangu enzi za TANU mliitikia vyema sera za Ujamaa na Kujitegemea, mkawa mfano wa VIJIJI VYA UJAMAA, leo hii Dr. Slaa & CO mnawapa nafasi hadi vijijini kwenu kufungua matawi.

Mkuchika, Ghasia, Mama Kasembe, Murji, Mkapa wa Nanyumbu, Njwayo na Bwanausi fanyeni KIKAO CHA DHARULA tuepuke FEDHEHA ya leo CHADEMA kuingia hadi maeneo ya jikoni!!!!

Watanzania wenzangu nilikuwa na ziara katika majimbo ya Kawe, Ubungo, Mbeya Mjini, Iringa Mjini, Rombo, Singida Mashariki, Hai na Kigoma Kaskazini nimekutana na mambo yasiyoridhisha katika halmashauri husika. Wabunge wao wameshindwa kukaa chini ili kusikiliza kero za wananchi na kuzitafuatia ufumbuzi.
Wananchi wa maeneo hayo wamesema "wanajuta kuwachagua wabunge ambao wawapo bungeni wanashikiria maslahi ya chama zaidi kuliko matakwa ya wapiga kura". Mbaya zaidi wabunge wao wanatumia muda mwingi kuhamasiha wananchi washiriki maandamano badala ya kuwahimiza wafanye kazi ili wajiletee maendeleo. Wanachadema muwe wawazi kuwaambia wabunge wenu WABADILIKE!!


2. Uongo:

Huyu Mnyika tangu amekuwa mbunge nini katufanyia wana Ubungo??? Barabara ya Golani - Suka kashindwa, Makabe usiseme; wananchi tunamkumbuka Keenja
Hapa ni wa Ubungo.

Nasie wakazi wa Mwanjelwa twamtaka Sugu aje kugani mistari
Hapa wa Mwanjelwa Mbeya
Samahani kwa kutoa malalamiko dhidi ya mbunge wangu. Mie mambo ya Temeke, Ilala, Ubungo nk hayanihusu nimezungumzia mbunge wetu. Wapiga kura wamepigwa na polisi pia wakachomewa nyumba na mashamba yeye ameshindwa kuwasaidia wala kuwapa pole. Kuwa mkweli Halima Mdee hatupi haki yetu wana Kawe

Hapa unakana Ubungo sasa wewe ni wa Kawe.

Hata kama ni siasa, zijenge kwenye msingi wa ukweli na uungwana.

Otherwise you will not be taken seriously!
 
SERIKAKI!!??? rudi darasa la pili A
Ni vyema ikafahamika kuwa miradi ya wananchi inatekelezwa na serikali au wahisani jwa niaba ya serikali. Hivyo bila serikali kuuamua na kutenga fedha, hata mbunge apige kelele vipi haitasaidia. Hii ni kwa wabunge wote bila kujali vyama. Ndo maana pamoja na kumpongeza mbunge kwa ufuatiliaji ni lazima pia serikali ipongezwe
 
Hongera sana halima,sasa ebu mpe mbinu mnyika ili nasi tuweze kupata maji,watu wa mbezi/kimara /mpigi-msakuzi tunapata shida sana ya maji.
 
she did a nice job, congratulation kamanda wetu , mpiganaji wa matatizoya wananchi wa kawe
 
Back
Top Bottom