Gesi imepanda bei kuanzia leo tar 9/2/2017

Nasoma msg imetumwa muda huu.. KUANZIA LEO TAR 11/2/17
Kg 15 wakala watanunua kwa sh 45"000 badala ya 46"000 na mdogo 18"000 badala ya 18"500

Watauza kg 15 kwa sh 51"000 badala ya 52"000 ya awali na ndogo 21"000 badala ya 21"500 ya awali

Tuendelee kupiga kelelee waziri husikaa hii ni dhahama kwa taifa masikini kama hili. Nina imani hamjawapindishia kodi ya kufikia kuongeza elfu tisa kwa mtungi wa 15kg. tunaomba sauti zenu zitumike kusaidia wananchi na sio kwenye umeme tu

Wenu
Nchi ya viwanda
 
Hakika kuzaliwa Tanzania ni Tunu ninayojivunia hakuna anae jali.
Gesi imepanda kwa Asilimia Ishirini (20%) hakuna anaejali Business as usual!
Hata Hili litapita Na Tutasahau ni suala la Mda..
Mda ni msemakweli
 
Hakika kuzaliwa Tanzania ni Tunu ninayojivunia hakuna anae jali.
Gesi imepanda kwa Asilimia Ishirini (20%) hakuna anaejali Business as usual!
Hata Hili litapita Na Tutasahau ni suala la Mda..
Mda ni msemakweli
Wengi wakipato chakawaida ni kuni na mkaaa, bado nchi hii nimaskin sana so wengi hawajaguswa, tumuombe mungu tu!!! Nchi ishakata kona hii
 
Tangu nianze kusikia habari za gesi ya songo songo nadhani nilikuwa shule ya msingi. Ni takribani miaka 20 na zaidi sasa imepita majuzi juzi ndiyo nikaona mitambo ya kufua umeme inayotumia gesi ikizinduliwa kwa sherehe na nderemo pale Kinyerezi.

Lakini swali langu ambalo limekuwa likinisumbua daima ni kwamba hivi hii gesi sisi wananchi wa kawaida tutanufaika nayo vipi?

Leo sasa nimegundua kuwa kumbe tunadanganywa kama watoto wa kuku. Wiki tatu zilizopita gesi ya kupikia LPG ilikuwa inauzwa shilingi 43,000 kwa mtungi wa kilo 15.

Leo nimeenda kununua nimekuta imepanda na kuwa shilingi 52,000 yaani bei imeongezeka kwa shilingi 9,000 ambayo ni sawa na asilimia 21%.

Mpaka sasa sijaelewa kwanini watanzania tunahangaishwa na makumpuni ya kibepari yaliyokuja kuvuna pesa kwa maskini sie wakati tuna gesi yetu ambayo kama tungekuwa na dhamira ya dhati ya kuwasaidia watanzania na kunusuru miti na mazingira yetu basi mtungi wa gesi wa kilo 15 usingezidi shilingi elfu 15,000.

Nimeahirisha kununua gesi naenda kununua gunia la mkaa ambalo kwa mazingira ninayoishi mimi nitalinunua kwa shilingi 45,000 na litatumika kwa mwezi na siku kadhaa wakati kwa gesi huwa natumia mitungi miwili ya kilo 15 kwa mwezi.

Wenye mamlaka angalieni hili suala kwa jicho la tatu. Sina ugomvi na wafanyabiashara wa gesi maana wao wanatafuta faida na siku zote faida hutengenezwa panapofursa.

Masikitiko yangu ni kwa miti maelfu kwa maelfu inayooendelea kukatwa kwa kuwa bado kuna demand kubwa ya mkaa kwa watanzania kuliko gesi. Gesi imeendelea kuwa nishati ya anasa kuipikia kama ilivyo kwa umeme nchi hii.

Ni aibu kwa gesi kuendele kuwa bei juu huku tukijinasibu tuna metric feet trilioni sijui ngapi wakati watanzania tunaumia kwa kununu gesi kwa bei ya ajabu. Siku ikishuka bei mnijuze nitaaanza kunua tena gesi ila kwasasa miti na inivumilie.

Asanteni na siku njema
 
  • Thanks
Reactions: bne
pole sana ndugu yangu kwa kujiuliza swali hilo kila mara .
mi naona uache tu maana utakonda bure fanya mambo mengine.
unajua kwenye siasa hakuna swali lisilokuwa na majibu, kwaiyo watakuja watu kukujibu.
kumbuka miongoni mwafasiri za siasa nikua na uwezo wa kuzungumza jambo au kuahidi jambo kuwa utafanya au uta wezesha kufanyika halafu kuwa na uwezo wa kurudi kusema kwanin hujafanya
kwa maana hiyo hakuna hata skumoja mahali mwanasiasa anasema samahani niliahid hiki na kile sikufanya
kuna wakati huwa naona kuwa uongo nimiongoni mwa vitendea kazi vya mwanasia
 
Kabla ya kupost ungejiuliza pia kuwa, Almasi iliyopo mwadui, Tanzanite, my. Kilimanjaro ,dhahabu, mbuga za wanyama, nikwafaida ya nani? nadhani usingepoteza na kumaliza chaji kwenye simu yako.
 
Yawezekana gesi tunayotumia haitoki Tz.

Lakini kama kunauwezekano ni vizuri waziri wa nishati afanye utaratibu tutumie ges yetu.

Na serikali ijitahidi ges hiyo ipatikane kila kona ya nchi yetu kwa bei walau ya mwananchi wa chini kabisa kuimudu.

Kwa hali hiyo tutatunza vizuri mazingira .

Waziri wa nishati na madini wakishirikiana na waziri wa maliasili chini ya Raisi wetu nadhani tutaweza.
 
Tumulize lizaboni&co naona gesi imewasaidia sana

Ova
Kumuliza Lizaboni ni kumuonea tu wakati wahusika wakuu unao huko huko ,tusisahau tulitakiwa pia kuwa tuwe tunatumia hata umeme kwa kupikia lakini Mzee Richmond kaufanya umeme anasa na yeye ndie ananufaika,Mzee wa dili mnaye huko huko na hata haya mambo ya gesi yumo,yeye kila sehemu ya ulaji yupo ndio maana mtoto wa mjini akamchinjia mbali.
 
Tangu nianze kusikia habari za gesi ya songo songo nadhani nilikuwa shule ya msingi. Ni takribani miaka 20 na zaidi sasa imepita majuzi juzi ndiyo nikaona mitambo ya kufua umeme inayotumia gesi ikizinduliwa kwa sherehe na nderemo pale Kinyerezi.

Lakini swali langu ambalo limekuwa likinisumbua daima ni kwamba hivi hii gesi sisi wananchi wa kawaida tutanufaika nayo vipi?
LPG bado haijaanza kutengenezwa Tanzania , ndio bado wapo kwenye mpango. Hii gesi tunayoitumia inatoka nje ya nchi.
Leo sasa nimegundua kuwa kumbe tunadanganywa kama watoto wa kuku. Wiki tatu zilizopita gesi ya kupikia LPG ilikuwa inauzwa shilingi 43,000 kwa mtungi wa kilo 15.

Leo nimeenda kununua nimekuta imepanda na kuwa shilingi 52,000 yaani bei imeongezeka kwa shilingi 9,000 ambayo ni sawa na asilimia 21%.

Mpaka sasa sijaelewa kwanini watanzania tunahangaishwa na makumpuni ya kibepari yaliyokuja kuvuna pesa kwa maskini sie wakati tuna gesi yetu ambayo kama tungekuwa na dhamira ya dhati ya kuwasaidia watanzania na kunusuru miti na mazingira yetu basi mtungi wa gesi wa kilo 15 usingezidi shilingi elfu 15,000.

Nimeahirisha kununua gesi naenda kununua gunia la mkaa ambalo kwa mazingira ninayoishi mimi nitalinunua kwa shilingi 45,000 na litatumika kwa mwezi na siku kadhaa wakati kwa gesi huwa natumia mitungi miwili ya kilo 15 kwa mwezi.

Wenye mamlaka angalieni hili suala kwa jicho la tatu. Sina ugomvi na wafanyabiashara wa gesi maana wao wanatafuta faida na siku zote faida hutengenezwa panapofursa.

Masikitiko yangu ni kwa miti maelfu kwa maelfu inayooendelea kukatwa kwa kuwa bado kuna demand kubwa ya mkaa kwa watanzania kuliko gesi. Gesi imeendelea kuwa nishati ya anasa kuipikia kama ilivyo kwa umeme nchi hii.

Ni aibu kwa gesi kuendele kuwa bei juu huku tukijinasibu tuna metric feet trilioni sijui ngapi wakati watanzania tunaumia kwa kununu gesi kwa bei ya ajabu. Siku ikishuka bei mnijuze nitaaanza kunua tena gesi ila kwasasa miti na inivumilie.

Asanteni na siku njema
 
Faida ya walioaini mikataba, na waliopitisha sheria ya kuratibu kwa hati ya dharula bungeni.
 
Niliwahi kuambiwa kuwa zile 97% za madini zinazoenda nje, kuna watz wenzetu huenda nje ya kujichukulia mpaka 17% kutoka kwenye hiyo 97%.
 
kwa sasa matumizi ya gesi ni kuzalishia umeme.. Zaidi ya asilimia sitini ya umeme ubaopatikana leo ni wa gesi.. Bila gesi na ukame huu, mgao wa umeme ungekuwa umefikia pabsya zaidi ya ule wa mwaka 2006/2007!
 
Tangu nianze kusikia habari za gesi ya songo songo nadhani nilikuwa shule ya msingi. Ni takribani miaka 20 na zaidi sasa imepita majuzi juzi ndiyo nikaona mitambo ya kufua umeme inayotumia gesi ikizinduliwa kwa sherehe na nderemo pale Kinyerezi.

Lakini swali langu ambalo limekuwa likinisumbua daima ni kwamba hivi hii gesi sisi wananchi wa kawaida tutanufaika nayo vipi?

Leo sasa nimegundua kuwa kumbe tunadanganywa kama watoto wa kuku. Wiki tatu zilizopita gesi ya kupikia LPG ilikuwa inauzwa shilingi 43,000 kwa mtungi wa kilo 15.

Leo nimeenda kununua nimekuta imepanda na kuwa shilingi 52,000 yaani bei imeongezeka kwa shilingi 9,000 ambayo ni sawa na asilimia 21%.

Mpaka sasa sijaelewa kwanini watanzania tunahangaishwa na makumpuni ya kibepari yaliyokuja kuvuna pesa kwa maskini sie wakati tuna gesi yetu ambayo kama tungekuwa na dhamira ya dhati ya kuwasaidia watanzania na kunusuru miti na mazingira yetu basi mtungi wa gesi wa kilo 15 usingezidi shilingi elfu 15,000.

Nimeahirisha kununua gesi naenda kununua gunia la mkaa ambalo kwa mazingira ninayoishi mimi nitalinunua kwa shilingi 45,000 na litatumika kwa mwezi na siku kadhaa wakati kwa gesi huwa natumia mitungi miwili ya kilo 15 kwa mwezi.

Wenye mamlaka angalieni hili suala kwa jicho la tatu. Sina ugomvi na wafanyabiashara wa gesi maana wao wanatafuta faida na siku zote faida hutengenezwa panapofursa.

Masikitiko yangu ni kwa miti maelfu kwa maelfu inayooendelea kukatwa kwa kuwa bado kuna demand kubwa ya mkaa kwa watanzania kuliko gesi. Gesi imeendelea kuwa nishati ya anasa kuipikia kama ilivyo kwa umeme nchi hii.

Ni aibu kwa gesi kuendele kuwa bei juu huku tukijinasibu tuna metric feet trilioni sijui ngapi wakati watanzania tunaumia kwa kununu gesi kwa bei ya ajabu. Siku ikishuka bei mnijuze nitaaanza kunua tena gesi ila kwasasa miti na inivumilie.

Asanteni na siku njema
Subiri, habari za gesi utazisikia tena 2020...utamwona Magu anavotokwa povu kwamba gesi isambazwe bure kwa wananchi wote...mkishampa tena kura na akaapishwa sikilizia tena matusi yake baada ya hapo!
 
Back
Top Bottom