Ninajua wasifu wa Prof. Joseph Mbwiliza kwa kina. Ni Muha wa Kasulu huko Kigoma na ni mmoja wa maprofesa wa mwanzo kabisa wa kutoka maeneo ya ziwa Tanganyika.
Mtoto wa mkulima aliyepata elimu yake huko Marekani. Alishika madaraka makubwa serikalini na kwenye siasa. Amewahi kuwa Mkuu wa Chuo cha CCM Kivukoni.
Cha ajabu ameshidwa kupaza sauti kutetea siasa safi Tanzania ameishia kulilia Rawlings bila hata kujadili na kutoa mtazamo wake kuhusu kubakwà kwa demokrasia Tanzania.
Hana masilahi kwenye serikali ya Magufuli kama akina Prof. Kabudi. Uoga wa kupaza sauti kwa wasomi hawa ni wa nini sasa?
Mtoto wa mkulima aliyepata elimu yake huko Marekani. Alishika madaraka makubwa serikalini na kwenye siasa. Amewahi kuwa Mkuu wa Chuo cha CCM Kivukoni.
Cha ajabu ameshidwa kupaza sauti kutetea siasa safi Tanzania ameishia kulilia Rawlings bila hata kujadili na kutoa mtazamo wake kuhusu kubakwà kwa demokrasia Tanzania.
Hana masilahi kwenye serikali ya Magufuli kama akina Prof. Kabudi. Uoga wa kupaza sauti kwa wasomi hawa ni wa nini sasa?