Harusi ni mwanzoni wa Septemba, wageni ni 250, lakini 80% bado hawajachanga. Hao 20% waliomaliza wachache ila wengi wamepunguza michango.
Nataka kufanya sherehe ndogo nzuri bila presha kwa bajeti isiyozidi tsh milioni 5-6.
Naomba ushauri wenu wakuu.
Hivi inakuwaje mwanaume mzima unafikia hatua ya kupiga simu na kutuma meseji za kuombaomba michango ya sherehe ya harusi yako?
Unajikuta ghafula umeungwa kwenye group la harusi, humo bwana harusi mtarajiwa anajidhalilisha kwa kuombaomba michango mpaka unaona aibu wewe.
Hivi ni lazima...
Hivi karibuni kwenye mijadala ya harusi, gumzo limekuwa kadi za mchango. Ukitazama kadi, single unachangia elfu 50, double elfu 90. Hapo mtu anajisikia kama amenunua Tiketi ya Mechi fulani, kumbe unakwenda kuwapiga tafu watu katika harusi yao. Lakini ukifika, unakutana na ujumbe kuwa: “Chakula...
Michango ya harusi imekuwa mzigo kwa familia na wachangiaji. Ingawa ni desturi ya kijamii kutoa michango katika matukio haya, ni naona lazima kutafakari kama michango hii inasaidia kweli familia au inawaongezea mzigo wa kifedha.
Badala ya kuendelea na utaratibu wa kuchangia harusi na misiba, ni...
Wakuu hivi ni namna gani unaweza kuepuka kuchangia harusi hasa hawa wanoomba michango randomly kisa tu ulisoma naye unaamka unajikuta kwenye group na wengine wako na audacity unakuta hadi amount ya mchango ameshakujazia.
Imenilazima kuweka private setting za WhatsApp nisiaddiwe kwenye magroup...
Dar bwana unashangaa mwanaume amekuzoea ghafla.anajileta bana anajileta tena hakujui humjui unasema mtu kanielewa nini? unamshukuru Mungu mkeka wa wa maombi kumi na mbili kwa mwamposa umetick mapema kabla ya juni maana kwenye mkeka tatu bora pale umeandika future husband awe hata anapumua tu...
Africans, we are poor, lakini we are acting rich.
Kwamba unaogopa kusemwa?
Unaogopa kuitwa masikini?
Unaogopa lawama za kutoarika watu?
Unaogopa kutoendana na mila tulizozizoea?
Au ndio njia mbadala ya kupatia pesa za michango kujiboost maisha kidogo?
Muda mwingine hadi tunageuka kero pale...
Habari za kuchakarika wakuu,
Aisee hapa navyoandika nimeungwa kwenye magroup matatu ya harusi zinazokuja mwisho wa mwaka huu, 1 ni binti ndugu wa ukoo sio immediate family link kwa mababu huko, mmoja ni jamaa nilitinga nae job kabla sijahamia nilipo, mwingine jamaa tumesoma wote high school...
Siku hizi ukikutana na mtu ambae hukumchangia harusi yake basi utakuta hakuchangamkii kama zamani.
Jamani sisi sio fake friends ni hali ngumu jamani mtusamehe bure
Embu tujadili na kuangalia umuhimu/ulazima wa hii michango ya harusi .Tunaishi kijamaa ndani ya mifumo ya kipepari,tuna vipato vya kawaida sana hasa kwa ndugu zangu wafanyakazi.
Wafanyakazi wanakipato kidogo mno hakiendani na uhalisia wa maisha,na pale anapoishi kijamaa kwa kushiriki hizi...
Hii app ya Whatsapp sioni faida yake kabisaaa imegeuka kausha damu kwangu, imagine nina group tano za michango ya harusi na zote zinadai 50K kwenda juu. Na bado sijui kama kutakucha bila kuongezwa kwenye group jingine.
Yaani kila siku unaungwa kwenye magroup mpya za harusi, watu hata huwajui...
Kwanza vitu vingine kwenye maisha sio lazima ni sifa tu, hakuna utofauti wowote kwenye ndoa either ufanye sherehe au usifanye, lakini kumekua na kero kubwa sana juu ya hii Michango ya harusi, ndoa sio bahati mbaya ni maandalizi ya muda mrefu, unakuta mtu huna mazoea naye ya karibu sana kwa...
Salaam,Shalom!!
Ndugu mmoja akapita Kwa jamaa zake katika eneo alilokuwa akifanyia biashara, akawashirikisha kuwa amepata mchumba na ataoa hivi karibuni, hivyo anaomba michango Kutoka Kwa wadau.
Jambo Hilo likawa kheri masikioni mwa Rafiki zake. Ndugu huyo, akachangisha michango pesa nyingi...
Habari wanajamii,
Mimi ni software developer, nilikuwa nina idea ya kutengeneza app/tool ya kusaidia kufuatilia na kukumbusha watu ahadi za michango kwa ajili ya harusi na sendoff.
App ina lengo la kutatua kero zifuatazo kwa mtu anayefuatilia, kukusanya na kutoa taarifa za makusanyo ya...
Katika maeneo ambayo Watanzania wameonesha ushirikiano wa hali ya juu mno, ni kwenye masuala ya sherehe. Wengi wanaoshirikishwa wamekuwa wakitoa ushirikiano murua kuanzia kwenye uuandaji kamati, kuchangisha michango na hata kula na kunywa.
Miongoni mwa shughuli za sherehe ambazo zimekuwa...
Tabia ya kutuchangisha michango ya harusi halafu mnakaa mwezi mnaachana sio nzuri.
Acheni kuchezea hela zetu wakuu.
Kabla hamjaachana, fikirieni hela zetu na usumbufu mliotupa wakati wa ndoa yenu.
Mfanyabiashara maarufu wilaya ya Hai, Mkoa wa Kilimanjaro, James Mushi amefungua maombi madogo akiiomba Mahakama ya Wilaya hiyo itoe zuio la kusitisha usambazaji wa kadi na michango ya harusi ya mtu anayedaiwa kutumia jila lake na familia yake kuchangisha michango hiyo.
Akiwasilisha maombi...
Kwakuwa shauri lipo mahakamani ni vizuri tusubiri maamuzi ya mahakama.
Lakini michango ya Harusi ni mingi kuliko hata Tozo tunazozipigia kelele kila uchao. Na hili nalo mkaliangalie.
Na kesi ya msingi wakati inasikilizwa ni vizuri kusitisha michango ya harusi kwanza tupate muongozo wa...
Hali ya maisha haifai, kila kitu juu huku mishahara ikiwa chini na biashara kuwa ngumu sana.
Tozo kila mahali, mafuta ya nishati juu, yakupikia juu, pesa haionekani , athari ni kuzidi kuongeza gepu la matajiri na masikini, Hali hii inadidimiza zaidi masikini huku matajiri wakineemeka na kipanda...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.