Tungelikuwa nchi makini inayosisitiza katika UWAJIBIKAJI, huyu 'bwana umeme' wa sasa, alipaswa kuwa ameshawajibika au kuwajibishwa siku nyingi sana, hasa kwa UONGO! Huyu mtu ni muongo muongo muongo unakuwa muongo kisha unaongezea na 'intellectual arrogance'.
Kama usingekuwa uongo, basi angeshawajibika kwa mambo kama haya. Anyway, acha watu kama hawa wazidi kuonesha na kudhihirisha kuwa sera za CCM zimeshindwa na zinazidi kushindwa. Wacha wazidi kuwaonesha Watanzania kuwa mabadiliko yako nje ya CCM na wakati wenyewe ni huu.
Hakuna tatizo hata moja linalosumbua Watanzania sasa hivi ambalo halina uhusiano na UFISADI wa status quo!