Mhe Lema amevuliwa Ubunge kwa sababu tu ya ujasiri wake kiasi cha kutanguliwa jela kabla ya kukamatwa.
Nawamba wapiganaji wote kambi iliyokuwa Arumeru kuhamia Arusha mjini kuhakikisha kwamba Lema anarejeshwa Bungeni kwa mara ya pili.Ikumbukwe kwamba Lema ndiye aliyejitoa kwa gharama ya kifo kulinda kura za Nassary zisiibiwe!!
Leo hii Serikali inayoshindwa kulipa mishahara ya vyombo vya dola na Madaktari wameamua kutapanya mali kwa kutengua ubunge ambao utagharimu zaidi ya 20billions mbali na rushwa ambazo watu binafsi kama Lowassa watatoa rushwa.
Mtakumbuka kuwa Yusufu makamba alisha toa order kuwa wabunge wake nchi nzima wawafungulie kesi wabunge wa upinzani ili waenguliwe na sasa zipo kesi zaidi ya 40 nchi nzima ambaozo gharama ya kuizindeshe ni kubwa na kutengua kutaleta hasara ya zaidi ya 500billis.
Wakati hayo yakiendelea kesi zote za EPA zinazowausu Makada wa CCM zimewekwa kando , sasa dawa ni Moja , arumeru wameonyesha Njia!!!