Gavana Prof. Ndulu: Benki wapo sahihi

Gavana Prof. Ndulu: Benki wapo sahihi

Mambo NDINDINDI hapo ndo tutajua Tundu ni mwanasheria au mhalifu. Nilimsikiliza sana Bwana TRA nikajiuliza hii ni nini? Sijapata jibu
 
Huyu gavana hana msaada wowote nchini.ydio maana BOT ina mauzauza kibao..atoke tu hizi nyakati zimemzidi uwezo.
Nakubaliana na wewe mkuu, TRA hoja yao ni kwamba benki zinatakiwa kulipa serikali 18 % ya charges wanazotukata, yeye anakuja na habari tofauti kwamba benki ni wakusanyaji tuu wa hiyo 18 %.
 
Ni watu wachache sana wanaoweza kujua prof kazungumzia nini huwezi kumuelewa kama ulienda shule kwa ushabiki
 
Nasikia hata bodaboda nao wanakamatwa kwa kosa la kuendesha bodaboda. Tunakoelekea sasa ni wapi?
 
Mlizoea kona kona sasa zimebanwa ...mlikuwa mnawakamua wananchi tu halafu mrejesho kwa serikali hakuna...

mlikuwa mnakopesha serikali fedha yake sasa hakuna...

ni vyema penye ukweli kila mmoja wetu auseme huo ukweli,kuupindisha huo ukweli sio jambo sahihi ata kidogo.
 
Naungana na Tyta kosa la kwanza ni kuita hilo tozo VAT, hapo ndio mzizi wa fitna unapoanzia. TRA nao wanasemaje mabenki hayalipi kodi wakati wakiweka taarifa zao za kifedha kuna kua na before tax au after tax? Sasa kama hizo charges ni sehem ya hiyo faida, si ndio unakua imejumuishwa kwenye income tax zinazolipwa na mabenki? Any way, vyovyote itakavyokua, mwananchi ndio akataeumia.
kibaya zaidi wanajichanganya changanya,Mpango anaiita excise duty,TRA wanaiita VAT lakini mzigo mnamdondokea Taasisi ya Fedha(Kituko hiki) na BOT nao wanasema hii mzigo unaenda kwa mlaji(final consumer)..Yaan ''vurugu mechi''...
 
Huyo prof naye hajui. TRA wamesema mabenki yalikuwa yakusanya bila kulipa. Sio new makato. Mwee
Mkuu usiseme siyo makato mapya,ni makato mapya kwa sababu awali yalikuwa hayakatwi. Benki zinafanya biashara ni lazima ziongeze tozo kufidia hiyo kodi itakayotozwa na serikali. Vat inalipwa na mteja,benki zinakusanya kwa niaba ya tra. Prof.ndullu yupo sahihi sana!!
 
Gazeti la Mwananchi: Wakati TRA ikiitaka BOT izichukulie hatua bank zilizotangaza kuongeza gharama za huduma za kibenk, BOT imesema mabenki yapo sawa!

Prof.Ndulu anasema mabenk watakuwa mawakala wa TRA tu katika kukusanya VAT lakini si walipaji,kwa hiyo hawezi kuwachukulia hatua.

Beno Ndulu ametolea mfano unapokua unauza duka unakuwa wakala tu wa TRA na sio mlipaji.....KUMEKUCHA

View attachment 362128
Gazeti la Mwananchi: Wakati TRA ikiitaka BOT izichukulie hatua bank zilizotangaza kuongeza gharama za huduma za kibenk, BOT imesema mabenki yapo sawa!

Prof.Ndulu anasema mabenk watakuwa mawakala wa TRA tu katika kukusanya VAT lakini si walipaji,kwa hiyo hawezi kuwachukulia hatua.

Beno Ndulu ametolea mfano unapokua unauza duka unakuwa wakala tu wa TRA na sio mlipaji.....KUMEKUCHA

View attachment 362128
Hii vita tamu kwel, mwanasiasa tra vs Msomi Bot tamu kwel.... acha wararuane tuone huu uchumi
 
Ukweli unabaki palepale.always mzigo wa kodi ni wa mlaji!!!nakukubali prof.that is a simple and clear principle!!!
 
Hahahaa...mkuu hii mada imewachanganya watu mpaka inakua ngumu kutambua ambae haelewi ni yupi na ambaye anaongea sarcastically ni yupi

Kama kamishna ameshindwa kuelezea VAT pamoja na waziri wake wa fedha, kweli wataweza complex terms za uchumi wa viwanda?

Nchi nyingine kwa sasa kamishna angekua amefukuzwa kazi.

Kamishna anaposhindwa kuelezea VAT kwa sababu za kisiasa, anatoa picha gani kwa muekezaji, kwamba TRA will interpret the tax law however it wants -- in a populist manner -- and you shall pay.

Body language yake inaonyesha haamini anachokiongea.
 
Ni watu wachache sana wanaoweza kujua prof kazungumzia nini huwezi kumuelewa kama ulienda shule kwa ushabiki
Mkuu me mwenyewe sijawai hata kusoma hayo masomo siju accounts..sijui bookkeeping...sijui commerce ila nimemuelewa vzuri Kabisa....Na nilishabishana sana Na watu kuhusu hii kitu kuwa mzigo utakuwa kwa mlaji wa Mwisho ila baadhi ya watu hawaelewi Kabisa mkuu...ni ishu ndogo sana ila kama ulivosema kama mtu alienda shule kimkumbo hawezi kuelewa Kabisa alichosema Gavana..
 
Kama kamishna ameshindwa kuelezea VAT pamoja na waziri wake wa fedha, kweli wataweza complex terms za uchumi wa viwanda?

Nchi nyingine kwa sasa kamishna angekua amefukuzwa kazi.

Kamishna anaposhindwa kuelezea VAT kwa sababu za kisiasa, anatoa picha gani kwa muekezaji, kwamba TRA will interpret the tax law however it wants -- in a populist manner -- and you shall pay.

Body language yake inaonyesha haamini anachokiongea.

Halafu cha kushangaza zaidi...waziri wa fedha safari hajateuliwa tu mwanasiasa..ameopolewa mtu ambaye tulitegemea ni mbobezi kutoka TRA..akapewa ubunge na uwaziri. Sasa kama ubobezi wenyewe ndio huu...kwakweli nchi hii hatuna msalia mtume.
 
Huyo prof naye hajui. TRA wamesema mabenki yalikuwa yakusanya bila kulipa. Sio new makato. Mwee
Wewe ndo hujui,walikuwa wanakusanya wapi wakati hii kodi kwenye miamala ya fedha na imeanza Jana,ccm imekuharibu ubongo mpaka hujielewi,usikute mtu mwenye unae tusumbua umeishia darasa la pili
 
Halafu cha kushangaza zaidi...waziri wa fedha safari hajateuliwa tu mwanasiasa..ameopolewa mtu ambaye tulitegemea ni mbobezi kutoka TRA..akapewa ubunge na uwaziri. Sasa kama ubobezi wenyewe ndio huu...kwakweli nchi hii hatuna msalia mtume.

Nchii hii kuna utamaduni wa kushindwa kumkosoa bosi.

Si ajabu kwenye cabinet meetings kila kitu ni ndio mzee. Ukishakua mtu wa "ndio mzee" inamaanisha elimu umefungia kabatini.

Huku uraiani kwa sababu mtu ni dokta anaonekana nusu mungu. Watu wanaamini kila atakachosema. Kumbe alishafungia akili kabatini siku nyingi.
 
Lakini kuelewa ni rahisi sana!!!mwenyekuelewa hapa ni mtu yeyote atakae tumia huduma za kibenki!!!practical?tutaelewa tu wala haihitaji shule kuuuuubwa!!!just cash in bank!!!
 
Back
Top Bottom