Mkwepakodi,Jamani Ndugu zangu wa ukawa naomba tuweke Silaha chini tumuunge mkono mh. Raisi katika hili, hata kama kuna makosa yalifanywa na ccm siku zilizopita lakini sasa wanayarekebisha hilo ni jambo jema kwa nchi yetu, nchi kwanza siasa baadaye, wazungu wanasema hata kama umetembea umbali gani ukigundua umepotea geuka urudi ulikotoka ili ufuate njia sahihi
Hakuna mtanzania analikataa hilo la kurekebisha nchi, kinacholeta malumbano ni jinsi gani ya kukabiliana na hawa wenye nguvu zao ambao tuliwapa nchi yetu kwa kupenda wenyewe.
Hivi nikuulize,
Ni sahihi kurekebisha makosa kwa kufanya makosa?
Inahitaji mjadala, inahitaji jopo la wanasheria nguli wakae waumize vichwa vyao ili tupate upenyo wa kuponyoka mikononi mwa hawa watu.
Tukitumia "Uzalendo" zaidi bila kuchungulia wapi tumenasa na jinsi ya kujinasua basi itakuwa heri hata kuibiwa kuliko kutoibiwa.