Hakuna Mgao wa Umeme Tanzania...

Hakuna Mgao wa Umeme Tanzania...

Mzee Mwanakijiji,una maoni gani na hii power crisis tangu Jk aingie madarakani?unafikiri ni uzembe tu,matokeo ya uzembe fulani huko nyuma,economic sabotage(mnyukano wa mafisadi),kutengeneza mazingira ya ufisadi present na ujao au nini?nauliza hivi kwa kuwa siamini kama wasomi walioko serikalini wanaweza kuendesha mambo kijinga hivi!hainiingii akilini kama huu ni uzembe tu!
 
Last edited by a moderator:
Hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme. Kama huamini rudia tena mawazo haya hadi ujishawishi kuwa unachoshuhudia ni kitu kingine zaidi ya mgao wa umeme. Kwanini hakuna mgao wa umeme? Kwa sababu walisema hakutakuwepo mgao wa umeme tena, mgao wa umeme utakuwa historia. Kwa hiyo kinachotokea ni historia tu ya mgao wa umeme ulivyokuwa; wanatumia nafasi hii kuwakumbusha historia ya mgao wa umeme msije mkasahau.

Na hakuna namna nzuri ya kuwakumbusha watu kuhusu tukio la nyuma kama kwa kutumia 'mfano halisi'. Kwa hiyo, wale waliokuwa wamesahau au ambao hawajui mgao basi hii ni namna nzuri ya kukumbuka. Hiki ndicho alichokisema Waziri Yule kuwa mgao wa umeme utakuwa ni "historia".

Mkuu Mwanakijiji,
Waziri Muhongo alidai kuwa sisi watanzania ni WAVIVU wa KUFIKIRI.....sasa na hili nalo wengi watafikiri kuwa huu ni MGAO WA UMEME wakati Muhongo na TANESCO yake wanajaribu kutukumbusha HISTORIA kuhusu umeme. Huenda Muhongo aka-prove kuwa yuko right as watanzania wengi ni wavivu wa kukumbuka juu ya statements zake kuhusu mgao wa umeme kuwa historia.
 
Mi nilidhani baada ya Profesa kuteuliwa kuwa waziri tatizo lingekwisha.

Manake huyo Profesa ni msomi, ni kichwa, mwenye kipaji maalum, na mengineyo mengi.

Sasa iweje tena leo kuna mgao? Profesa msomi atashindwaje kuleta umeme wa uhakika bana?

Haiwezekani kabisa. Hakuna mgao wa umeme Tanzania.
Hebu fafanua hapo kwenye red.
Nadhani huyu jamaa ni academician na sio mtendaji mzuri
 
Hebu fafanua hapo kwenye red.
Nadhani huyu jamaa ni academician na sio mtendaji mzuri

Kwa nini unadhani si mtendaji mzuri? Maana hili tatizo halijaanza na yeye. Yeye kalikuta tu.

Kwa hiyo ina maana miaka yote hiyo ambapo tatizo limekuwepo watendaji wa hiyo wizara ndo si wazuri?
 
Kwa nini unadhani si mtendaji mzuri? Maana hili tatizo halijaanza na yeye. Yeye kalikuta tu.

Kwa hiyo ina maana miaka yote hiyo ambapo tatizo limekuwepo watendaji wa hiyo wizara ndo si wazuri?

Kama amelikuta tatizo alitakiwa atafute solutions na sio kuendelea kulifuga na kulichekelea tatizo.

Kama watendaji wa wizara hiyo sio wazuri basi alitakiwa a-clean up the house and get things in order
 
Mi nilidhani baada ya Profesa kuteuliwa kuwa waziri tatizo lingekwisha.

Manake huyo Profesa ni msomi, ni kichwa, mwenye kipaji maalum, na mengineyo mengi.

Sasa iweje tena leo kuna mgao? Profesa msomi atashindwaje kuleta umeme wa uhakika bana?

Haiwezekani kabisa. Hakuna mgao wa umeme Tanzania.

Mkuu umenikumbusha kauli za mashabiki wake alipoteuliwa kuwa Waziri wa Nishati na Madini!
 
Kama amelikuta tatizo alitakiwa atafute solutions na sio kuendelea kulifuga na kulichekelea tatizo.

Kama watendaji wa wizara hiyo sio wazuri basi alitakiwa a-clean up the house and get things in order

Waliomtangulia walishindwa. Yeye ana utofauti gani hadi aweze kufanya yaliyowashinda wengine?

Au yeye ndo alitakiwa awe deus ex machina?
 
Waliomtangulia walishindwa. Yeye ana utofauti gani hadi aweze kufanya yaliyowashinda wengine?

Au yeye ndo alitakiwa awe deus ex machina?
Kama hana tofauti na waliopita na hakuna yoyote atakaeweza kuja na suluhisho la kudumu (including yeye Mr Muhogo) basi hiyo wizara nzima inabidi ivunjwe tujue moja. Sababu ni mzigo kwa walipa kodi
 
Kama hana tofauti na waliopita na hakuna yoyote atakaeweza kuja na suluhisho la kudumu (including yeye Mr Muhogo) basi hiyo wizara nzima inabidi ivunjwe tujue moja. Sababu ni mzigo kwa walipa kodi

Mark my words. Hilo tatizo haliwezi kupatiwa ufumbuzi in either mine or your lifetime.

And I stand to be proven wrong.
 
Hata kwa mtutu nisingeamini na nitaendelea kutoamini iwapo tutakuwa na viongozi hawa wanaotumia VX v8 kutoka masaki hadi Posta ilhali wajawazito wakitumia bajaji na baiskeli kufuata kujifungua km 20 away.

Wewe ni GT wa JF!
 
Mark my words. Hilo tatizo haliwezi kupatiwa ufumbuzi in either mine or your lifetime.

And I stand to be proven wrong.
Kwa maana hiyo Mr January Makamba na ile report yake ya kuutokomeza mgawo niliyoiona hapa jamvini jana ni uzushi mtupu?
 
Haa! mgao gani tena?
Nilimsikia waziri Muhongo akisema baada ya miaka miwili tutauza umeme nchi za jirani kwasababu tutakuwa na ziada.Hivi tutauza mgao au umeme? Miaka 2 ni mwaka 2015! kama tuna mgao sasa ina maana tutakuwa na ziada miezi 24 ijayo!!
 
Kwa maana hiyo Mr January Makamba na ile report yake ya kuutokomeza mgawo niliyoiona hapa jamvini jana ni uzushi mtupu?
Kwa Tanzania unaweza kusikia tangazo la kurusha satellite kwenda Mars Feb 5 2014, siku ya maazimisho.
 
Kama hana tofauti na waliopita na hakuna yoyote atakaeweza kuja na suluhisho la kudumu (including yeye Mr Muhogo) basi hiyo wizara nzima inabidi ivunjwe tujue moja. Sababu ni mzigo kwa walipa kodi
Nakubaliana nawe, hadi tutakapopata mtu mwenye ubongo si 'kichwa tu'
 
Back
Top Bottom