Feedback
JF-Expert Member
- Mar 14, 2011
- 7,988
- 4,514
MakeneTwo things wakuu. Walipanga kufanya hila na hujuma Arumeru Mashariki ili washinde huku pia wakituwinda Arusha Mjini ili wafanye kama walivyofanya. Thinking yao ikiwa ni kulenga total demoralization kwa chama mbadala CHADEMA na upinzani wenye nguvu kwa ujumla dhidi ya Watawala. Arumeru Mashariki ikashindikana.
Bahati mbaya risk calculation zao ni mbovu sana. Hazifanyia kazi sawasawa kwa sababu wamefika mwisho. Huwezi kutegemea mahakama kushinda ubunge Arusha Mjini dhidi ya CHADEMA. Watu wa Arusha wanaamini kwa dhati katika hii struggle. Wanakiamini na kukipenda chama chao. Wako pamoja na mbunge wao. Wasubiri waone.
Mimi nililiona hilo mapema kabisa walitaka wapige double blow, imeshindikana.Kitu wasichojua ni kwamba wanafanya publicity ya bure kwa CDM. CDM wasiwe wanyonge kwa hili kwa sababu siasa si kukaa ofisini siasa ni kuwa karibu na wananchi kuongea nao. Hasara za kuvuliwa Lema kichama ni CCM na serikali yake kwa sababu inazidi kudumaza maendeleo ya wana Arusha hivyo kuongeza hasira za wananchi dhidi ya serikali ya CCM.
Ushauri wangu kwa chama na Lema asikate rufaa kwani miezi mitatu si mingi, kwa sababu nina uhakika uchaguzi ukirudiwa atashinda vizuri ya alivyofanya last time. Hii itakuwa ni advantage kwa CDM, itavunja rekodi yake kwa kushinda chaguzi ndogo mfululizo, kwa hiyo watu watazidi kukiamini.
Ushauri mwingine ni kuwa, strategically kampeni za Arusha mjini zitajipiga zenyewe, nguvu kubwa (50-60%) kama ni kwenye budget au mali watu ipelekwe kwenye ulinzi wa kura, vituo vijulikane mapema na wapiga kura wajulikane mapema, nafikiri kama ni mtaji wa vijana basi Arusha mjini mnao mkubwa kuliko Arumeru Mashariki.