Tozo (fees/charges) wanazotoza benki kama vile makato ya kila mwezi, ATM withdraw fees, nk zinalipwa na mtumiaji wa huduma za benki (mteja wa benk). Serikali inachosema ni kuwa hizo fees kwa sasa zitakuwa na VAT (inclusive VAT) yaani ndani yake kutakuwa na 18% ya serikali.
Mfano: Kama gharama ya kutoa fedha kwenye ATM ni shs 1,000 fedha yote hii ilikuwa inachukuliwa na benki. Kwa utaratibu mpya ni kuwa fedha hiyo sasa benki watailipa serikali 18%, yaani benk watachukua shs 847 na Serikali watachukua shs 153 kama kodi ya ongezeko la thamani, VAT. Utaona kuwa gharama kwa mtumiaji wa benki inaendelea kuwa ile ile shs 1,000.
Utaratibu huu benki hawataki kwa sababu utapunguza mapato yao ya hizo tozo kwa 18%. Benki wanachotaka ni kuwa waongeze 18% kwenye tozo wanazotoza saa hivi, yaani kwenye 1000 waongeze 18% na kuwa sh 1180 na hivyo kusukuma hilo ongezeko kwa mtumiaji wa mwisho wa huduma za benki kwa ongezeko la gharama za huduma za benki.
Mpaka sasa benk wanawatoza wateja wao gharama kubwa na wanachokirudisha kwa wateja wao kama riba ni kidogo sana, riba ya mkopo wa benki ni kati ya 20% hadi 25% kwa mwaka lakini ukiweka fedha zako benki utapata riba ya kati ya 2% na 6%, bado hizo fedha wanazifanyia biashara na kupata faida kubwa. Utaona kuwa hata hizo fees hazikupaswa kuwepo na kama zinapaswa kuwepo zinatakiwa ziwe kidogo sana.
Benki zetu haziko tayari kuwasaidia wateja wao kujikwamua na hali ngumu ya maisha badala yake wamekuwa zikandamiza wateja wako. Nashangaa hata huyo Prof wa BOT anawasapoti ili hiyo 18% iende kwa watumiaji wa mwisho (wateja wa benk).
Tukumbuke serikali imeweka kodi, 18% kwenye fees ambazo benki tayari walikuwa wanazikusanya lakini walikuwa hawazilipii kodi.