Hakuna jambo baya kama baba kumtegemea mwanaye

Hakuna jambo baya kama baba kumtegemea mwanaye

Pia hata sisi kama tunao uwezo wa kuwapiga tafu watoto wetu sio mbaya
Hata kwa wajukuu zetu kama tutakuwa na huo uwezo

Na kama ukifikiri kwa makini utagundua hata wazazi wetu walitamani sana na kujitahidi ili hata tukija kukwama kimaisha watusaidie


Kweli wapo waliotamani na kujitahidi kufanya wajibu wao. Ila wapo pia waliokimbia majukumu yao, wapo waliotegea majukumu yao na kukimbizana na ulimwengu
 
Utapinga lakini ukweli uko palepale kwamba Afrika kwa ujumla kuna kundi kubwa la vijana wanakua ilihali serikali karibia zote wala hazioni hili


Si kweli na nina pinga vikali!
Kila kitu kinakuja na mbinu zake, acha uvivu wa ubunifu wa mbinu mbali mbali za maendeleo walahi!
Aamka kijana mdogo na ujue kila unacho kiwaza kitakupata wewe na uzao wako tu walahi!
 
Haya masuala ya extended family yanaleta sana umaskini. Umepata kikazi utaona ndugu, jamaa .mpaka wazazi wanakutegemea. Unahangaika nao ukija kushtuka huna ulichofanya. Baadae wanaanza kukucheka .mara jamaa alikua na kazi nzuri hana kitu. Shida sana
Hii inatokea sana. Hasa hapo kwenye kukucheka ama kucheka wanao unapokuwa umetangulia mbele ya haki mapema.
 
Huna lolote zaidi ya roho MBAYA tu. Mzee asiyejiweza kule kijijini aliyewekeza kila kitu cha thamani maishani mwake kulea toto lenye majivuno na jeuri dizaini yako anakuwa na msaada gani zaidi ya wale aliowakuza? Kumbuka sio Ulaya hapa ambapo wazee wanatunzwa na gharama za serikali.
 
Mtoa mada asante mkuu uko vzr..! Kupitia hii mada nimegundua kuna watu wako smart sana... Nasikitika baadhi wana ufikiri hafifu.... Thnx to God Ujumbe umefika panapohusika


Mkuu Kuna watu wanadhani siwapendi wazazi wangu, wengine wanadhani huenda mapembe yamekuwa baada ya mimi kukua. Jambo ambalo si kweli. Mada hii inatuasa sisi kama vijana tuwe chachu na role model wa watoto wetu. Watoto kwa sehemu kubwa huiga wazazi wao. Endapo Baba/Mama utakuwa mvivu ukiwa kijana hii itapelekea na watoto warithi tabia hiyo hiyo.

Siku hizi kuna mashamba ya laki mbili, tatu na kuendelea. Lakini mtu mpaka anafikisha miaka 30 hana hata shamba wakati huo huo amewahi kumiliki simu zaidi ya kumi zenye thamani ya laki nane mpaka milioni moja. Akifikisha miaka 50 hana hata cha kusimulia zaidi ya kusimulia ujinga. Mara enzi hizo wadada walinikoma, sijui wanaume nilikuwa nabadilisha. Upuuzi mtupu. Mara Bar zote zilikuwa zinanijua.

Sijui kama naeleweka lakini
 
Kwa mtazamo wangu,

Hua ni msomaji wa vitabu vyote ninavopata vya dini, kuanzia Biblia, Quran, Torah (torat) na hata vya Monks. Na ni mpenzi wa vitabu vya falsafa na siasa.

Nashukuru kwa kunisaidia mwandishi kwa kuweka vipande vya Biblia katika uzi wako.

Ningependa kuwakumbusha haya machache ambayo niliyakuta katika Quran kuhusu wazazi (Yani Baba Na Mama)

Sura ya 17: 23... Inasema hivi "Na mungu wenu amewa amrisha msimuabudu yoyote isipokua yeye tu, na fanyeni wema kwa WAZAZI wenu. Na kama mmoja ama wote wawili (WAZAZI) wamefikia umri wa UZEE (wamezeeka) basi msi wasimange na wala msi wakemee kwa hasira, wala msiwaambie aaarghh, ongeeni nao kwa wema na upole"


Mama kakubeba miezi 9 kwa shida tumboni mwake, na kakuzaa kwa machungu makali sana, Baba kakulea kwa shida mpaka umekua mtu mzima (pengine kakusomesha mpaka chuo).

Sasa, hizi ndio fadhila za mema waliotufanyia wazazi toka tulipokua wadogo, tuwalipe kwa kuwaita majina machafu kama hili la "BABA JINGA" ????????
Kusaidia wazazi ni jambo jema. Lakini mzazi kutotayarisha maisha yake akitegemea kusaidiwa na watoto siku moja ni ujinga pia. Namwomba Mungu anisaidie nijitegemee wakati wa uzee wangu. Kama ni msaada uwe wa kunibeba toka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kama hali ya mwili itakuwa hainiruhusu siyo msaada wa kunipa pesa ya chakula.
 
Huna lolote zaidi ya roho MBAYA tu. Mzee asiyejiweza kule kijijini aliyewekeza kila kitu cha thamani maishani mwake kulea toto lenye majivuno na jeuri dizaini yako anakuwa na msaada gani zaidi ya wale aliowakuza? Kumbuka sio Ulaya hapa ambapo wazee wanatunzwa na gharama za serikali.


Ushasema kawekeza kwangu kwa nini asile alichowekeza. Huwezi vuna usipopanda hiyo ni kanuni katika mfumo wa maisha. Asiyefanya kazi na asile.

Kama umefika kidato cha nne huwezi shindwa elewa mantiki ya mada hii. Lakini kama madarasa ni machache huwezi kunielewa.
 
. Wakati wewe ukifanya hayo ukifikiri ndio maisha wenzako wananunua hekari tatu kwa laki tisa. Baada ya miaka ishirini unashangaa wanamiliki si chini ya heka 50 unaona kama waliiba pesa kumbe ni akili.

wapi huku mkuu hekari3 kwa laki 9
 
Kusaidia wazazi ni jambo jema. Lakini mzazi kutotayarisha maisha yake akitegemea kusaidiwa na watoto siku moja ni ujinga pia. Namwomba Mungu anisaidie nijitegemee wakati wa uzee wangu. Kama ni msaada uwe wa kunibeba toka sehemu moja kwenda sehemu nyingine kama hali ya mwili itakuwa hainiruhusu siyo msaada wa kunipa pesa ya chakula.


Mkuu umeongea vizuri sana. Mungu hawezi kujipinga hata siku moja. Biblia inasema "Mkumbuke Muumba wako siku za ujana wako, kabla hazijaja siku mbaya ukasema sina raha katika haya". Kumkumbuka Mungu siku za ujana ni kushika sheria zake moja wapo ni kufanya kazi kwa bidii ukimcha Mungu. Ukimkosea Mungu Ujanani subiri uzeeni utamuelewa vizuri.

Lazima watu tufanye kazi jamani
 
. Wakati wewe ukifanya hayo ukifikiri ndio maisha wenzako wananunua hekari tatu kwa laki tisa. Baada ya miaka ishirini unashangaa wanamiliki si chini ya heka 50 unaona kama waliiba pesa kumbe ni akili.

wapi huku mkuu hekari3 kwa laki 9


Mkuu mbona sehemu nyingi tuu Hapa Tanzania. Nenda Morogoro ndani ndani. Nenda Songea huko, Sehemu ni Nyingi sana.
 
kama ndiyo tayari imeshatokea wazazi wanakutegemea utafanyaje??
Kama wazazi tayari wanakutegemea, endelea kuwasaidia. Lakini hakikisha kuwa unajiandaa wewe mwenyewe kukata mnyororo wa utegemezi kwa watoto wako. Usipowategemea watoto watoto wako na wao hawatawategemea watoto wao.
 
Mkuu Baba ni mfano wa Mungu. Anapooa tayari anajua Mke wake atakula nini, atavaa nini na mambo mengine. Atakapo hitaji watoto tayari ameshajiseti kuwa hao watoto wataishi vipi iwe kwa kula, kuvaa na mambo mengine. Mzazi kuzaa watoto wengi si kigezo cha yeye kuwategemea watoto wake uzeeni kiuchumi.

Hata Mungu kabla hajakuumba amekuwekea Fursa nyingi ili ukizaliwa unaamua ufanye ipi. Ukiamua kuwa mkulima utajua mwenyewe, ukiamua kuwa mwindaji, mfugaji, mhubiri, mfanyabiashara ni wewe tuu. Embu fikiria kama Mungu angetuumba bila kuwepo Ardhi unafikri maisha yangekuwaje? Bila kuwepo maji. Mungu ni Baba anayetutegemea katika kusimamia huu mradi wake hapa duniani. Hahitaji chochote zaidi ya usimamizi mzuri. Ndivyo hata sisi tunavyotakiwa kufanya kama Baba huku duniani. Tuandae miradi mingi kusudi watoto na wajukuu waamue nini wafanye kupitia miradi ya Baba yao('wewe/mimi).
Sio kwa maisha haya ya kibongo maana wazazi wengi wangefata hayo wengine tusingezaliwa.

Wazazi wengi walichojitahidi ni kuwaachia watoto nyumba na elimu basi. Na wazazi wakibakia na Maisha duni ya uzeeni kutokana na nguvu nyingi wametumia kusomesha watoto na ujenzi wa nyumba
 
Habari wakuu!

Mtaniwia radhi kwa maneno makali na machungu nitakayoyatoa hapa. Lengo ni kuweka mambo sawa na kutufanya tujiandae mapema.

Hakuna jambo baya kama Baba kumtegemea Mtoto. Ni jambo la aibu tena aibu kubwa sana. Ni dalili ya laana na kuendekeza ujinga katika jamii. Ni fedheha kubwa sana Baba kumtegemea mtoto kiuchumi.

Baba bora ndiye huamua kwa kiasi kikubwa Future ya watoto wake. Hupigana kufa na kupona ili watoto wake watimize ndoto zao. Zamani kidogo Baba ndiye humsaidia mtoto wake wakiume kutafuta maisha kwa kumuongezea mtaji. Kama haitoshi Baba ndiye huhusika kwa asilimia mia moja katika ishu ya Kutoa Mahari kwa kijana wake. Hii ni kutokana na kuwa Kijana wake anaenda kuongeza ukoo wake.

Biblia inatuambia kuwa Mzazi mwema ni yule anayeacha urithi kwa watoto wake hata vizazi vitatu. Andiko hili linatoa chachu na ari kwa wanaume kufanya kazi kwa bidii kusudi wawapatie watoto na wajukuu wao urithi mwema. Pia maandiko hayo hayo matakatifu yanatuambia "Heri mtu asiyeamini kuliko yule ashindwaye kuhudumia watu wa kwao" Huyo ni paulo.

Hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la Baba Jinga. Baba wenye kutoa sababu lukuki pindi linapokuja suala la majukumu yao. Wababa wengi wanakimbia majukumu yao. Kijana unayesoma sasa hivi ikiwa unamawazo ya kusaidiwa na watoto wako uzeeni ujue upo kwenye kundi la Baba Jinga. Hujui thamani ya jina "Baba".

Watu wengi hutegemea watoto wao. Huu ni ujinga na kuendekeza uvivu usiovumilika. Ujana wote unashindia pombe, unavaa nguo za gharama, unatembelea magari mazuri bila kuwekeza alafu uzeeni unaanza kusumbua watoto.

Wababa wa zamani licha ya kuwa hawakuenda shule lakini walijua kuwekeza kwenye kilimo, kwenye ufugaji na mambo mengine. Ndio maana ule msemo wa Jungu kuu halikosi ukoko ulikuwa ni halisi. Lakini kwa sasa Wababa wengi wanazembea sana. Unakuta mtu hafanyi kazi akiwa kijana mwenye nguvu anaanza kukurupuka akiwa na miaka 45+ huko. Hivi uliona wapi Watu wakipanda wakati wa mavuno. Uzee ni msimu wa kuvuna kile ulichokipanda.

Kama ulipanda zinaa basi utavuna maradhi kama ya mgongo, mfumo wa mkojo, magonjwa ya zinaa. Kama uliwekeza kwenye pombe basi jiandae kisukari, Shinikizo la damu. Hapa ndipo penye lawama hapa. Unakuta unaumwa halafu hauna hela ya matibabu. Ukicheki nyuma hukuwekeza. Kazi kulia lia kwa watoto. Amini amini nakuambia Hata utoe laana ya namna ipi haiwezi kufanikiwa na wewe mwenyewe utakuwa shahidi.

Hata Biblia haimtambui Mgane kama ni sehemu ya kupewa msaada. Mwenye haki ya kupewa ofa za uzeeni ni Mjane(Bibi). Babu(Mgane) Hatambuliki kwani ni Baba yaani anamuwakilisha Mungu. Sasa kama Mungu anapewa msaada sijui kwa kweli.

Vijana tunaoenda kuwa Baba tuwekeze jamani. Maisha ni mara moja. Umri unakimbia mbaya sana. Leo miaka 25 unasema muda upo unashangaa miaka 40 hii hapa ndio unashtuka. Usipende makubwa wakati wa kutafuta. Wenzako wananunua gari nawe umo. Wenzako wananunua Iphone sijui ngapi nawe umo. Wakati wewe ukifanya hayo ukifikiri ndio maisha wenzako wananunua hekari tatu kwa laki tisa. Baada ya miaka ishirini unashangaa wanamiliki si chini ya heka 50 unaona kama waliiba pesa kumbe ni akili. Wakati wa uzee wanaweza kuwarithisha watoto mashamba. Wewe unaanza kupiga mizinga watoto ujinga tuu.

Nabii Ibrahimu aliweza kutoa mahari kwa kijana wake Isack. Lakini leo ni Wababa wangapi wangiambiwa watoe hata ng'ombe kumi tuu kama mahari watakavyoanza kushikana mashati. Ujinga ni kutegemea watoto ilihali wewe ndiwe uliwaleta duniani.

Inatakiwa uwategemee watoto kwa kuendesha miradi yako uliyowaachia ili waweze kujikimu wa na familia zao. Huku wewe ukimsubiri Israeli mtoa roho kwa shauku kubwa. Hata Israel huwaogopaga wazee wa hivi. Kwani wamevipiga vita vizuri mwendo wameumaliza na mali wamezitunza. Sula la imani sitaliongelea kwa leo.


Vijana tupambane kwa kweli kupunguza Baba Jinga.

Nawasilisha.

Povu lolote linaruhusiwa nguo zipo nyingi za kufua
Umeongea bonge la point mkuu.kingine mzazi kumlea mtoto ni lazima sio ombi
 
Kwa mtazamo wangu,

Hua ni msomaji wa vitabu vyote ninavopata vya dini, kuanzia Biblia, Quran, Torah (torat) na hata vya Monks. Na ni mpenzi wa vitabu vya falsafa na siasa.

Nashukuru kwa kunisaidia mwandishi kwa kuweka vipande vya Biblia katika uzi wako.

Ningependa kuwakumbusha haya machache ambayo niliyakuta katika Quran kuhusu wazazi (Yani Baba Na Mama)

Sura ya 17: 23... Inasema hivi "Na mungu wenu amewa amrisha msimuabudu yoyote isipokua yeye tu, na fanyeni wema kwa WAZAZI wenu. Na kama mmoja ama wote wawili (WAZAZI) wamefikia umri wa UZEE (wamezeeka) basi msi wasimange na wala msi wakemee kwa hasira, wala msiwaambie aaarghh, ongeeni nao kwa wema na upole"


Mama kakubeba miezi 9 kwa shida tumboni mwake, na kakuzaa kwa machungu makali sana, Baba kakulea kwa shida mpaka umekua mtu mzima (pengine kakusomesha mpaka chuo).

Sasa, hizi ndio fadhila za mema waliotufanyia wazazi toka tulipokua wadogo, tuwalipe kwa kuwaita majina machafu kama hili la "BABA JINGA" ????????
Kk yangu jamaa kamuongelea baba kwani wababa wengi wanajisahau sana.Mama ana special respect na itabaki hivyo.Nani kama mama?
 
Sio kwa maisha haya ya kibongo maana wazazi wengi wangefata hayo wengine tusingezaliwa.


Ndio hivyo mimi mwenyewe nimezaliwa kwa mfumo huo. Silaumu. Napambana kuhakikisha sina wakumlaumu isipokuwa anayejua kusudi langu la kuwepo Duniani.

Lakini lazima nitimize wajibu wangu kama kijana, nifanye kazi kwa bidii kwani tayari Mungu ameniahidi Baraka. Jukumu langu ni kufanya kazi kwa bidii. Kuwa na nidhamu ya pesa na kila kitu, Kuulinda muda alafu Mungu yeye anaweka baraka zake. Mungu ananitegemea sana kutimiza mipango yake katika maisha yangu. Ananitaka nishike tuu sheria zake Basi.

Nikiwa kama Joka kiumbe wa zama zangu, najitahidi kumuiga Baba yangu aliyembinguni kwa kufanya katika familia yangu.
Lazima tujitahidi, tusiwe watu wakukata tamaa kwa mambo madogo. Mwanaume lazima upambane
 
Sio kwa maisha haya ya kibongo maana wazazi wengi wangefata hayo wengine tusingezaliwa.

Wazazi wengi walichojitahidi ni kuwaachia watoto nyumba na elimu basi. Na wazazi wakibakia na Maisha duni ya uzeeni kutokana na nguvu nyingi wametumia kusomesha watoto na ujenzi wa nyumba
Jiwe anasema tufyatue watoto.... akili za kuambiwa changanya na za kwako. Ukipata mzazi wa kukujengea nyumba na kukupa elimu bila shaka huyo anajitambua sana. Na aina ya wazazi hao hawahitaji msaada wa kununuliwa chakula na watoto wao. Wanahitaji msaada wa kupelekwa hospitali kama ni wagonjwa, ama kuvalishwa nguo kama wanakiharusi nk.
 
Kk yangu jamaa kamuongelea baba kwani wababa wengi wanajisahau sana.Mama ana special respect na itabaki hivyo.Nani kama mama?


Na nimemuongelea Baba kwani yeye ndiye aliyekabidhiwa huu ulimwengu akiwepo na Mwanamke. Sasa kufeli kwingi katika huu ulimwengu chanzo ni mwanaume. Wanaume wakiamua jambo fulani liwe linakuwa.
 
Back
Top Bottom