Hali ya wanachuo mtaani

Hali ya wanachuo mtaani

Quartz360

Senior Member
Joined
Mar 27, 2023
Posts
133
Reaction score
318
Siku hizi mitaa imepambwa na degrees za kutosha kutoka mavyuoni, Lakini cha ajabu vijana wamekua wakitia huruma kuliko hata aliyemaliza la saba, WANACHUO wengi wanapata taabu sana huku mtaani kuliko hata raia wa kawaida, kiukweli inahuzunisha. Pale kijana anapotoka chuo na matarajio makubwa Lakini ghafla maisha ya mtaa yanazima ndoto zake.

Yapi matunda ya mfumo wetu wa Elimu? Au ni uzembe wa vijana kutojituma wawapo mtaani?

#MyCountryPeople.
 
wengine sie hata ajira ziwe wazi wazi, kuna vigezo vinatutoa nje ya mfumo.

Na tusharidhikaaa, polee zao wenye matarajio ya ajira, wanabaki kufurahishwaa km sio kushangazwaa,

Jamaa wa Petroleum anaendesha bajaji, GPA 3.8

Namuangalia nasemaa hiiii,
 
Kuna dada mmoja alikuwa pini sana chuoni..kamaliza mwaka jana..nilimfukuzia sana lkn wapi alikuwa anaweka ngumu sana( nadhani alikuwa na mshkaji wake) sasa mwaka huu nipo kwenye mishemishe zangu si nikakutana nae sehemu anauza vitumbua...ameisha...ule uzur wake umepungua haswaaaaa...yani alishtuka kuniona akawa anavunga tu...nikamuungisha nikasepa zangu

Sikutaka kufanya lolote kwan nilijua tu huyu safar hii hachomoi..na zigo lote litaniangukia mm(gharama za kumtunza)
 
Kuna dada mmoja alikuwa pini sana chuoni..kamaliza mwaka jana..nilimfukuzia sana lkn wapi alikuwa anaweka ngumu sana( nadhani alikuwa na mshkaji wake) sasa mwaka huu nipo kwenye mishemishe zangu si nikakutana nae sehemu anauza vitumbua...ameisha...ule uzur wake umepungua haswaaaaa...yani alishtuka kuniona akawa anavunga tu...nikamuungisha nikasepa zangu

Sikutaka kufanya lolote kwan nilijua tu huyu safar hii hachomoi..na zigo lote litaniangukia mm(gharama za kumtunza)
Kijana una akili Sana
 
Shida watu hawataki kuface reality mkuuu

We ushashauriwa kuwa uende veta after f4 we unashupaza tu shingo matokeo yake ndo haya....

Ukienda chuo nenda kuchukua ujuzi tu hakikisha unachokisomea ni rahisi kujiajiri

Sasa mtu unaskmea civil engineering ajira hamna mtaji inatakiwa 47M huna uhakika wa tenda ni majuto tu

All in all sikuizi ajira ni bahati ya mtu
Kazi ipo,. Imagine baada ya miaka 10 mbele hali itakuaje.
 
zamani nilivyokuwa nasikia mtu amesomachuo nilikuwa namheshimu sana. Nilidhani wanajua/ wamesomea vitu vingi sana kumbesio kabisa

Kumbe wanasomea kitu kimoja tuu ukimaliza unasaka ajira ukikosa imekula kwako mana vitu vingine ukikosa ajira kujiajiri inakuwa mtiti labda ujiongeze ukajifunze kitu kingine au ufanye biashara yoyote ile

Mtu mwingine unamuuliza chuo umesomea nini jibu analokupa unatamani umzomee kwa kupoteza muda wake kwenye kitu ambacho hakiwezi kumsaidia kamwe ila tunavunga tuu

imagn mtukasoma masomo ya sayansi nabado maisha kwake nimagumu sana dah
 
Mleta agenda hii uko sahihi kwa 100%
Shida ya ajira imekuwa kubwa mno
Na inaendelea kuwa kubwa sana
Ukiangalia mfumu ya elimu umekaa kibiashara pia
(Yaani vyup pia ni biashara inafanywa)
Maana unalipa Ada ili upate elimu
What next baada ya kumaliza sio issue kwa
Wanabaki ku focus kupata batch mpya
Hili jambo linahitaji mjadala mpana labda pia kubadilisha mfumo mzima wa elimu.
Ifike mahali tuachane na bookish
(Elimu ya kuwinda white colour jobs)
Na kwenda elimu ya ufundi na vitendo zaidi
Ama elimu ya kumuwezesha kijana kufanya jambo la
Either
Ufundi
Ukulima(hapa ardhi tunayo maji tunayo)
Uvuvi(bahari na maziwa tunavyo)
Ufuguji wa kisasa(Ardhi kubwa ipo)
Uzalishaji wa nguo(kurejesha viwanda vya pamba na kuanza kuzalisha vitambaa)
Nk
Hayo ni baadhi ya madadililo yanapaswa kufanyika top down
Kimfumo na mtu mmoja mmoja
Nawasilisha.
 
Mleta agenda hii uko sahihi kwa 100%
Shida ya ajira imekuwa kubwa mno
Na inaendelea kuwa kubwa sana
Ukiangalia mfumu ya elimu umekaa kibiashara pia
(Yaani vyup pia ni biashara inafanywa)
Maana unalipa Ada ili upate elimu
What next baada ya kumaliza sio issue kwa
Wanabaki ku focus kupata batch mpya
Hili jambo linahitaji mjadala mpana labda pia kubadilisha mfumo mzima wa elimu.
Ifike mahali tuachane na bookish
(Elimu ya kuwinda white colour jobs)
Na kwenda elimu ya ufundi na vitendo zaidi
Ama elimu ya kumuwezesha kijana kufanya jambo la
Either
Ufundi
Ukulima(hapa ardhi tunayo maji tunayo)
Uvuvi(bahari na maziwa tunavyo)
Ufuguji wa kisasa(Ardhi kubwa ipo)
Uzalishaji wa nguo(kurejesha viwanda vya pamba na kuanza kuzalisha vitambaa)
Nk
Hayo ni baadhi ya madadililo yanapaswa kufanyika top down
Kimfumo na mtu mmoja mmoja
Nawasilisha.
Comment nzuri sana hii.
Shida Sasa vijana wetu wanawaona walioenda vyuo vya kati mfano VETA kwenda kusomea ufundi ni Kama wamefeli vile, hata jamii nayo inamwona aliyeenda chuo kikuu ni kipanga na alieko VETA ni kilaza,,, Lakini maajabu yanakuja pale wote wanapohitimu.
 
Siku hizi mitaa imepambwa na degrees za kutosha kutoka mavyuoni, Lakini cha ajabu vijana wamekua wakitia huruma kuliko hata aliyemaliza la saba, WANACHUO wengi wanapata taabu sana huku mtaani kuliko hata raia wa kawaida, kiukweli inahuzunisha. Pale kijana anapotoka chuo na matarajio makubwa Lakini ghafla maisha ya mtaa yanazima ndoto zake.

Yapi matunda ya mfumo wetu wa Elimu? Au ni uzembe wa vijana kutojituma wawapo mtaani?

#MyCountryPeople.
Mchawi wao alikuwa ni magufuri aliacha ameharibu kila kitu vijana wanatakiwa kwanza wajikubali na wawe na mioyo migumu kama jiwe popote pale ikitokea fursa wewe jichanganye hata zambia nendeni
 
Back
Top Bottom