Gavana Prof. Ndulu: Benki wapo sahihi

Gavana Prof. Ndulu: Benki wapo sahihi

Mwananchi alishaumizwa muda mrefu na mabank ...sasa ni vyema aumie lakini katika kile alichoumizwa nacho kiasi kidogo kirudi serikalini...Nia ya serikali ni njema mno lakini kuna wahuni wanachezea koki na lazima walowane!

Unajua kwamba mabenki yanalipa income tax? Kwanini hautaki kuelewa kwamba kosa lipo kwenye kuita hilo tozo VAT? Badili jina mkuu!
 
Huko TRA ndio unategemea tuwe tumejaza wataalamu wa haya mambo ya kodi na management accounting kuweza kudadavua vizuri kushinda BoT; Kaazi kweli kweli
 
Mwananchi alishaumizwa muda mrefu na mabank ...sasa ni vyema aumie lakini katika kile alichoumizwa nacho kiasi kidogo kirudi serikalini...Nia ya serikali ni njema mno lakini kuna wahuni wanachezea koki na lazima walowane!
haah haah mkuu wewe baki kuwa msomaji tu,waache kina Tyta mbeziboy wakueleweshe
 
Hahahahaha jana nilijua tunaingizwa chaka na T. R. A

Tangu lini V. A. T akalipa mfanya biashara. V. A. T ni consumption tax.

Nchi ya miujiza hiii. Tangu lini kuwe na double standards kwamba bank ndo zilipe VAT ila biashara zingine mteja ndo alipishwe.

Yani tumefikia pabaya sana kama taasisi kubwa hivi za kuaminika zinapishana kauli hadharani.

The Commissioner should simply resign for not being clear on the issue kwa hofu za siasa.

Any investor ataogopa akijua kuna hatari ya kubambikiziwa mikodi na huyu Commissioner kwa sababu za siasa.
 
Huyo prof naye hajui. TRA wamesema mabenki yalikuwa yakusanya bila kulipa. Sio new makato. Mwee
Amesema vat onalipwa na mteja siyo mwuza duka. Mwuza duka anakodi yake tayari anayolipa siyo vat. Vat is value added tax. Inalipwa na mteja
 
Huyo ni profesa, hana hofu, wala hafanyi kazi kwa mihemko. Hebu kubalini kwamba tumeliwa! Huu ni mfumo wa soko huria, mabenki hayataendesha benki kwa hasara. Tuko katika ubepari (capitalism) na ujamaa (socialism) serikali ku-control masoko! Usidanganyike! Alichokwambia Prof. ndio sahihi zaidi, mengine ni siasa tu!
 
The Commissioner should simply resign for not being clear on the issue kwa hofu za siasa.

Any investor ataogopa akijua kuna hatari ya kubambikiziwa mikodi na huyu Commissioner kwa sababu za siasa.
Kamishna ametoa ufafanuzi jana na instructions anayebisha ajitokeze.
 
Tra watanyamaza na mchezo umeishia hapo...mzigo kwa mlaji
 
Unategemea nini kwa Wabunge wa CCM? Labda kuwatusi Wapinzani na kumsifia mtawala. Ni aibu kubwa kuwa Mbunge kwa ticket ya CCM

Wanashupalia wengine kulipa kodi wakati wenyewe kukatwa kodi kwenye kiinua mgongo imekua nongwa. Nafikiri watolewe misamaha yote ya kodi wakatwe na kwenye mshahara huenda wakaanza kuchangia na kujadili mambo kwa kina, sarakasi za kuzima mambo ya Escrow, Lugumi zitaisha.
 
Huyo prof naye hajui. TRA wamesema mabenki yalikuwa yakusanya bila kulipa. Sio new makato. Mwee


Gazeti la Mwananchi: Wakati TRA ikiitaka BOT izichukulie hatua bank zilizotangaza kuongeza gharama za huduma za kibenk, BOT imesema mabenki yapo sawa!

Prof.Ndulu anasema mabenk watakuwa mawakala wa TRA tu katika kukusanya VAT lakini si walipaji,kwa hiyo hawezi kuwachukulia hatua.
c.KUMEKUCHA

Gavana wa BoT yupo sawa. Ukiangalia maelezo ya VAT kwenye website ya TRA ( chini sub-heading ya How VAT works utaona maelezo haya"The broad effect of the scheme is that businesses are not affected by VAT except in so far as they are required to administer it, and the burden of the tax falls to the final consumer."

Kama TRA wangetaka mzigo usiende kwa wananchi wangetumia kodi nyingine na sio VAT. Mara baada ya bajeti ya serikali 2016/2017 kusomwa, wataalam wa masuala ya kodi walionya kuwa jambo hili lataleta mkanganyiko lakini hawakusikilizwa.
 
Huko TRA ndio unategemea tuwe tumejaza wataalamu wa haya mambo ya kodi na management accounting kuweza kudadavua vizuri kushinda BoT; Kaazi kweli kweli
sasa inategemeana mkuu na utii bila shurti
 
Gavana wa BoT yupo sawa. Ukiangalia maelezo ya VAT kwenye website ya TRA ( chini sub-heading ya How VAT works utaona maelezo haya"The broad effect of the scheme is that businesses are not affected by VAT except in so far as they are required to administer it, and the burden of the tax falls to the final consumer."

Kama TRA wangetaka mzigo usiende kwa wananchi wangetumia kodi nyingine na sio VAT. Mara baada ya bajeti ya serikali 2016/2017 kusomwa, wataalam wa masuala ya kodi walionya kuwa jambo hili lataleta mkanganyiko lakini hawakusikilizwa.
wabunge wa CCM hawakuona hili?
 
Kamishna ametoa ufafanuzi jana na instructions anayebisha ajitokeze.

Kamishna kaaibisha profession.

Kasema kwenye bank charges ya Shs. 1000 wao wanachukua Shs. 153 na Bank Shs. 847.

Swali, tarehe 30 June bank charge ilikua Shs. 1000 au Shs. 847?

Kamishna anaogopa kusema wazi gharama zimeongezeka kwa mtumiaji.
 
Prof. Ndulu yupo sahihi, maadam hii kodi imekwishapitishwa na Bunge, hakuna namna wananchi mtailipa tu. Ni "value added tax" (kwa lugha rahisi=kiwango cha ziada kwa gharama halisi inayotozwa katika bidhaa au huduma kulingana na kiwango cha asilimia kilichowekwa na sheria/
mtoza kodi).

TRA wanawachezea akili tu au mnachanganywa akili zenu tu kama itasaidia kupunguza maumivu, lakini mwisho wa siku mtailipa.
 
Back
Top Bottom