Tunavuna matunda ya Serikali ya CCM kwa kuwa madarakani kwa miaka hamsini halafu wanazunguka nchi nzima eti Chadema hawajafanya uchaguzi, Katiba ya Chadema ina matatizo, eti Mbowe hafai kuwa M/Kiti wa Chadema na kuendela...
Ukiwauza Mambo ya Umeme na Rasilimali za Nchi wanatokwa na Povu, na kuna makada wao kila siku utasikia jitambue eti kwa kuishabikia chama ambacho kimetufikisha hapa, Miaka saba ijayo hatutakuwa na dhahabu, Tembo watakuwa wameisha kwenye hifadhi maana ndugu zao waachina wamewapa sumu ambayo akipewa tembo penzo zinanyofoka tu bila kutumia nguvu sana.
Bado wanasema tujitambue, kuna mavuvuzela kibao yanazunguka nchi nzima eti kuelimisha wananchi waichague CCM kwa lipi???
Elimu wameiuwa, Afya hakuna Kitu, Nishati na Umeme tabu huku Gesi inachukuliwa bure.