Godbless Lema: Nimemaliza Arusha sasa nashuka Mtwara

Godbless Lema: Nimemaliza Arusha sasa nashuka Mtwara

Watu wa Arusha wamedhihirisha maana halisi ya kujitambua,na namna bora zaidi ya kusimamia misingi ya utu wa mwanadamu,Watanzania tuige mfano huu!!!
 
Ki-ufupi naweza kukubaliana kuwa mtu kama Lema ni mpango wa mungu kwa magumu yote ambayo umekuwa ukiyapitia kiukweli hadi sasa naona umepungua kamanda pole sana kwa majukumu mazito ya kuwatetea wanyonge ipo siku historia itakukumbuka na hakika ushindi wa leo unaonyesha ni kwa jinsi gani ulivyo karibu na wananchi wako kamanda kura ulizopata 56,000 ni halali mbele ya mungu. Arusha somo limeshaeleweka ukombozi uelekee sehemu nyingine pia
Nakubaliana na wewe kwenda kuwakomboa wana Mtwara nakuombea mungu akutie nguvu iwapo itampendeza urudi salama maana Mtwara kwa sasa eneo hatari mno kiusalama lakini tunawatakia hao wenzetu pia wapate ukombozi wa kweli maana hawana mtetezi
Mzee Tupa tupa nakubaliana na wewe kuwa AR magamba hamtakiwi lakini vijana wako waliopewa rungu wanafikiri wanazijua sana siasa na kupewa madaraka makubwa matokeo yake ndo hayo. Naamini mtaliona hilo katika tathmini zenu hapo Lumumba lakini kwa kuwa sikio la kufa halisikii mnaweza kujipa moyo kuwa mmmeshinda na Arusha.
Ogopa sana mtu anayeanza na mungu na kumaliza na mungu................. Giza haliwezi kushindana na nuru.

Kila la kheri makamanda.

Well well said mkuu pia naungana na wewe ktk kumtakia kila la heri
 
Hii ndo habari ya mjini,siasa za uzushi,mabomu,vitisho na ukanjanja kuleee,peopleeeeeees poweeeeeeeer!!!
 
Hongereni watu wa Arusha, kazi ni huku kwetu, mitaa ya kusini mwa Tz.
 
Hatimaye yametimia.Makamanda wa CDM kazi imefanyika,lazima tujipongeze.
Iliyobaki sasa tupewe uongozi wa jiji 'Geneva ya Africa' tupige kazi.Vijana wote wa Arusha tupo pamoja,tusikubali kugawanywa kimakabila na CCM.
Nimewakumbuka sana waliopoteza maisha kwenye mlipuko kwenye mkutano wetu CDM;Ee Mungu uwajalie pumziko la Milele.Amina.
 
shikamoo mh MBUNGE LEMA!!MARHABA MTOTO MWIGULU NCHEMBA!
 
Kijana mwenye mikakati madhubuti ya ushndi Godbless Lema, ametamka kuwa amemaliza Arusha kurudisha kata zote 4 kama zawad ya wananchi kwa Lema kurudisha Ubunge wake, sasa atamka kuwa anadondoka rasmi kuikomboa Mtwara.

Amesema Mtwara imekosa mpambanaji wa kweli mwenye kujiamini na hvyo anashuka rasmi mtwara. Chadema leo imetwaa kata zote 4 licha ya nguvu kubwa ya CCM na jesh la Polisi hadi kupelekea naibu katbu mkuu Mwigulu kupga kambi Arusha mwezi mzima. LEMA amethbitisha umwamba wake katka siasa za Arusha. Lema ni kpenz cha wanaArusha bila shaka.

Amesema CCM wajiandae Mtwara kwa kuwa anaenda na kuipatia uhuru mtwara. Kumbuka A GRAIN OF WHEAT.

kama kawaida yake lema POROJO nyingi..
 
Wana Mtwara na kusini kwa ujuma tunahitaji kuongezewa nguvu kisiasa ktk kile tulichokianza. Rejea harakati za Masasi, Liwale na Mtwara mjini. Ni wakati muafaka kwa CDM kupiga kambi mikoa ya kusini ili kuwasha moto utakaodumu tangu sasa hadi 2015 ili kuing'oa CCM.
CUF imeshawatelekeza wanaMtwara na sasa ni dhahiri tunahitaji CDM si vinginevyo. NCCR ni kama imekufa kibudu hapa Mtwara tangu tukio la kutimuliwa jukwaani kwa M/kiti wake Bw. Mbatia.
 
Back
Top Bottom