Gharama za michango ya harusi na sintofahamu ya chakula

Gharama za michango ya harusi na sintofahamu ya chakula

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
6,148
Reaction score
10,573
Hivi karibuni kwenye mijadala ya harusi, gumzo limekuwa kadi za mchango. Ukitazama kadi, single unachangia elfu 50, double elfu 90. Hapo mtu anajisikia kama amenunua Tiketi ya Mechi fulani, kumbe unakwenda kuwapiga tafu watu katika harusi yao. Lakini ukifika, unakutana na ujumbe kuwa: “Chakula hakipakuliwi kiholela, kuna catering service waliobobea katika kupakua chakula.”
images (66).jpeg

Sasa mtu anabaki kushangaa, hivi hela yangu niliyoitoa kwa moyo mmoja ni mchango au ni tiketi ya chakula cha kupimwa? Kwanini kwenye harusi watu wanajiona kama wameingia kwenye mgahawa wa five star hotel ya Dubai? Na mbaya zaidi, ukitamka kidogo tu, “mimi leo nataka nyama tu,” unachunguliwa kana kwamba umetukana bibi harusi mbele ya maharusi wote, na wakati mwingine kupewa mifupa.
kiporo-pic.jpg

Jamani, kama mtu hajui, nyama ndiyo kiburudisho kikuu wa sahani. Wali, ndizi na chapati ni wachezaji wa akiba tu. Mchango wangu ni kama mzazi wa mjukuu, siwezi kupewa kipimo cha kijiko kimoja cha nyama eti kwa sababu kuna “uwiano.”
images (65).jpeg

Lakini, tuseme ukweli, hizi harusi zetu zinatufundisha kitu: mchango si bei ya chakula, ni kuunga mkono. Ila basi, wenyeji wakumbuke, ukimpa mtu kadi ya mchango, usimfanye ajisikie kama ameingia kwenye jaribio la kidiplomasia la kula kwa mizani.
1700656734556.jpeg

Weka ucheshi, acha watu wale mchele, nyama ipate wadau, na watu wabaki na kumbukumbu tamu badala ya kumbukumbu za kuhesabiwa idadi ya nyama.
 
Kwenye miharusi huwa kuna vituko vingi wakati wa kula kutokana na hadhi ya harusi na bajeti ya misosi. Kuna harusi unakuta zina vyakula vya awali kabla ya muda wa kula msosi mkubwa. Msosi wa awali unaweza kushiba na kuishia kula nyama tu kwenye msosi wa bufee. Bufee zingine ni ndefu sahani hujaa pomoni mpaka aibu. Harusini tunakula kistaarabu si lazima ujaze sahani. Tunachagua vile ambavyo hatuli mara kwa mara nyumbani
 
Hivi karibuni kwenye mijadala ya harusi, gumzo limekuwa kadi za mchango. Ukitazama kadi, single unachangia elfu 50, double elfu 90. Hapo mtu anajisikia kama amenunua Tiketi ya Mechi fulani, kumbe unakwenda kuwapiga tafu watu katika harusi yao. Lakini ukifika, unakutana na ujumbe kuwa: “Chakula hakipakuliwi kiholela, kuna catering service waliobobea katika kupakua chakula.”
View attachment 3471398
Sasa mtu anabaki kushangaa, hivi hela yangu niliyoitoa kwa moyo mmoja ni mchango au ni tiketi ya chakula cha kupimwa? Kwanini kwenye harusi watu wanajiona kama wameingia kwenye mgahawa wa five star hotel ya Dubai? Na mbaya zaidi, ukitamka kidogo tu, “mimi leo nataka nyama tu,” unachunguliwa kana kwamba umetukana bibi harusi mbele ya maharusi wote, na wakati mwingine kupewa mifupa.
View attachment 3471397
Jamani, kama mtu hajui, nyama ndiyo kiburudisho kikuu wa sahani. Wali, ndizi na chapati ni wachezaji wa akiba tu. Mchango wangu ni kama mzazi wa mjukuu, siwezi kupewa kipimo cha kijiko kimoja cha nyama eti kwa sababu kuna “uwiano.”
View attachment 3471399
Lakini, tuseme ukweli, hizi harusi zetu zinatufundisha kitu: mchango si bei ya chakula, ni kuunga mkono. Ila basi, wenyeji wakumbuke, ukimpa mtu kadi ya mchango, usimfanye ajisikie kama ameingia kwenye jaribio la kidiplomasia la kula kwa mizani.
View attachment 3471400
Weka ucheshi, acha watu wale mchele, nyama ipate wadau, na watu wabaki na kumbukumbu tamu badala ya kumbukumbu za kuhesabiwa idadi ya nyama.
Roho yako haina hadhi ya kuchangia harusi kiuhalisia, una uroho. Unasaidia mtu ili ufaidike wewe.

Kuna harusi za jamaa na ndugu zetu wa mbali tunachangia na tunashindwa kwenda, je nazo tuombe delivery ya chakula. Harusi ya mwisho nilochangia last month hata sijui imefanyika mkoa gani.

Badala ya kuchanga hiyo 50k wewe nunua kuku ule maana inaonekana kuku ni vitu vya kukugombanisha na watu.

Watu wanajua umechanga kwa upendo kumbe unategeshea ubebe mfuko wa Rambo ukaponee kuku nyumbani.
 
Harusi za ukumbini unaweza ukakosa chakula kama kuna ongezeko la watu ambao hawakupigiwa mahesabu wameingia kinyemela kula. Ukichanga usitegemee kuwa utakula, hata kama ni harusi ya uswahilini huko mitaani wageni hutangulizwa kula na wenyeji huwa wa mwisho na hupelea vyakula, inaudhi sana ikiwa ulichanga na ukakosa chakula
 
Raha ya sherehe ya harusi, kuwepo na watu watakao kosa nyama/kuku na kachumbari!
Halafu yaani uchangie 50k uachiwe ujipakulie mwenyewe? Hapo ujue kuna gharama nyingine, kama ukumbi, mapambo, muziki, mc, picha, usafiri, vinywaji, n.k!
Kama hujafanya hii shughuli, subiri muda wako ukifika ukihitaji kufanya utaona kichwa kitakavyopata moto kama itakuwa unategemea michango ya watu, unless usichangishe kabisa!
 
Hivi karibuni kwenye mijadala ya harusi, gumzo limekuwa kadi za mchango. Ukitazama kadi, single unachangia elfu 50, double elfu 90. Hapo mtu anajisikia kama amenunua Tiketi ya Mechi fulani, kumbe unakwenda kuwapiga tafu watu katika harusi yao. Lakini ukifika, unakutana na ujumbe kuwa: “Chakula hakipakuliwi kiholela, kuna catering service waliobobea katika kupakua chakula.”
View attachment 3471398
Sasa mtu anabaki kushangaa, hivi hela yangu niliyoitoa kwa moyo mmoja ni mchango au ni tiketi ya chakula cha kupimwa? Kwanini kwenye harusi watu wanajiona kama wameingia kwenye mgahawa wa five star hotel ya Dubai? Na mbaya zaidi, ukitamka kidogo tu, “mimi leo nataka nyama tu,” unachunguliwa kana kwamba umetukana bibi harusi mbele ya maharusi wote, na wakati mwingine kupewa mifupa.
View attachment 3471397
Jamani, kama mtu hajui, nyama ndiyo kiburudisho kikuu wa sahani. Wali, ndizi na chapati ni wachezaji wa akiba tu. Mchango wangu ni kama mzazi wa mjukuu, siwezi kupewa kipimo cha kijiko kimoja cha nyama eti kwa sababu kuna “uwiano.”
View attachment 3471399
Lakini, tuseme ukweli, hizi harusi zetu zinatufundisha kitu: mchango si bei ya chakula, ni kuunga mkono. Ila basi, wenyeji wakumbuke, ukimpa mtu kadi ya mchango, usimfanye ajisikie kama ameingia kwenye jaribio la kidiplomasia la kula kwa mizani.
View attachment 3471400
Weka ucheshi, acha watu wale mchele, nyama ipate wadau, na watu wabaki na kumbukumbu tamu badala ya kumbukumbu za kuhesabiwa idadi ya nyama.
Roho yako haina hadhi ya kuchangia harusi kiuhalisia, una uroho. Unasaidia mtu ili ufaidike wewe.

Kuna harusi za jamaa na ndugu zetu wa mbali tunachangia na tunashindwa kwenda, je nazo tuombe delivery ya chakula. Harusi ya mwisho nilochangia last month hata sijui imefanyika mkoa gani.

Badala ya kuchanga hiyo 50k wewe nunua kuku ule maana inaonekana kuku ni vitu vya kukugombanisha na watu.

Watu wanajua umechanga kwa upendo kumbe unategeshea ubebe mfuko wa Rambo ukaponee kuku nyumbani.
 
Roho yako haina hadhi ya kuchangia harusi kiuhalisia, una uroho. Unasaidia mtu ili ufaidike wewe.

Kuna harusi za jamaa na ndugu zetu wa mbali tunachangia na tunashindwa kwenda, je nazo tuombe delivery ya chakula. Harusi ya mwisho nilochangia last month hata sijui imefanyika mkoa gani.

Badala ya kuchanga hiyo 50k wewe nunua kuku ule maana inaonekana kuku ni vitu vya kukugombanisha na watu.

Watu wanajua umechanga kwa upendo kumbe unategeshea ubebe mfuko wa Rambo ukaponee kuku nyumbani.
Acha fix zako nawee, uongo mtupuu. Lol
 
Mbinu za kutokukosa msosi harusini au kwenye semina ni kuwahi mbelembele, wa mbelembele hufaidi mapande makubwa ya nyama. Utasikia wagawaji chakula wakiambiana punguzeni migao watu bado wengi. Hawa wanaokuwa wa mwishomwisho hupata kidogo kwa kuwa mgao umepunguzwa. Mi huwa nawafuata wazazi wa maharusi nyuma yao, kuwa wa mwisho ni kujitakia kukosa chakula
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom