Ubena Zomozi
JF-Expert Member
- Jun 19, 2022
- 1,182
- 918
Usishindane na dola yoyote kwenye masuala ya uchaguzi, matokeo yake huwa yanajulikana ukifanya nao ushindani wa aina yoyote ile. Watakachokuambia kazi yako ni kutii tu bila shuruti.
vipi kuhusu uchaguzi wao wa kikabila pia tuuige?Hayo ni mapungufu kidogo sana tofauti na Tanzania ambapo mapungufu ni mengi sana
nadhani wanatakiwa kuiga uchaguzi wako wa nguo ipi ya kuvaa kila unapoianza siku mpyavipi kuhusu uchaguzi wao wa kikabila pia tuuige?
Hata huko ni hvyo Kuna watu wamekutwa na masanduku yakiwa na kura fekiBora hata Kenya huku Tanzania walikuta sanduku la kura lipo kwenye zizi la ng'ombe.
wanatumia mfumo wa biometrics kule!!Hata huko ni hvyo Kuna watu wamekutwa na masanduku yakiwa na kura feki
Kenya wote weziHabari za weeknd wakuu..!
Kwa wale tunaoendelea kufuatilia uchaguzi wa majirani zetu naomba nitangulize pole zangu za dhati kwa wote kutokana na kile kinachoendelea.
Baadhi yetu tuliposema kwamba Tume ya uchaguzi na Mipaka Kenya (IEBC) inajiandalia bomu yenyewe kwa kuruhusu media kurusha matokea ya uchagzui huo wapo wana JF walikuja na na mapambio ya media freedom.
View attachment 2323548
Wengine mlikuja na miluzi mingi ya oooh....tujifunze kwa wenzetu...mara oooh kenya baba wa demokrasia...!! Kiko wapiiii?? hadi leo IEBC wanarukaruka na sarakasi za matokeo huku pande zote TEAM BABA (ODINGA) NA TEAM HUSTLERS (RUTO) zimeshaitangaza washindi kutokana na matokeo ya vyombo vya habari ...kwanza nchekee...ha ha ahaaa.
KWA MATUKIO HAYA NDUGU ZANGU NAWAAMBIA WAMESHAFELI...TUWAOMBEE TU WASIPIGANE MAANA HAYA YANAYOENDELEA HAYATAWAACHA SALAMA NA NATHUBUTU KUSEMA TANZANIA HATUNA CHA KUJIFUNZA KATIKA UCHAGUZI WA KENYA ILA IEBC INAPASWA KUJIFUNZA KWETU.
Una ushahidi wa mapungufu mengi ya tanzaniaHayo ni mapungufu kidogo sana tofauti na Tanzania ambapo mapungufu ni mengi sana
Kwa mfumo huo matokeo yangekua tayariwanatumia mfumo wa biometrics kule!!
Hakunaga mambo ya ovyo ovyo ya akina Mahera
Uwongo mtupu, mbona mpaka sasa hawajatangaza matokeo? Kenya kuna ushindani wa ki kabila,na sio uchaguzi. Hakuna la kujifunza Kenya.Ukiwa na akili timamu, mkweli wa nafsi na asiye na unafiki, utakiri kikamilifu, bila shaka kuwa uchaguzi wa Kenya ni mfano mzuri wa pekee kwa Afrika nzima, na Asia (ukiondoa Japan, Singapore na Malaysia).
We huna akili, yaani kwenye kituo watu wamejuandisha 100,alafu Kura ziwe 1700 kwenye kituo hicho hicho,alafu useme hayo ni mapungufu madogo?!Hayo ni mapungufu kidogo sana tofauti na Tanzania ambapo mapungufu ni mengi sana
Mmmmh yaani upuuzi wa Tanzania ya ccm,unasema unafanana na Uchaguzi wa Kenya!?inawezekana Uchaguzi wa Kenya usiwe Bora kwa asilimia 100,lakini huwezi kulinganisha na upuuzi mavi wa chaguzi za Tanzania,ni bongo pekee,ambapo Kuna watu wanapita bila kupingwa!!simu haziruhusiwi kwenye vyumba vya kuhesabia kura,mgombea anapata kura nyingi kuliko idadi ya wapiga kura!!ilitokea chato hii,kwa shetani Jiwe.Nikiwa napitia katika mitandao mbalimbali ya kijamii nchini niliona baadhi ya wanaharakati, wafuasi na viongozi wa vyama vya upinzani wakidai kuwa Tanzania inapaswa kujifunza kutoka uchaguzi Mkuu wa Kenya. Wakidai kuwa uchaguzi huo ni huru na wa haki.
Kwa ufuatiliaji nilioufanya katika uchaguzi huo kwa kweli sijaona hicho kinachodiwa kuwa uchaguzi huo ni huru na wa haki. Sioni kama kuna la kujifunza kutoka katika uchaguzi huo kwa sababu zifuatazo:-
#13/08/2022 Daniel Musyoka Msimamizi wa Uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi (IEBC) aliripotiwa kutoweka na mpaka sasa haijulikani alipo.
#13/08/2022 iliripotiwa kuhusu uwepo wa dalili za wizi wa kura katika baadhi ya maeneo ambayo inadaiwa William Ruto amepata kura nyingi ambapo ilielezwa kuwa kura katika vifaa vya KIEMS hazilingani na idadi iliyopo katika Makaratasi.
#12/08/2022 iliripotiwa kuwa Maafisa wa Tume wameitisha Kikao cha Dharura baada ya sintofahamu kutokea katika Ukumbi wa kuhakiki kura za Urais, baada ya Kompyuta kuingizwa ukumbini kinyume na Taratibu.
#12/08/2022 iliripotiwa kuhusu msimamizi wa uchaguzi kukutwa na karatasi za kupigia kura katika kituo cha kuhesabia kura cha Jamhuri katika Jimbo la starehe.
#10/08/2022 iliripotiwa kuwa Polisi wawili na Raia mmoja walikutwa na karatasi za kupigia kura zenye tiki. Pia, Miongoni mwa vifaa vingine vilivyokutwa nao ni sahihi moja ya wapiga kura, Madaftari 2 ya matokeo ya Uchaguzi, pakiti mbili za karatasi za kupigia kura za Urais.
# Kubwa zaidi na la kusikitisha ni kwamba mpaka sasa Tume huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) haijatangaza matokeo ya kura za Urais pasipo sababu za msingi huku siku zikizidi kwenda hii inatilia mashaka juu ya matokeo yatakayotangazwa kama yatakuwa na uhalisia.
Katika mazingira haya, kweli watanzania wenye akili timamu wanawezaje kuishauri serikali iige kinachotokea Kenya? Ni kweli kuwa viongozi wa vyama vya upinzani wataweza kusubiri wiki nzima bila kujua aliyeshinda?.
Kitendo cha Vyombo vya habari kutangaza matokeo kiliwafanya wanaharakati pamoja na viongozi wa vyama vya upinzani kuamini kuwa kufanya hivyo ndio uhuru na haki, tujiulize hiyo haki sasa iko wapi? Hivi hamuoni kuwa mlijichanganya kuwahi kuongea bila kufukiria mwisho wa mnachokisema utakuwa nini? Kutofikiria kwenu kumewafanya mkose la kuongea baada ya hali inayoendelea kujitokeza.
Hii ni ishara ya ukosefu wenu wa uweledi katika mambo makubwa yanayohusu uongozi wa nchi.
Kwa mfumo huo matokeo yangekua tayari
Maana yake mfumo huo ni geresha tu ndiyo maana matokeo mpaka sasa hakunaUnataka kujenga hoja gani?
Kweli kabisa hata hapa tz wapo wanao kimbia madeni na kwenda nje ya nchi na wengine hufanya uhuni kibao mitaani wakiajibishwa na jamii utasikia sababu za kisiasa tu ndio zilizowaponzaHapa ni uhalifu tu. Na kama kweli umefuatlia, inadaiwa matukio ya kupotea kwa watu ktk eneo hilo ni ya kawaida. Kwahiyo hayana uhusiano na uchaguzi.
Acha kujikuna upele wenye harufu mbele za watu halafu (uchafuzi Tanzania) ukaufananisha na chunusi (uchaguzi Kenya)
Wanatumia biometric na manual system ili kuepusha udanganyifu.Maana yake mfumo huo ni geresha tu ndiyo maana matokeo mpaka sasa hakuna
Zote porojo ndugu,matokeo yalitakiwa yawe tayariWanatumia biometric na manual system ili kuepusha udanganyifu.
Na uhakiki wa kina unahitajika ili kujiridhisha chaguo la wapiga kura