Gazeti la Rai limekusanywa leo na halipatikani kabisa. Taarifa tulizonazo zinaeleza kuwa lilikuwa na habari inayoonyesha kuwa Beno Malissa na Ridhwan Kikwete wanaandaa mapinduzi ya kumng'oa Katibu wa UVCCM Martine Shigella. Taarifa za ndani kutoka Habari Cooperation zinaeleza kuwa habari hiyo iliwanukuu wenyeviti 17 wa UVCCM mikoa ambao walikuwa wakipingana na harakati hizo. Tena inaelezwa kuwa Usalama wa Taifa wamepewa jukumu la kuhakikisha gazeti hilo haliingii mtaani. Wenye taarifa zaidi mnaweza kuendelea ikiwemo kutupa habari iliyosababisha gazeti kukusanywa.