funaku
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 39,124
- 31,645
Muda ni muamuzi mzuriTujipe muda mkuu
Muda ni muamuzi mzuriTujipe muda mkuu
Gazeti la Mwananchi: Wakati TRA ikiitaka BOT izichukulie hatua bank zilizotangaza kuongeza gharama za huduma za kibenk, BOT imesema mabenki yapo sawa!
Prof.Ndulu anasema mabenk watakuwa mawakala wa TRA tu katika kukusanya VAT lakini si walipaji,kwa hiyo hawezi kuwachukulia hatua.
Beno Ndulu ametolea mfano unapokua unauza duka unakuwa wakala tu wa TRA na sio mlipaji.....KUMEKUCHA
View attachment 362128
TRA jana na waandishi wa habari walipinga ongezeko hilo la gharama za kifedha kwa wananchi iliyofanywa na mabenki wakisema ni upotoshaji na kutaka BOT iwashughulikie
Ni kweli kabisa kwa haya unenayokitendo cha ile kodi kuiita VAT,Basi mzigo unaenda moja kwa moja kwa mlaji.Labda ibadilishwe jina na isiwe VAT.Profesa yuko sahihi.TATIZO HII NCHI KWA SASA MAAMUZI YA TULIOWAPA DHAMANA YANATOLEWA KWA HOFU YA KUTUMBULIWA.
Sa faida ya benki ikipungua na corporate tax si itapunguaHapa ilitakiwa serkall iseme makato yanayofanywa na benki ni makubwa
Mfano kama ni tshs 1000
Basi kuanzia julaii makato yabaki ni 1000 na katika hiyo 750 iende bank na 250 iwe kusanyo la kodi.
Hapo bado anayelipa kodi bado ataendelea kuwa mlaji na faida kubwa ambayo benk ingepata itapungua
Maana yangu hapo ni kwamba kila mkuu wa idara anajitokeza katika vyombo vya habari ili aonekane kwa mkulu anafanya kazi asije akatumbuliwa. Hakuna weledi.Mkuu acha wajae hofu ili mali zetu zipone
utekelezaji umeenza baadhi ya benki zimewataarifu wateja juu ya VAT mi mwenyewe nimestushwa kuona tasisi kubwa sana za baba moja serikali zikitofautiana juu ya VAT walikuwa wapi kufafanua kabla ya kupitishwa bungeni.au ni hofu ndo wanaogopa kutumbuliwa.ni heri ukatumbuliwa ukiwa unasimamia ukweli kuliko kunyamaza na kusubiri matokeo hasi ndo utoke kufafanua kweli inakuweka huru inakulinda sijui watamuaje maana huduma za benki zitakuwa garama kwa wateja na watu watakwepa kutumia benkSwali la msingi ni Je wizara husika walipopitisha kodi hii waliwashirikisha BOT,TRA na wahusika wengine kama watendaji wa juu wa Benki zilizopo Tanzania ili kufikikia makubaliano ya utekelezaji wa makusanyo haya?
Inashangaza kuona mamlaka mbili zilizopo chini ya serikali moja kutoa matamko tofauti kwenye swala moja linalowagusa/kuwaunganisha wakati utekelezaji wa maamuzi ya serikali umeshaanza na unawagusa wananchi moja kwa moja.
Kwa nini gavana wa BOT ama mabenki hawakutuonya/kutoa tamko kabla ya makusanyo hayo kuanza? Au hawakushirikishwa katika hatua za awali za uundaji wa utaratibu huu mpya wa ukusanyaji kodi na hivyo hawakuwa na namna ya kuzuia mfumo huo zaidi ya kukubaliana nao na kuhamishia gharama kwa mteja.
Either way hii haijakaa vizuri kwa serikali maana wananchi ndio wanaachwa katikati hawajui washike tamko la nani, cha msingi ni kujiandaa kisaikolojia kwa lolote sitashangaa nikisikia benki zilizopandisha tozo kufungiwa ama kunyang'anywa leseni maana lolote linaweza kutokea kutokana na maamuzi ya viongozi wetu ambayo hayajaona/hayajatambua madhara kamili ya utekelezaji wake.
Duuuu......mpaka watu waelewe hii kitu Kazi ipo...ila hapa shida inakuja pale unapoingiza siasa kwenye ishu za kitaalamu...umeeleza weeeee...ila ukweli utabaki pale pale...Tozo (fees/charges) wanazotoza benki kama vile makato ya kila mwezi, ATM withdraw fees, nk zinalipwa na mtumiaji wa huduma za benki (mteja wa benk). Serikali inachosema ni kuwa hizo fees kwa sasa zitakuwa na VAT (inclusive VAT) yaani ndani yake kutakuwa na 18% ya serikali.
Mfano: Kama gharama ya kutoa fedha kwenye ATM ni shs 1,000 fedha yote hii ilikuwa inachukuliwa na benki. Kwa utaratibu mpya ni kuwa fedha hiyo sasa benki watailipa serikali 18%, yaani benk watachukua shs 847 na Serikali watachukua shs 153 kama kodi ya ongezeko la thamani, VAT. Utaona kuwa gharama kwa mtumiaji wa benki inaendelea kuwa ile ile shs 1,000.
Utaratibu huu benki hawataki kwa sababu utapunguza mapato yao ya hizo tozo kwa 18%. Benki wanachotaka ni kuwa waongeze 18% kwenye tozo wanazotoza saa hivi, yaani kwenye 1000 waongeze 18% na kuwa sh 1180 na hivyo kusukuma hilo ongezeko kwa mtumiaji wa mwisho wa huduma za benki kwa ongezeko la gharama za huduma za benki.
Mpaka sasa benk wanawatoza wateja wao gharama kubwa na wanachokirudisha kwa wateja wao kama riba ni kidogo sana, riba ya mkopo wa benki ni kati ya 20% hadi 25% kwa mwaka lakini ukiweka fedha zako benki utapata riba ya kati ya 2% na 6%, bado hizo fedha wanazifanyia biashara na kupata faida kubwa. Utaona kuwa hata hizo fees hazikupaswa kuwepo na kama zinapaswa kuwepo zinatakiwa ziwe kidogo sana.
Benki zetu haziko tayari kuwasaidia wateja wao kujikwamua na hali ngumu ya maisha badala yake wamekuwa zikandamiza wateja wako. Nashangaa hata huyo Prof wa BOT anawasapoti ili hiyo 18% iende kwa watumiaji wa mwisho (wateja wa benk).
Tukumbuke serikali imeweka kodi, 18% kwenye fees ambazo benki tayari walikuwa wanazikusanya lakini walikuwa hawazilipii kodi.
Tozo (fees/charges) wanazotoza benki kama vile makato ya kila mwezi, ATM withdraw fees, nk zinalipwa na mtumiaji wa huduma za benki (mteja wa benk). Serikali inachosema ni kuwa hizo fees kwa sasa zitakuwa na VAT (inclusive VAT) yaani ndani yake kutakuwa na 18% ya serikali.
Mfano: Kama gharama ya kutoa fedha kwenye ATM ni shs 1,000 fedha yote hii ilikuwa inachukuliwa na benki. Kwa utaratibu mpya ni kuwa fedha hiyo sasa benki watailipa serikali 18%, yaani benk watachukua shs 847 na Serikali watachukua shs 153 kama kodi ya ongezeko la thamani, VAT. Utaona kuwa gharama kwa mtumiaji wa benki inaendelea kuwa ile ile shs 1,000.
Utaratibu huu benki hawataki kwa sababu utapunguza mapato yao ya hizo tozo kwa 18%. Benki wanachotaka ni kuwa waongeze 18% kwenye tozo wanazotoza saa hivi, yaani kwenye 1000 waongeze 18% na kuwa sh 1180 na hivyo kusukuma hilo ongezeko kwa mtumiaji wa mwisho wa huduma za benki kwa ongezeko la gharama za huduma za benki.
Mpaka sasa benk wanawatoza wateja wao gharama kubwa na wanachokirudisha kwa wateja wao kama riba ni kidogo sana, riba ya mkopo wa benki ni kati ya 20% hadi 25% kwa mwaka lakini ukiweka fedha zako benki utapata riba ya kati ya 2% na 6%, bado hizo fedha wanazifanyia biashara na kupata faida kubwa. Utaona kuwa hata hizo fees hazikupaswa kuwepo na kama zinapaswa kuwepo zinatakiwa ziwe kidogo sana.
Benki zetu haziko tayari kuwasaidia wateja wao kujikwamua na hali ngumu ya maisha badala yake wamekuwa zikandamiza wateja wako. Nashangaa hata huyo Prof wa BOT anawasapoti ili hiyo 18% iende kwa watumiaji wa mwisho (wateja wa benk).
Tukumbuke serikali imeweka kodi, 18% kwenye fees ambazo benki tayari walikuwa wanazikusanya lakini walikuwa hawazilipii kodi.
Dr mpango kashtuka amejichanga,sasa amebadili gear anganikibaya zaidi wanajichanganya changanya,Mpango anaiita excise duty,TRA wanaiita VAT lakini mzigo mnamdondokea Taasisi ya Fedha(Kituko hiki) na BOT nao wanasema hii mzigo unaenda kwa mlaji(final consumer)..Yaan ''vurugu mechi''...
Bank Charges Haziepukiki,ziwe na kodi ndani yake ama zisiwe na kodi ndani yake.Kumbuka Zile ni sehemu ya gharama unazotozwa kwa huduma unazopata za kibenki.Sasa kama Serikali yako haikuwa inatoza chochote kwenye charge hizo si kosa la Benki ama jukumu la benki kuiambia Serikali iwacharge.Na vyovyote vile,Tozo hiyo ikiitwa VAT basi automatically jukumu linakuwa kwa mlaji,na hata iwe excise duty nyingine,Mabenki yatatafuta namna ya kuongeza mzigo kwa wateja kwa kigezo cha kupanda kwa gharama za uendeshaji.
Value-Added Tax (VAT) is a tax on consumer spending. It is collected by VAT-registered traders on their supplies of goods and services effected within the State, for consideration, to their customers.kwishaaaa!!!!Naona umejitahidi kuchangia lkn I hope uelewi unachoandika kama unao ufahamu wa kutosha on how these things are operating