Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,188
- 44,142
Hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme. Kama huamini rudia tena mawazo haya hadi ujishawishi kuwa unachoshuhudia ni kitu kingine zaidi ya mgao wa umeme. Kwanini hakuna mgao wa umeme? Kwa sababu walisema hakutakuwepo mgao wa umeme tena, mgao wa umeme utakuwa historia. Kwa hiyo kinachotokea ni historia tu ya mgao wa umeme ulivyokuwa; wanatumia nafasi hii kuwakumbusha historia ya mgao wa umeme msije mkasahau.
Na hakuna namna nzuri ya kuwakumbusha watu kuhusu tukio la nyuma kama kwa kutumia 'mfano halisi'. Kwa hiyo, wale waliokuwa wamesahau au ambao hawajui mgao basi hii ni namna nzuri ya kukumbuka. Hiki ndicho alichokisema Waziri Yule kuwa mgao wa umeme utakuwa ni "historia".
SICHO HICHO
Hiki kilichoko sicho, hiki sicho kilichoko,
Ndicho hiki hichohicho, ndicho hiki hakiko,
Hiki ni kile si hicho, kile kisichokuwako
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya mgao!
Aliyesema hakiko, kwamba hakitakuwapo,
Yeye mwenyewe hayuko, alichosema hakipo,
Huyu bwana yuko yuko, kama popo mwenye pepo,
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya mgao!
Wanachogawa hakipo, kwani kisingekuwepo,
Ugawe vipi hakipo, hakipo huko mlipo,
Kama wafuata upepo, ndugu zangu mpo mpo,
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Cha nini hki cha nani, kwanini tena ni nini?
Tutamuuliza nani, kinaendelea nini?
Tunakuwa kama nyani, kujenga nyumba mtini!
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Tukubalini watani, janja ya jiwe ya nini?
Hili jambo siyo geni, linarudia kwa nini?
Ahadi zao jamani, twaamini kama dini!
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Na hakuna namna nzuri ya kuwakumbusha watu kuhusu tukio la nyuma kama kwa kutumia 'mfano halisi'. Kwa hiyo, wale waliokuwa wamesahau au ambao hawajui mgao basi hii ni namna nzuri ya kukumbuka. Hiki ndicho alichokisema Waziri Yule kuwa mgao wa umeme utakuwa ni "historia".
SICHO HICHO
Hiki kilichoko sicho, hiki sicho kilichoko,
Ndicho hiki hichohicho, ndicho hiki hakiko,
Hiki ni kile si hicho, kile kisichokuwako
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya mgao!
Aliyesema hakiko, kwamba hakitakuwapo,
Yeye mwenyewe hayuko, alichosema hakipo,
Huyu bwana yuko yuko, kama popo mwenye pepo,
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya mgao!
Wanachogawa hakipo, kwani kisingekuwepo,
Ugawe vipi hakipo, hakipo huko mlipo,
Kama wafuata upepo, ndugu zangu mpo mpo,
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Cha nini hki cha nani, kwanini tena ni nini?
Tutamuuliza nani, kinaendelea nini?
Tunakuwa kama nyani, kujenga nyumba mtini!
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Tukubalini watani, janja ya jiwe ya nini?
Hili jambo siyo geni, linarudia kwa nini?
Ahadi zao jamani, twaamini kama dini!
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!
Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)