Godbless Lema aanza ziara ya kuteketeza CCM Arusha

Godbless Lema aanza ziara ya kuteketeza CCM Arusha

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema na Mbunge wa Jimbo la Arusha Godbless Lema leo ameanza rasmi kazi ya kusambaratisha CCM Arusha.

Lema ambaye ameamua kutembelea kata zote za Jimbo la Arusha kabla ya kurudi bungeni wiki ijayo leo alikuwa katika kata ya Kimandolu na Kaloleni.

Katika kata hiyo aliyoanza kutembelea tangu asubuhi amefanikiwa kuzindua mashina 12 ya CHADEMA.Akizungumza na wanachama katika maeneo hayo Lema alielezea kwa kina uonevu uliofanywa na mkuu wa mkoa Magessa Mulongo dhidi yake na CHADEMA kwa ujumla.

Wachambuzi wa siasa za Arusha wanasema mpaka kumaliza ziara hii katika kata zote Lema atakuwa ameijeruhi vibaya CCM.
 
Sio ataijeruhi ccm akimaliza ziara yake ktk kata zote hapa jijini Arusha..hiyo ccm hapa arusha ni kama haipo..huku ktk kata hata hao mabalozi walishindwa kuwapata ktk uchaguzi wao,watu walikataa.
 
Huyu jamaa bunge linaendelea yeye anazurura tu!

Nayeye ikifika wakati wa kutoa hotuba yake ya mambo ya ndani asije kuleta vituko kama vya Msigwa!!!

Lema, kaa chini uandae hotuba inayoeleweka. Acha kuzurura...
 
mbunge wa viti maalumu betty machangu akichangia mjadala wa wizara ya maliasili na utalii hivi punde ameeleza kuwa mkoa wa arusha ni wa pili kwa ulipaji na ukusanyaji kodi hapa nchini lakini hivi sasa maendeleo ya mkoa huo yanazidi kudidimia kwa sababu arusha mjini haina muwakilishi kwa sababu mbunge wake yuko bize na maandamano na siasa za vurugu kila kukicha.
 
Lema amefanikiwa kuiua kabisa CCM Arusha.
Kwa sasa karibu kila mtu Arusha anaipenda CHADEMA kwa sababu ya Harakati za Lema na makamanda wa CHADEMA.

CCM Arusha kwa sasa hawana raha kabisa.
 
Ama ataijeruhi au ataiua tusubiri akimaliza ziara tuone lipi la kweli.
 
Huyu jamaa bunge linaendelea yeye anazurura tu!

Nayeye ikifika wakati wa kutoa hotuba yake ya mambo ya ndani asije kuleta vituko kama vya Msigwa!!!

Lema, kaa chini uandae hotuba inayoeleweka. Acha kuzurura...

Tatizo unajifanya mjuaji huku ukiwa hujui kitu.Kwa taarifa yako waziri kivuli wa mambo ya ndani ni Vicent Nyerere
 
mbunge wa viti maalumu betty machangu akichangia mjadala wa wizara ya maliasili na utalii hivi punde ameeleza kuwa mkoa wa arusha ni wa pili kwa ulipaji na ukusanyaji kodi hapa nchini lakini hivi sasa maendeleo ya mkoa huo yanazidi kudidimia kwa sababu arusha mjini haina muwakilishi kwa sababu mbunge wake yuko bize na maandamano na siasa za vurugu kila kukicha.
Huyo Bety Machange ana wivu sana.
Watu wa Arusha tulimchagua Lema ili akapiganie haki zetu.
Kama kupigania haki, huyo Bety Machange anaona ni Vurugu, basi watu wa Arusha tunazipenda hizo vurugu.
 
Tatizo unajifanya mjuaji huku ukiwa hujui kitu.Kwa taarifa yako waziri kivuli wa mambo ya ndani ni Vicent Nyerere

Kumbe alipopigwa BAN na uwaziri ukawa byebye.

Hawa mawaziri vivuli hatuwajui kwa sababu they are no where to be seen. Wako kwenye makaburasha tu!
 
Jana waziri mmoja analia anadai siku hizi wana ccm hawana hata ujasiri wa kuvaa sare za chama chao kwa kuwa wanaona aibu mitaani watu wanawazomea au kuwashangaa, ccm hawajahi kufikia wakati mgumu kama walivyo sasa katika historia yake, na mimi sio mtabiri ila najua, the old party is suffocating tujiandae tu kwa mazishi..
 
Huyu jamaa bunge linaendelea yeye anazurura tu!

Nayeye ikifika wakati wa kutoa hotuba yake ya mambo ya ndani asije kuleta vituko kama vya Msigwa!!!

Lema, kaa chini uandae hotuba inayoeleweka. Acha kuzurura...

acha pumba wewe nenda kapate posho ya usik lumumba, kwan hao wabunge wa magamb wanafanya nn zaidi ya kulala mjengoni, wambunge 2 wa chadema wanatosha kuwatoa povu wabunge wa mgamba!
 
Lema ni waziri kivuli wa wizara gani nasubiri kituko cha hotuba yake.
 
Kumbe alipopigwa BAN na uwaziri ukawa byebye.

Hawa mawaziri vivuli hatuwajui kwa sababu they are no where to be seen. Wako kwenye makaburasha tu!
Nenda kule kwenye thread ya Pasco kuhusu kuifuta Chadema unasubiriwa ukaichangie.
 
Mh,huku ndiko kuwajibika kwa mbunge,Lema kituko,CDM hawajui walifanyalo,kikao kinaendelea,yeye ahudhurii na mshahara wake anapata,cjui sheria za bunge zimekaaje kwenye mazingira kama haya mtu kutokuhudhuria na kujifanyia mambo yake na kwa faida zake,kweli wabunge tunao,wanakula hela za wananchi huku wakiwadanganya,shame on you Lema.
 
Back
Top Bottom