Makamura
JF-Expert Member
- May 19, 2022
- 356
- 550
Nyota huyo wa zamani wa Uingereza, ambaye sasa ni mmoja wa watangazaji maarufu zaidi kwenye Kituo cha utangaji cha BBC, alituma tena chapisho la Kampeni ya Palestina ya Kususia Kielimu na Utamaduni ya Israeli (PACBI) kwenye X, ambayo zamani ilikuwa Twitter.
Katika Chapisho Hilo, PACBI ilitoa wito wa "shinikizo la kimataifa la umma na rasmi kwa mashirika ya kimataifa ya michezo" - ikiwa ni pamoja na shirikisho la soka la FIFA na Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki (IOC) - kusimamisha uanachama wa Israel na kuipiga marufuku kushiriki mashindano na michezo ya kimataifa.
Kundi hilo la (BDS: affiliated with the wider Palestinian-led Boycott, Divestment and Sanctions movement), lilitoa wito wa kususia "hadi Israel itakapomaliza ukiukaji wake mkubwa wa sheria za kimataifa, hasa utawala wake wa kibaguzi na uhalifu wa mauaji ya kimbari inayoendeleza huko Gaza.