Jadda
JF-Expert Member
- May 20, 2019
- 31,541
- 88,493
Yaani wanapenda kuambiwa kile wanachotaka kusikia tu yaani kwao mtu yeyote anayetetea single mothers basi na yeye ni single mother mtu yeyote anayetetea unmarried women basi na yeye ni unmarried woman mtu yeyote anayewaambia ukweli anaonekana anataka usawa au ushindani nao na mtu yeyote anayewaponda anaonekana ameshawahi kutendwa kwenye uchumba au ndoaUsijichoshe kuanza kuelezea mtu asiekujua mama.
Yani wanaonaga mtu akiwa na vitu wanavyovitamani wao na hawana basi anabrag au hana anaandika kujifurahisha.
Eti JF wote. Kwahiyo kama mtu ana ndoa asiseme? Ni wivu tuu unawasumbua na wameshazoea kuwaweka kundi fulani wanawake wa JF ndio maana wakiona ambae hayupo huko wanapata hasira na kuanza kutoa comments za chuki
Mwanaume mwenzao akianzisha uzi wowote wa kuwaponda wanawake basi wanasema "ukisikia yalaa ujue limempata" yaani furaha yao ni kuona wanawake wote tunakubaliana na pumba na shudu wanazoongea kuhusu sisi halafu mbaya zaidi wanalazimisha ionekane kwamba wanawake tu tuna stress za mapenzi ila wanaume hawana na wala hawajawahi kuwa nazo kabisa ndiyo maana wote wanajitutumua humu
Kuna mmoja humu alinilazimisha nikubali eti kuwa mimi ni single mother nikamwambia oohh kumbe shida yako ni kusikia hivyo tu haya basi mimi ni single mother yaani nilivyomwambia hivyo alifurahi kweli akapata pa kutolea maneno yake nikaamua kujitolea tu kuwa trashcan ya stress zake ili afurahi na roho yake
Maana ndicho wanaume wengi humu wanachokitaka ukiponda tu hoja zao utaitwa majina yote mabaya sasa kwa vile mimi nimeshawajulia hata hawanisumbui nawapa makavu kama kawaida maana najua hata wakiniita hayo majina mabaya hayawezi kubadilisha ukweli wala uhalisia



