Hakuna jambo baya kama baba kumtegemea mwanaye

Hakuna jambo baya kama baba kumtegemea mwanaye

Jiwe anasema tufyatue watoto.... akili za kuambiwa changanya na za kwako. Ukipata mzazi wa kukujengea nyumba na kukupa elimu bila shaka huyo anajitambua sana. Na aina ya wazazi hao hawahitaji msaada wa kununuliwa chakula na watoto wao. Wanahitaji msaada wa kupelekwa hospitali kama ni wagonjwa, ama kuvalishwa nguo kama wanakiharusi nk.


Kweli kabisa. Ukiwa mzazi wa hivi unaangalia ni mtoto wako yupi amepungukiwa akili za maisha ili umsaidie baadhi ya ishu kama kusomesha watoto wake n.k. Kwani hao ndio ukoo wako wewe. Wametoka kiunoni mwako
 
Mkuu umeongea hoja nzuri lakini hakuna sehemu kwenye mada inasema watoto wasiwahudumie wazazi wao. Ninachojaribu kukieleza hapa ni kuwa sisi Wababa wa sasa tupambane kuhakikisha watoto wetu wankaa poa na kulinda siku za uzee wetu
Lakini kichwa cha habari kinasomeka "hakuna jambo baya kama wababa kuwategemea watoto wao", hapo ndipo nilipopata hofu ya kuhoji aina hii ya mafunzo ambayo kwangu niliona in kinyume kabisa na mafundisho, ila yote kwa yote naunga mkono hoja ya kututaka wazazi Wa sasa tupambane ili tuweze kujenga familia bora zitakazokuwa na uwezo wa kupambana na changamoto za maisha ya sasa na baadae na hii itatufanya kuwa na haki ya kudai maziwa kwa ng'ombe uliemlisha.
 
Wanalalamika kuwasaidia wazazi wao huku wanahonga mademu, pumbavu kabisa!
You have nailed it Madam! Halafu bila haya mtu mzima mwenye akili timamu
anakaa chini anaandika thread ya kukashfu wazazi wanaotegemea vijana wao. Sasa unataka mzazi wako akawe ombaomba mitaani? Pumbavu squared.
 
Lakini kichwa cha habari kinasomeka "hakuna jambo baya kama wababa kuwategemea watoto wao", hapo ndipo nilipopata hofu ya kuhoji aina hii ya mafunzo ambayo kwangu niliona in kinyume kabisa na mafundisho, ila yote kwa yote naunga mkono hoja ya kututaka wazazi Wa sasa tupambane ili tuweze kujenga familia bora zitakazokuwa na uwezo wa kupambana na changamoto za maisha ya sasa na baadae na hii itatufanya kuwa na haki ya kudai maziwa kwa ng'ombe uliemlisha.


hofu lazima uwe nayo kwa Muktadha wa kichwa cha Habari. Lakini ukweli ni kuwa mtoto anapaswa awaheshimu wazazi wake hiyo ndiyo Torati. Mzazi lazima ahangaike kwa manufaa ya mwanae. Ni kama serikali lazima ijitahidi kuhakikisha inaweka miundo mbinu bora watoto(Wananchi) ili waweze kuendesha maisha yao. Jukumu la watoto ni kuitii tuu na kutoa kodi ambayo ni kidogo tu.

Hata Mungu kabla ya kukuumba alikuwekea miundombinu yote ili ukija utanue tuu. Uamue nini ufanye na nini usifanye. Badae anakutaka utoe Zaka na Sadaka kama sehemu ya shukrani. Ndivyo ilivyo kwa wazazi wetu. Lazima tulipe fadhil
a kwa wazazi
 
You have nailed it Madam! Halafu bila haya mtu mzima mwenye akili timamu
anakaa chini anaandika thread ya kukashfu wazazi wanaotegemea vijana wao. Sasa unataka mzazi wako akawe ombaomba mitaani? Pumbavu squared.
Nyie ndio wale mnaoamini kuwa hamna undugu na mke. Mmewe akifariki basi anyang'anywe mali zote na kufukuzwa.
 
You have nailed it Madam! Halafu bila haya mtu mzima mwenye akili timamu
anakaa chini anaandika thread ya kukashfu wazazi wanaotegemea vijana wao. Sasa unataka mzazi wako akawe ombaomba mitaani? Pumbavu squared.


Nimekukashifu wewe usiyetumia ujana wako vizuri kujijenga na kuwekeza ili baadae uanze kusumbua watoto
 
Mm ni
Mkuu umeongea vizuri sana. Mungu hawezi kujipinga hata siku moja. Biblia inasema "Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, kabla hazijaja siku mbaya ukasema sina raha katika haya". Kumkumbuka Mungu siku za ujana ni kushika sheria zake moja wapo ni kufanya kazi kwa bidii ukimcha Mungu. Ukimkosea Mungu Ujanani subiri uzeeni utamuelewa vizuri.

Lazima watu tufanye kazi jamani
mm ni mfano wa haya,ninaye baba ila kastaafu ss ila alikuwa na kazi nzuri,ila playboy kwa sana tupo kama 13 hakuhangaika na watoto wake coz aliwadump kwa mama zao,ss hv analima mihogo huku analalamika watoto hawamjali.just imagine
 
Ukiona unaombwa pesa na huyo baba jinga jua anatambua kuwa wewe mwanae ni baba jinga unayesubiri mda kufika,ukishaona upo kwenye mfereji huu jitafakari mara mbili namna ya kutoka katika mfumo huu,na sio kulalama.Mzazi ambaye alijipanga vizuri atatamani sana kuona ukifanya vitu vya maendeleo na wala hana tabia ya kuomba pesa.
Ila naomba kukushauri kuwa katika maisha ya duniani some shit happens,kama vile kuhujumiwa,kutapeliwa,majanga kama vile moto,mafuriko na kadhalika,kwa hiyo mtoa mada we cant judge all fathers kama ulivyo generalize""baba jinga"",and some time watoto wajinga sana sana hawa wa sasa hivi ambao wanasomea kwenye simu,na kwenye shule zisizokuwa na mitaala rasimi,wanaweza waka misuse rasilimali zote za baba,au hata ikitokea familia ikawa na msukosuko wa ndoa ;watoto wanaweza kushirikiana na mama yao kuhujumu mali ya baba yao.
Swala la ubaba lina maana sana,maana unapokuwa baba unakuwa umezaa mpaka wake za wanao wa kiume,au baba wa wanaume ,walio oa wanao wa kike,kwa hiyo hili swala sio la kuliendea kimchezo mchezo,ndo maana ikitokea baba akatokea amehujumiwa,au kuwekwa chini ya mufilisi,the only solution ni ku-officialise suicide ili kuepuka fedheha kama hizi za huyo mtoa mada.
 
Mm ni

mm ni mfano wa haya,ninaye baba ila kastaafu ss ila alikuwa na kazi nzuri,ila playboy kwa sana tupo kama 13 hakuhangaika na watoto wake coz aliwadump kwa mama zao,ss hv analima mihogo huku analalamika watoto hawamjali.just imagine


Alizembea mwenyewe. Lakini katika bajeti yako sharti bajeti ya wazazi iwepo.

Kwa Mtu mwenye kipato cha laki 600000/=
10% Zaka 60,000/=
5% Sadaka 30,000/=
10% Wazazi 60,000/=
40% Maendeleo 240,000/=
5% Akiba 30,000/=
5% Misaada 30,000/=
20% matumizi 120,000/=
5% Mengineyo 30,000/=
Jumla 600000/=
 
Back
Top Bottom