Hakuna jambo baya kama baba kumtegemea mwanaye

Hakuna jambo baya kama baba kumtegemea mwanaye

Ukiona unaombwa pesa na huyo baba jinga jua anatambua kuwa wewe mwanae ni baba jinga unayesubiri mda kufika,ukishaona upo kwenye mfereji huu jitafakari mara mbili namna ya kutoka katika mfumo huu,na sio kulalama.Mzazi ambaye alijipanga vizuri atatamani sana kuona ukifanya vitu vya maendeleo na wala hana tabia ya kuomba pesa.
Ila naomba kukushauri kuwa katika maisha ya duniani some shit happens,kama vile kuhujumiwa,kutapeliwa,majanga kama vile moto,mafuriko na kadhalika,kwa hiyo mtoa mada we cant judge all fathers kama ulivyo generalize""baba jinga"",and some time watoto wajinga sana sana hawa wa sasa hivi ambao wanasomea kwenye simu,na kwenye shule zisizokuwa na mitaala rasimi,wanaweza waka misuse rasilimali zote za baba,au hata ikitokea familia ikawa na msukosuko wa ndoa ;watoto wanaweza kushirikiana na mama yao kuhujumu mali ya baba yao.
Swala la ubaba lina maana sana,maana unapokuwa baba unakuwa umezaa mpaka wake za wanao wa kiume,au baba wa wanaume ,walio oa wanao wa kike,kwa hiyo hili swala sio la kuliendea kimchezo mchezo,ndo maana ikitokea baba akatokea amehujumiwa,au kuwekwa chini ya mufilisi,the only solution ni ku-officialise suicide ili kuepuka fedheha kama hizi za huyo mtoa mada.


Mkuu mbona kama umepaniki hivyo. Mzazi ni mzazi tuu bila kujali nafasi yake. Ila mada hii ipo kwa lengo kwa kuwaasa vijana wa sasa wafanye kazi na kuwekeza ili uzeeni wasipate tabu. Wawe msaada kwa watoto wao. Ikiwa itatokea dhararu kama ya kuhujumiwa, kutapeliwa, kudhulumiwa hiyo ni kesi nyingine.

Umegusia vitu muhimu sana. Ishu ya ndoa endapo Mama atathubutu kumhujumu Baba kwa kushirikiana na Watoto ujue kuna tatizo la msingi Aidha Baba unatabia ya kutapanya mali. Au hukuimudu familia yako tokea mwanzo
 
Mkuu Baba ni mfano wa Mungu. Anapooa tayari anajua Mke wake atakula nini, atavaa nini na mambo mengine. Atakapo hitaji watoto tayari ameshajiseti kuwa hao watoto wataishi vipi iwe kwa kula, kuvaa na mambo mengine. Mzazi kuzaa watoto wengi si kigezo cha yeye kuwategemea watoto wake uzeeni kiuchumi.

Hata Mungu kabla hajakuumba amekuwekea Fursa nyingi ili ukizaliwa unaamua ufanye ipi. Ukiamua kuwa mkulima utajua mwenyewe, ukiamua kuwa mwindaji, mfugaji, mhubiri, mfanyabiashara ni wewe tuu. Embu fikiria kama Mungu angetuumba bila kuwepo Ardhi unafikri maisha yangekuwaje? Bila kuwepo maji. Mungu ni Baba anayetutegemea katika kusimamia huu mradi wake hapa duniani. Hahitaji chochote zaidi ya usimamizi mzuri. Ndivyo hata sisi tunavyotakiwa kufanya kama Baba huku duniani. Tuandae miradi mingi kusudi watoto na wajukuu waamue nini wafanye kupitia miradi ya Baba yao('wewe/mimi).
Umeongea vizuri kabisa, ila hua nawashangaa watoto wengine wanapolalamika na kupiga kelele wakati baba anapojibana kwaajili ya kuwekeza miradi ili hapo baadae asiwe tegemezi kwa watoto. Watoto tusipende kulalama wakati baba akitafuta na kuwekeza tuwe wavumilivu tutakula matunda baadae.
 
Umeongea vizuri kabisa, ila hua nawashangaa watoto wengine wanapolalamika na kupiga kelele wakati baba anapojibana kwaajili ya kuwekeza miradi ili hapo baadae asiwe tegemezi kwa watoto. Watoto tusipende kulalama wakati baba akitafuta na kuwekeza tuwe wavumilivu tutakula matunda baadae.


Hhaahahahah!!
 
Mkuu mbona kama umepaniki hivyo. Mzazi ni mzazi tuu bila kujali nafasi yake. Ila mada hii ipo kwa lengo kwa kuwaasa vijana wa sasa wafanye kazi na kuwekeza ili uzeeni wasipate tabu. Wawe msaada kwa watoto wao. Ikiwa itatokea dhararu kama ya kuhujumiwa, kutapeliwa, kudhulumiwa hiyo ni kesi nyingine.

Umegusia vitu muhimu sana. Ishu ya ndoa endapo Mama atathubutu kumhujumu Baba kwa kushirikiana na Watoto ujue kuna tatizo la msingi Aidha Baba unatabia ya kutapanya mali. Au hukuimudu familia yako tokea mwanzo
umesomeka;ninayo mengi ila naona nipishe wengine.
 
Habari wakuu!

Mtaniwia radhi kwa maneno makali na machungu nitakayoyatoa hapa. Lengo ni kuweka mambo sawa na kutufanya tujiandae mapema.

Hakuna jambo baya kama Baba kumtegemea Mtoto. Ni jambo la aibu tena aibu kubwa sana. Ni dalili ya laana na kuendekeza ujinga katika jamii. Ni fedheha kubwa sana Baba kumtegemea mtoto kiuchumi.

Baba bora ndiye huamua kwa kiasi kikubwa Future ya watoto wake. Hupigana kufa na kupona ili watoto wake watimize ndoto zao. Zamani kidogo Baba ndiye humsaidia mtoto wake wakiume kutafuta maisha kwa kumuongezea mtaji. Kama haitoshi Baba ndiye huhusika kwa asilimia mia moja katika ishu ya Kutoa Mahari kwa kijana wake. Hii ni kutokana na kuwa Kijana wake anaenda kuongeza ukoo wake.

Biblia inatuambia kuwa Mzazi mwema ni yule anayeacha urithi kwa watoto wake hata vizazi vitatu. Andiko hili linatoa chachu na ari kwa wanaume kufanya kazi kwa bidii kusudi wawapatie watoto na wajukuu wao urithi mwema. Pia maandiko hayo hayo matakatifu yanatuambia "Heri mtu asiyeamini kuliko yule ashindwaye kuhudumia watu wa kwao" Huyo ni paulo.

Hivi karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la Baba Jinga. Baba wenye kutoa sababu lukuki pindi linapokuja suala la majukumu yao. Wababa wengi wanakimbia majukumu yao. Kijana unayesoma sasa hivi ikiwa unamawazo ya kusaidiwa na watoto wako uzeeni ujue upo kwenye kundi la Baba Jinga. Hujui thamani ya jina "Baba".

Watu wengi hutegemea watoto wao. Huu ni ujinga na kuendekeza uvivu usiovumilika. Ujana wote unashindia pombe, unavaa nguo za gharama, unatembelea magari mazuri bila kuwekeza alafu uzeeni unaanza kusumbua watoto.

Wababa wa zamani licha ya kuwa hawakuenda shule lakini walijua kuwekeza kwenye kilimo, kwenye ufugaji na mambo mengine. Ndio maana ule msemo wa Jungu kuu halikosi ukoko ulikuwa ni halisi. Lakini kwa sasa Wababa wengi wanazembea sana. Unakuta mtu hafanyi kazi akiwa kijana mwenye nguvu anaanza kukurupuka akiwa na miaka 45+ huko. Hivi uliona wapi Watu wakipanda wakati wa mavuno. Uzee ni msimu wa kuvuna kile ulichokipanda.

Kama ulipanda zinaa basi utavuna maradhi kama ya mgongo, mfumo wa mkojo, magonjwa ya zinaa. Kama uliwekeza kwenye pombe basi jiandae kisukari, Shinikizo la damu. Hapa ndipo penye lawama hapa. Unakuta unaumwa halafu hauna hela ya matibabu. Ukicheki nyuma hukuwekeza. Kazi kulia lia kwa watoto. Amini amini nakuambia Hata utoe laana ya namna ipi haiwezi kufanikiwa na wewe mwenyewe utakuwa shahidi.

Hata Biblia haimtambui Mgane kama ni sehemu ya kupewa msaada. Mwenye haki ya kupewa ofa za uzeeni ni Mjane(Bibi). Babu(Mgane) Hatambuliki kwani ni Baba yaani anamuwakilisha Mungu. Sasa kama Mungu anapewa msaada sijui kwa kweli.

Vijana tunaoenda kuwa Baba tuwekeze jamani. Maisha ni mara moja. Umri unakimbia mbaya sana. Leo miaka 25 unasema muda upo unashangaa miaka 40 hii hapa ndio unashtuka. Usipende makubwa wakati wa kutafuta. Wenzako wananunua gari nawe umo. Wenzako wananunua Iphone sijui ngapi nawe umo. Wakati wewe ukifanya hayo ukifikiri ndio maisha wenzako wananunua hekari tatu kwa laki tisa. Baada ya miaka ishirini unashangaa wanamiliki si chini ya heka 50 unaona kama waliiba pesa kumbe ni akili. Wakati wa uzee wanaweza kuwarithisha watoto mashamba. Wewe unaanza kupiga mizinga watoto ujinga tuu.

Nabii Ibrahimu aliweza kutoa mahari kwa kijana wake Isack. Lakini leo ni Wababa wangapi wangiambiwa watoe hata ng'ombe kumi tuu kama mahari watakavyoanza kushikana mashati. Ujinga ni kutegemea watoto ilihali wewe ndiwe uliwaleta duniani.

Inatakiwa uwategemee watoto kwa kuendesha miradi yako uliyowaachia ili waweze kujikimu wa na familia zao. Huku wewe ukimsubiri Israeli mtoa roho kwa shauku kubwa. Hata Israel huwaogopaga wazee wa hivi. Kwani wamevipiga vita vizuri mwendo wameumaliza na mali wamezitunza. Sula la imani sitaliongelea kwa leo.


Vijana tupambane kwa kweli kupunguza Baba Jinga.

Nawasilisha.

Povu lolote linaruhusiwa nguo zipo nyingi za kufua


Mbona unawapiga madongo wanaume wa Kiha, watakulaani shauri yako.

cc: Baba Diamond, Baba Kiba, Baba Dimpoz
 
Si kweli mzee akishazeeka ni jukumu la mtoto kumtunza mzazi, sema wazazi Wanatakiwa kuwapa elimu watoto wao, hata vitabu vya dini vinasema,
 
Si kweli mzee akishazeeka ni jukumu la mtoto kumtunza mzazi, sema wazazi Wanatakiwa kuwapa elimu watoto wao, hata vitabu vya dini vinasema,


Apandacho mtu ndicho avunacho
 
Haya masuala ya extended family yanaleta sana umaskini. Umepata kikazi utaona ndugu, jamaa .mpaka wazazi wanakutegemea. Unahangaika nao ukija kushtuka huna ulichofanya. Baadae wanaanza kukucheka .mara jamaa alikua na kazi nzuri hana kitu. Shida sana
Alafu usidhani WANAOMBA msaada..ni WANADAI as if ni legal right yao.. na wanakuhukumu kwa kiwango cha msaada unaowapa! Sawa tusaidiane ila tukumbuke kua mtoa msaada naye ana MALENGO na NDOTO zake!
 
Tatizo kuplan familia zetu ndo tatizo tunafyatua tuu huo Msingi utaandaaje huku una furushi la watoto 11 na benchi yupo mmoja
 
Back
Top Bottom