Glenohumeral joint
JF-Expert Member
- Oct 29, 2017
- 2,055
- 2,911
Baba akizeeka mlee ...acheni kulishwa limbwata...
Baba akizeeka mlee ...acheni kulishwa limbwata...
Kama hatimizi majukumu yake ya msingi katika familia kwa aidha uvivu/Upuuzi na uzembe wanamna hiyo jina "Baba jinga" Haliepukiki.Kwa mtazamo wangu,
Hua ni msomaji wa vitabu vyote ninavopata vya dini, kuanzia Biblia, Quran, Torah (torat) na hata vya Monks. Na ni mpenzi wa vitabu vya falsafa na siasa.
Nashukuru kwa kunisaidia mwandishi kwa kuweka vipande vya Biblia katika uzi wako.
Ningependa kuwakumbusha haya machache ambayo niliyakuta katika Quran kuhusu wazazi (Yani Baba Na Mama)
Sura ya 17: 23... Inasema hivi "Na mungu wenu amewa amrisha msimuabudu yoyote isipokua yeye tu, na fanyeni wema kwa WAZAZI wenu. Na kama mmoja ama wote wawili (WAZAZI) wamefikia umri wa UZEE (wamezeeka) basi msi wasimange na wala msi wakemee kwa hasira, wala msiwaambie aaarghh, ongeeni nao kwa wema na upole"
Mama kakubeba miezi 9 kwa shida tumboni mwake, na kakuzaa kwa machungu makali sana, Baba kakulea kwa shida mpaka umekua mtu mzima (pengine kakusomesha mpaka chuo).
Sasa, hizi ndio fadhila za mema waliotufanyia wazazi toka tulipokua wadogo, tuwalipe kwa kuwaita majina machafu kama hili la "BABA JINGA" ????????
Umetoa mifano mingi kutoka ktk biblia inayowataka wazazi wasiwategemee watoto wao wakati wa uzee wao,sijui ndivyo hivyo maana hiyo biblia inavyosema mi sijui kwa kuwa si mtaalamu wa hicho kitabu. Kama hayo ndio mafunzo ya ukristo basi usichanganye watu wote kwa sababu sisi wengine sio wakristo hivyo ustupoteshee vijana wetu.Sisi ktk uislamu tunafundishwa ni wajibu Wa Mtoto kuwatunza wazazi wake na hata kor'an imeenda mbali zaidi kwa kusema ili Mtoto apate radhi za Allah inategemea sana jinsi alivyowafanyia wema wazazi wake wawili.Kwa hiyo hoja yako ungewaelekezea wakristo wenzako na si kujenerelaizi kwa sababu sisi wengine kwa mujibu wa dini yetu tunafundishwa tuwaonee huruma wazazi wetu kama wao walivyotuonea huruma na kutuvumilia wakati tulipokuwa wadogo.
Jamani tuwe makini na wazazi wetu,nisemi hivi mtoa maada hata wewe usipo msaidia Baba yako au Mama yako Mungu atawasaidia Maana waliishi kabla yako wewe kuwepo Duniani na wewe umewakuta may be wana umri wa 20+ Sasa kipindi chote hicho Nani kawalisha au kawasupport.
Cha msingi tusiwaite baba zetu majina yasiyo kuwa na Maana,angalizo tujitahidi kuwasaidia pale tunapoweza na Mungu alivyotoka kwavyo.
Madhaifu ya wazazi wetu tuwaachie wenyewe na maisha ya,Kama tumeshindwa kuwasaidia let stay quite there is no need to call them with kwa majina yasiyowabariki nice day!
mada njema sana hii"..wanaoipinga na watakaoipinga wala usiwashangae " wanapinga kwa sababu" wameathirika na mfumo wa mzazi kumtegemea mtoto"...
Yaani wamekuwa " wakielezwa hivyo"
Kwenye hii maada kuna ukweli kiasi flani, pamoja na comments za wadau wengi.
Kwa kuongezea zaidi ni seme hivi:
1. Mtoto wako ukimlea vzr na kwa mapenzi mazuri, baadae atakujali sana. Lkn kama ukiwa baba usie jua majukumu yako watoto wako hawata kujali.
2. Watoto wetu tuwa shilikishe kwenye njia za kufta pesa ili waje kuwa na nguvu za kiuchumi, hii nimesema kwasababu kuna watu wanarithi pesa na vitu vingi lkn hawa kuwa sehemu ya utaftaji kwahiyo mali hizi zina washinda na wao walikua kwa raha kwahiyo shida itakuja kwa watoto watakao jitaftia baadae.
3. Tabia za akina baba, kama vile ulevu na kuwa na vimada wengi vina katisha tamaa watoto kuwa saidia. Mtoto anaona bora hiyo hela awekeze kwenye vitu vyake.
4. Kutokana somo hili basi sisi vijana iwe funzo tuchukue hatua sitahiki kutoka sasa.
N:B Waziza hata kama walitutendea vibaya, naomba tuwa jali kadili ya uwezo wetu.
Pamoja mkuuWewe unaakili sana. Wapo watu humu wameniona kama mtu ninaye wadharau wazazi wangu. Au nisiye wapenda. Kumbe lengo la mada ni kutoa elimu kwa vijana kuwa wawapo na nguvu watafute pesa na kuwekeza kwenye mambo ya msingi yatayowasaidia huko baadae. Ukiwapa watoto wako Elimu kama ndio urithi wao, ukiwatafutia miradi ambayo baadaye kama wapo watakaoshindwa maisha ya shule basi miradi hiyo waitumie kujikimu wao na kumlea mzee wao
Kitu ambacho tunatofautiana nadhani ni misimamo ya imani zetu sikuwahi kusema kwamba wazazi wasiwajibike kwa watoto wao kama vile kuwapa matunzo bora na elimu,lakini hata kama mzazi wakati Wa ujana wake pengine kutokana nahali yake ya kipato alishindwa kumpatia elimu ya kutosha Mtoto wake bado kwa mujibu Wa Uislamu haijawa sababu ya Mtoto kumtelekeza mzazi wake. hayo mafunzo ya mtoto kumtelekeza mzazi wake ktk Dini yetu hayapo.Swala la mzazi kumtelekeza mtoto wake hiyo ni hoja nyingine tofauti na ndio maana awali nilimwambia mleta hoja kwamba mafunzo yake awape wakristo wenzake na asiwachanganye watu wote.