Hakuna Mgao wa Umeme Tanzania...

Hakuna Mgao wa Umeme Tanzania...

Hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme. Kama huamini rudia tena mawazo haya hadi ujishawishi kuwa unachoshuhudia ni kitu kingine zaidi ya mgao wa umeme. Kwanini hakuna mgao wa umeme? Kwa sababu walisema hakutakuwepo mgao wa umeme tena, mgao wa umeme utakuwa historia. Kwa hiyo kinachotokea ni historia tu ya mgao wa umeme ulivyokuwa; wanatumia nafasi hii kuwakumbusha historia ya mgao wa umeme msije mkasahau.

Na hakuna namna nzuri ya kuwakumbusha watu kuhusu tukio la nyuma kama kwa kutumia 'mfano halisi'. Kwa hiyo, wale waliokuwa wamesahau au ambao hawajui mgao basi hii ni namna nzuri ya kukumbuka. Hiki ndicho alichokisema Waziri Yule kuwa mgao wa umeme utakuwa ni "historia".

Unajitekenya mwenyewe unacheka mwenyewe.

Unajuwa maana ya utakuwa? unajuwa miradi mingapi ya umeme ambayo inatekelezwa kwa sasa?

Nilikwambia wewe huku hapakufai wewe panakufaa kwenye udaku na ufataani.
 
Mgao huu unathibitisha Tanesco na washauri wetu wote wa nishati ni wajinga na mambumbu
Hawafanyi kazi zao kitaalamu bali waoo tu kazi yao kubwa ni washa na zima .
Tulioo anza kuzalisha gas tulijigamba sana kuwa suala la mgao litapubgua kwa sababu vyanzo vya kuzalisha umeme vimeongezeka
Leo tunaambiwa wenye gesi yao wanata kusafisha mitambo yao ! Hatuna cha kufanya hatuna gesi ya kuzalishia umeme kwa nini?
Wenyewe mlisema mlikua na taarifa miezi 2 kabla. Hivi gas si inasafirishwa kama petroli? Si inauzwa kila kona ya dunia? Gesi hii si inawekwa katika storage tanks kwa akiba na matumizi ya dharura?
Ina maana gesi yetu ni hand to mouth?
Kwa nini walipo ambiwa kutakuwa na service wasiweke akiba ya gesi kuzalisha umeme bila ya mgao?
Jee hizi mbio za mabomba ya mchina ya mtwara nayo stori si itakua hiyo hiyo?
Jee siku songo songo ikipata mafuriko au natural disaster si ndio tumekwisha?
Jamani gesi nayo inajengewa storage tanks na depots kama disel na petrol
Tanesco wao wanaleta gesi kutoka songas moja kwa moja hadi kwenye genereta!!! Kwa nini msiwe na akiba ?
Huu tanesco ni ujinga na hamlifanyii wema taifa bali mnaliangamiza
Garama ya kujenga deport ya kuweka gesi kwa matumizi ya mwezi mmoja haizidi 10bilion
Hata mkimpa mtu ajenge na nyie mkodi hio sehemu wapo watu watajenga

Jengine la ujinga na kuikomoa nchi si mliambiwa miezi 2 kabla kuhusu matengenezo? Kwanini msikae na hao symbion kuona kipindi hichi mnaagiza gesi kutoka nje?
Mambo yenu ya kuudhi kama vile mmepata hivo vyeti kwa kukopia tu
Hamuoneshi kama ni wataalam walobobea waliosoma sawa sawa na kujua mnachokifanya
Mnatuvuruga
Afadhali hili shirika liuzwe tu na hawa jamaa wapewe jembe wakalime
 
Mi nilidhani baada ya Profesa kuteuliwa kuwa waziri tatizo lingekwisha.

Manake huyo Profesa ni msomi, ni kichwa, mwenye kipaji maalum, na mengineyo mengi.

Sasa iweje tena leo kuna mgao? Profesa msomi atashindwaje kuleta umeme wa uhakika bana?

Haiwezekani kabisa. Hakuna mgao wa umeme Tanzania.

Ukishaingia ccm hakuna cha Kipaji maalumu wala usomi,hayo sahau kbs.Lzm uishie kuwa na akili kama za Lusinde,J. Komba, Serukamba, Mlugo, Kawambwa,Wasira, Ngeleja, Malima, Nyambari......... na wengineo, ONGEZEA
 
Hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme. Kama huamini rudia tena mawazo haya hadi ujishawishi kuwa unachoshuhudia ni kitu kingine zaidi ya mgao wa umeme. Kwanini hakuna mgao wa umeme? Kwa sababu walisema hakutakuwepo mgao wa umeme tena, mgao wa umeme utakuwa historia. Kwa hiyo kinachotokea ni historia tu ya mgao wa umeme ulivyokuwa; wanatumia nafasi hii kuwakumbusha historia ya mgao wa umeme msije mkasahau.

Na hakuna namna nzuri ya kuwakumbusha watu kuhusu tukio la nyuma kama kwa kutumia 'mfano halisi'. Kwa hiyo, wale waliokuwa wamesahau au ambao hawajui mgao basi hii ni namna nzuri ya kukumbuka. Hiki ndicho alichokisema Waziri Yule kuwa mgao wa umeme utakuwa ni "historia".

1458692_10153495617100508_800407691_n.jpg
 
Mengi hakukosea kusema Prof. apelekwe milembe
 
Ukishaingia ccm hakuna cha Kipaji maalumu wala usomi,hayo sahau kbs.Lzm uishie kuwa na akili kama za Lusinde,J. Komba, Serukamba, Mlugo, Kawambwa,Wasira, Ngeleja, Malima, Nyambari......... na wengineo, ONGEZEA

Mwigulu,lukuvi,Sendeka,zPinda aka wapigwe tu.
 
Mzee Mwanakijiji,una maoni gani na hii power crisis tangu Jk aingie madarakani?unafikiri ni uzembe tu,matokeo ya uzembe fulani huko nyuma,economic sabotage(mnyukano wa mafisadi),kutengeneza mazingira ya ufisadi present na ujao au nini?nauliza hivi kwa kuwa siamini kama wasomi walioko serikalini wanaweza kuendesha mambo kijinga hivi!hainiingii akilini kama huu ni uzembe tu!

Maoni yangu ni yale yale ya kila siku; kinachotokea katika Tanzania kwenye sekta yoyote ile - nishati ni mojawapo - ni kushindwa kwa sera mbovu za CCM. It is as simple as that. Watu hawaamini wanafikiria wakibadilisha watu basi sera hizo zitaweza kuanza kutekelezeka! Na wanasubiri watu wabadilihwe mambo ni yale yale. Hakuna RAis ambaye angeweza kutatua tatizo la nishati kama Kikwete; alikuwa Waziri wa NIshati mwanzoni mwa miaka ya tisini!
 
Mi nilidhani baada ya Profesa kuteuliwa kuwa waziri tatizo lingekwisha.

Manake huyo Profesa ni msomi, ni kichwa, mwenye kipaji maalum, na mengineyo mengi.

Sasa iweje tena leo kuna mgao? Profesa msomi atashindwaje kuleta umeme wa uhakika bana?

Haiwezekani kabisa. Hakuna mgao wa umeme Tanzania.

Yawezekana kabisa kuwa Profesa alikuwa sahihi, ila sasa kwa sababu za kiufundi, umetokea mgao wa dharula kwa sababu ambazo ni genuine kabisa na ambao pia hata yeye hakuutarajia, au umetengenezwa kiufundi ili aonekane kuwa na yeye anadanganya.
 
Ni kweli Muongo kasema hakuna mgao wa umeme?!
 
Hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme, hakuna mgao wa umeme. Kama huamini rudia tena mawazo haya hadi ujishawishi kuwa unachoshuhudia ni kitu kingine zaidi ya mgao wa umeme. Kwanini hakuna mgao wa umeme? Kwa sababu walisema hakutakuwepo mgao wa umeme tena, mgao wa umeme utakuwa historia. Kwa hiyo kinachotokea ni historia tu ya mgao wa umeme ulivyokuwa; wanatumia nafasi hii kuwakumbusha historia ya mgao wa umeme msije mkasahau.

Na hakuna namna nzuri ya kuwakumbusha watu kuhusu tukio la nyuma kama kwa kutumia 'mfano halisi'. Kwa hiyo, wale waliokuwa wamesahau au ambao hawajui mgao basi hii ni namna nzuri ya kukumbuka. Hiki ndicho alichokisema Waziri Yule kuwa mgao wa umeme utakuwa ni "historia".

SICHO HICHO

Hiki kilichoko sicho, hiki sicho kilichoko,
Ndicho hiki hichohicho, ndicho hiki hakiko,
Hiki ni kile si hicho, kile kisichokuwako
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya mgao!

Aliyesema hakiko, kwamba hakitakuwapo,
Yeye mwenyewe hayuko, alichosema hakipo,
Huyu bwana yuko yuko, kama popo mwenye pepo,
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya mgao!

Wanachogawa hakipo, kwani kisingekuwepo,
Ugawe vipi hakipo, hakipo huko mlipo,
Kama wafuata upepo, ndugu zangu mpo mpo,
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!

Cha nini hki cha nani, kwanini tena ni nini?
Tutamuuliza nani, kinaendelea nini?
Tunakuwa kama nyani, kujenga nyumba mtini!
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!

Tukubalini watani, janja ya jiwe ya nini?
Hili jambo siyo geni, linarudia kwa nini?
Ahadi zao jamani, twaamini kama dini!
Hakuna cha mgao, kilichoko ni historia;
Ya Mgao!

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Miaka kumi baadaye...
 
Miaka kumi baadaye...
Hivi kwa nini hakuna outrage ya kufa mtu kama ilivyokuwa kwenye Arab Spring?

Ni uoga na ujinga wa Watanzania au Watanzania wamezizoea shida na wanaona ukosefu wa huduma za msingi ni jambo la kawaida tu hivyo hakuna haja ya kukasirika?

Manake hili ni tatizo la muda mrefu sana na mpaka sasa serikali iliyopo madarakani [CCM] imeshindwa kabisa kulitatua!
 
Hivi kwa nini hakuna outrage ya kufa mtu kama ilivyokuwa kwenye Arab Spring?

Ni uoga na ujinga wa Watanzania au Watanzania wamezizoea shida na wanaona ukosefu wa huduma za msingi ni jambo la kawaida tu hivyo hakuna haja ya kukasirika?

Manake hili ni tatizo la muda mrefu sana na mpaka sasa serikali iliyopo madarakani [CCM] imeshindwa kabisa kulitatua!
Sababu ni zaidi ya moja.

1. Ujinga - mamilioni ya Watanzania hawaoni shida sana kutokuwa na umeme. Kinachofanyika viongozi huwapiga fix wananchi wajinga kwa kuwaambia umeme utapatikana baada ya muda mfupi na wananchi hawa wajinga huamini tu.

2. Woga - watu waoga kama kunguru wanaogopa virungu vya polisi hata kama hivyo virungu havipo. Ukichanganya na sababu namba 1 kila mtu anaona akae zake home kimya hata kama yupo gizani anang'atwa na mbu.

3. Kukosa umoja - wafuasi wa CCM wanaoba bora watetee viongozi wa serikali wanaofanya maamuzi ya hovyo kwasababu tu ni wanachama wenzao. Hapa sababu namba 1 na namba 2 zinachangia.

4. Kukata tamaa - watanzania hawaamini tena kama wanaweza fanya lolote tofauti na viongozi uchwara. Watu wameshakata tamaa bora kunywa uji na kulala kigazi.
 
Sababu ni zaidi ya moja.

1. Ujinga - mamilioni ya Watanzania hawaoni shida sana kutokuwa na umeme. Kinachofanyika viongozi huwapiga fix wananchi wajinga kwa kuwaambia umeme utapatikana baada ya muda mfupi na wananchi hawa wajinga huamini tu.

2. Woga - watu waoga kama kunguru wanaogopa virungu vya polisi hata kama hivyo virungu havipo. Ukichanganya na sababu namba 1 kila mtu anaona akae zake home kimya hata kama yupo gizani anang'atwa na mbu.

3. Kukosa umoja - wafuasi wa CCM wanaoba bora watetee viongozi wa serikali wanaofanya maamuzi ya hovyo kwasababu tu ni wanachama wenzao. Hapa sababu namba 1 na namba 2 zinachangia.

4. Kukata tamaa - watanzania hawaamini tena kama wanaweza fanya lolote tofauti na viongozi uchwara. Watu wameshakata tamaa bora kunywa uji na kulala kigazi.
Spot-on!
 
Back
Top Bottom