Hakuna Mgao wa Umeme Tanzania...

Hakuna Mgao wa Umeme Tanzania...

Zamani nikisikia mtu ni Profesa huwa namchukulia sio mtu wa kawaida.
Nilikuwa naamini upeo wao ni hali ya juu sana. Kamwe hawafanyi upuuzi puuzi.
lakini tangu huyu Waziri atumikie hii nafasi na kauli zake alizokuwa anazitoa, na hivi karibuni yule mbunge wa Urambo wamefanya niwe na mtazamo tofauti kabisa na ule niliokuwa nao.
Profesa Muhongo/muongo+Profesa Kapuya/mbakaji=CCM ya kuwaletea maisha bora kwa kila Mtanzania!
 
Inabidi watanzania wote bila kujali itikadi tuamuke! Suala la umeme halina itikadi sote tunaumia. Shughuli nyingi zimekwama. Uchumi wa watu na pia wa taifa vinaporomoka.

Leo nilikwenda Kariakoo na baadaye kwenda Posta. Ofisi tatu nilizokuwa nimepanga kwenda shida yangu haijatatuliwa kwa kuwa hakuna umeme! Wafanyakazi ambao kazi zao zinategemea umeme wamekaa tu na hakuna kinachoendelea. Katika mataifa yanayowajali watu wake basi hata kama kuna tatizo basi kunakuwa na utaratibu unaoeleweka unaowawezesha watu kupangilia mipango yao. Lakini si hapa kwetu ... maana wote ni kondoo au mbuzi tu!

Hivi wataalamu wanaweza kutueleza humu jamvini ni HASARA kiasi gani inayopatikana kwa siku kutokana na huu mgao wa umeme? Kila mtu kuwasha kajenerata kake (kama anako)... hapo hakuna kujali kitu ni vyovyote umeme japo kidogo upatikane! Vipi kuhusu matumizi ya mafuta? environmental polution? Noise polution na mengine mengi? Kila mtu anatafuta namna aweze kupata japo umeme aendeleze shughuli zake!

Hapa tatizo sio Profesa Muhongo Mwongo au nani. Tunahitaji sasa mawazo mapya ya kisiasa - Kwa sababu siasa ndiyo inayoongoza mambo. Mkibahatiwa mkipata wanasiasa shupavu na wenye muono nchi inakwenda na inafika mbali sana kimaendeleo. Ila mkipata viongozi kama wa kwetu, matokeo yake ndiyo hayo… Poleni watanzania!

Mimi ni mtanzania wa kawaida sana tena asiyeshabikia siasa. Kusema ukweli WANAOTUONGOZA KWA SASA AKILI YAO IMEFIKA MWISHO. IMEZEEKA NA HATA WAKIACHIWA MIAKA MINGINE YOYOTE, HAKUNA JIPYA AKILI IMEGOTA.


HAIWEZEKANI SERIKALI NA CHAMA SERIOUS MATATIZO YA UMEME YAKAONGELEWA KWA ZAIDI YA MIAKA 10 BILA SULUHISHO. ONENI MAPUNGUFU YENU MUACHIE WATANZANIA WENGINE WALETE MAWAZO MBADALA. SERA ZA CHAMA TAWALA (MAENEO MENGI) ZIMESHINDWA. NI UKWELI HATA KAMA MTANING'OA KUCHA.
 
Tunavuna matunda ya Serikali ya CCM kwa kuwa madarakani kwa miaka hamsini halafu wanazunguka nchi nzima eti Chadema hawajafanya uchaguzi, Katiba ya Chadema ina matatizo, eti Mbowe hafai kuwa M/Kiti wa Chadema na kuendela...

Ukiwauza Mambo ya Umeme na Rasilimali za Nchi wanatokwa na Povu, na kuna makada wao kila siku utasikia jitambue eti kwa kuishabikia chama ambacho kimetufikisha hapa, Miaka saba ijayo hatutakuwa na dhahabu, Tembo watakuwa wameisha kwenye hifadhi maana ndugu zao waachina wamewapa sumu ambayo akipewa tembo penzo zinanyofoka tu bila kutumia nguvu sana.

Bado wanasema tujitambue, kuna mavuvuzela kibao yanazunguka nchi nzima eti kuelimisha wananchi waichague CCM kwa lipi???

Elimu wameiuwa, Afya hakuna Kitu, Nishati na Umeme tabu huku Gesi inachukuliwa bure.


Halafu bado unamkuta kijana wa miaka 20 anaikubali ccm na serikali yake. Mi kwa kweli hili la ccm kung'ang'ana na madaraka cjui hawajitambui ama ni nini.
 
Vipi mheshimiwa Nape Nnauye na mzee wa Tembo hawajatoa tamko la kumuuita prof.Mhongo ajieleza kwenye NEC ya CCM?
 
Ngabu vipi bana? Unafanya kama huijui bongo?
Hapa watu wanaamini mgao unaweza kwisha kwa maombi tu ya kanisani.

Na kweli lakini....

Halafu, hivi wale waganga wa kienyeji wanaoweka matangazo yao kila sehemu hawawezi kweli kulipatia ufumbuzi hili tatizo la umeme?
 
But seriously, hivi kuna mtu aliamini kweli mgao sasa utakuwa historia?
Hata kwa mtutu nisingeamini na nitaendelea kutoamini iwapo tutakuwa na viongozi hawa wanaotumia VX v8 kutoka masaki hadi Posta ilhali wajawazito wakitumia bajaji na baiskeli kufuata kujifungua km 20 away.
 
Hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme. Kama huamini rudia tena mawazo haya hadi ujishawishi kuwa unachoshuhudia ni kitu kingine zaidi ya mgao wa umeme. Kwanini hakuna mgao wa umeme? Kwa sababu walisema hakutakuwepo mgao wa umeme tena, mgao wa umeme utakuwa historia. Kwa hiyo kinachotokea ni historia tu ya mgao wa umeme ulivyokuwa; wanatumia nafasi hii kuwakumbusha historia ya mgao wa umeme msije mkasahau.

Na hakuna namna nzuri ya kuwakumbusha watu kuhusu tukio la nyuma kama kwa kutumia 'mfano halisi'. Kwa hiyo, wale waliokuwa wamesahau au ambao hawajui mgao basi hii ni namna nzuri ya kukumbuka. Hiki ndicho alichokisema Waziri Yule kuwa mgao wa umeme utakuwa ni "historia".


tatizo mkuu unafikiri mgao ni fact, siyo ni mtizamo kutegemea umesimama wapi
 
Kinachoendelea sio mgao wa umeme, ni economic sabotage. Songosongo/PAT wanahujumu uchumi.

Kuzima mitambo ya umeme kwa siku 10 kwa kisingizio cha kusafisha visima ni uhuni uliopitiliza na inaonesha ni jinsi gani Songosongo/PAT wanavyodharau Tanzania.

Ingekuwa ni huko kwao, hawa wawekezaji wamezima mitambo kwa dakika 10 (sio siku 10) kuna watu wangepoteza kazi, na wangetozwa faini kwa kila dakika ambayo mitambo itakuwa imezimwa.

Lakini hapa Tanzania, kwa sababu wanaona ni nchi wa wendawazimu wanazima kwa siku 10 na bado wanaendelea kunywa whisky zao bila shida! Biashara za watu zimesimama, nani atawafidia?

Tanesco nao walivyobobea kwenye uzembe, hata ratiba ya mgao hawajatoa.

Hivi Baraza la mawaziri wakikutana huwa wanaongea nini maana mambo kama haya yanayotekea sasa hivi yanatia aibu na yanagharimu uchumi wa nchi. Wabunge nao ndio hivyo tunaambiwa wanazunguka dunia kwa kodi ya watu hawa hawa ambao wamekaa kwenye giza! Dhulma!
Nyie si mnaweza kuwekeza kwenye Juicy tu. Ila cha ajabu hizo juicy hazijawahi kuwa na mgawo. Huyu Profesa amekuja kudhalilisha sana jina la Profesa, hana tofauti na yule maji mafupi

 
Zamani nikisikia mtu ni Profesa huwa namchukulia sio mtu wa kawaida.
Nilikuwa naamini upeo wao ni hali ya juu sana. Kamwe hawafanyi upuuzi puuzi.
lakini tangu huyu Waziri atumikie hii nafasi na kauli zake alizokuwa anazitoa, na hivi karibuni yule mbunge wa Urambo wamefanya niwe na mtazamo tofauti kabisa na ule niliokuwa nao.
Siku hizi kuna Ma Pro-feza, si profesa.
 
Diwani wa Chama Cha Mabututu FaizaFoxy hebu njoo huku. Mi nashangaa mgao hamna wala umeme haujakatika lakini mtaa mzima ni giza totoro
 
Last edited by a moderator:
Wanasema ni bodaboda baada ya bodaboda baada ya bodaboda baada ya bodaboda...... ukiisha mgao wa umeme litakuja suala la kupandisha bei ya umeme mpaka kufikia Tsh. 332 kwa unit. Yaan mgao wa umeme utakuwa historia maana watakao weza mudu hizo gharama ni wachache na hivo wengi wataamua kurudi kwenye vibatari nahivo umeme utawatosheleza wale watakao kuwa na uwezo wa kumudu hizo gharama. Kweli umeme wa mgao utakuwa historia.
 
Mi nilidhani baada ya Profesa kuteuliwa kuwa waziri tatizo lingekwisha.

Manake huyo Profesa ni msomi, ni kichwa, mwenye kipaji maalum, na mengineyo mengi.

Sasa iweje tena leo kuna mgao? Profesa msomi atashindwaje kuleta umeme wa uhakika bana?

Haiwezekani kabisa. Hakuna mgao wa umeme Tanzania.
Mimi nimeadhirika sana na Hana marina yanayoanza na Profesa baada ya Ile issue ya Profesa wa Tabora
 
Sijaona popote ambapo huyu Profesa kakosea. Namuunga mkono, HAKUNA MGAWO WA UMEME. Hiki tunachoona ni kutufanya tusisahau kuwa tuliwahi kuwa na mgawo wa umeme tu. Profesa wetu amesoma saana hawezi kusema uongo. Kwanza alijua kuwa visima hivyo husafishwa baada ya muda fulani, najua alishajitayarisha kuzuia upungufu huo. Huyu Profesa alijua kuwa amewaahidi watanzania kuwa hatutauona tena mgawo wa umeme hivyo kama kweli huu ni mgawo, alitakiwa aje mwenyewe kwenye vyombo vya habari atuombe msamaha na kujiwajibisha mwenyewe kwa kushindwa kwake kufikia upeo wake wa kuona.
This is absurd, unculth, and unspeakable. Angekuwa na hofu ya utu kidogo tu asingeweza kuwatukana Watanzania kama anavyo fanya leo. Ati anatutishia atarudi kwenye ofisi zake za huko ughaibuni.
Prof. I tell yu frankly, yu are nothing but only a mzigo to Tz.
Kwaheri.
 
Mi nilidhani baada ya Profesa kuteuliwa kuwa waziri tatizo lingekwisha.

Manake huyo Profesa ni msomi, ni kichwa, mwenye kipaji maalum, na mengineyo mengi.

Sasa iweje tena leo kuna mgao? Profesa msomi atashindwaje kuleta umeme wa uhakika bana?

Haiwezekani kabisa. Hakuna mgao wa umeme Tanzania.
Mimi nimeadhirika sana na Haya majina yanayoanza na Profesa baada ya Ile issue ya Profesa wa Tabora, ni mtazamo tu.
 
Mi nilidhani baada ya Profesa kuteuliwa kuwa waziri tatizo lingekwisha.

Manake huyo Profesa ni msomi, ni kichwa, mwenye kipaji maalum, na mengineyo mengi.

Sasa iweje tena leo kuna mgao? Profesa msomi atashindwaje kuleta umeme wa uhakika bana?

Haiwezekani kabisa. Hakuna mgao wa umeme Tanzania.

Mkuu NN

Hapa waziri Muhongo anajaribu kuthibitisha ukweli wa alichokisema kuwa sisi watanzania ni "WAVIVU WA KUFIKIRI" Watanzania wengine hapa huenda wakafikiri kuwa huu ni MGAO WA UMEME wakati tunakumbushwa HISTORIA as Mzee Mwanakijiji alivyosema.
 
Back
Top Bottom