Thamani ya TZS katika mizani ya nguvu ununuzi sokoni imeshuka (purchasing power) hivi karibuni ingawa hatuwezi pata takwimu kutoka benki kuu..hii inachochea vitu kupanda bei, hapo awali ilikua upande wa vyakula hivi sasa tumeenda katika nishati ya gesi. Hatuwezi kupambanunua kesho itahamia sekta ipi.
Majibu hayapatikani kanisani katika maombi ya mfungo na kulia, wala viongozi waliopo bungeni maana wengi ni viziwi huku wale wanzao ni mabubu. Hata wakiongea hawajui kutengeza hoja, watajikita upande wa maslai ya chama na yao binafsi.
Usiniulize utatuzi ni upi na utatoka wapi, wahusika wanajijua ila hawajitambui.