Freeman Mbowe anamiliki jumba la kifahari Dubai!

Freeman Mbowe anamiliki jumba la kifahari Dubai!

Ishu si umiliki wa nyumba kwamba ni yake au sio yake, mjadala hapa ni kwa nini malipo yalifanyika in cash. Kama alilipa kupitia bank basi athibitishe hilo kuwa hakulipa kwa cash.

una ushahidi kuwa ni cash system.na umejiridhisha kama malipo yalikuwa bank kutumia kampuni zake za nje,labda we na tume yako ya kondefu mseme kuwa kwa nini mmeleta mambo yasiyoiusu fedha uswis tena kabla ya wakati
 
Fredrick alisoma UK zaidi ya miaka 10 iliyopita, hii habari ndio kwanza inatoka? Also Fred sio mjinga kucheza na mapesa kiasi hicho, habari hii ni zile tunazozungumza huku tukipata gahwa
 
una ushahidi kuwa ni cash system.na umejiridhisha kama malipo yalikuwa bank kutumia kampuni zake za nje,labda we na tume yako ya kondefu mseme kuwa kwa nini mmeleta mambo yasiyoiusu fedha uswis tena kabla ya wakati
umeandika upumbavu gani huu?? kwa hiyo ni sahihi mbowe aibe fedha zetu akanunue majumba dubai ila namna anayotumia kusafirisha hizo fedha ndio iwe siri yake?
 
Kutokana na mjadala ambao
tayari umeshawekwa hapa na kujadiliwa kwa siku mbili mfululizo ,
nimeona kuwa kuna watu wanafanya propaganda badala ya kujaribu
kuutafuta ukweli wa jambo lenyewe na kuangalia rationale ya jambo
linalojadiliwa .

Mimi niliamua kufanya jambo moja la kujaribu kuangalia nini alichokua
amedeclare Mbowe kwenye Tume ya maadili ya viongozi kwa mujibu wa Sheria
ya maadili ya viongozi wa umma , nimekuwa mambo yafuatayo na kama yupo
ambaye anaweza kunichallenge na aje a seem hapa na sio kuhangaika na
Gutter politics ,

Mbowe Freeman , kwenye fomu zake alideclare kuwa anamiliki nyumba kwenye
nchi zifuatazo,USA, UK, SOUTH AFRICA , DUBAI NA NAIROBI . Nyumba zote
hizo alionesha alizinunua lini na zipo maeneo gani kwenye nchi hizo ,

Aidha, kuhusu kumiliki Akounti ya Benki nje ya Nchi alionesha kuwa
anamiliki Akaunti iliyopo London Barclays Bank na nyingine iko Hull
City, na Benki moja USA .Ila hana Akaunti katika nchi ya Uswisi wala
kwenye offshore nyingine zozote zile .

vyote hivyo vipo kwenye fomu ya maadili ya viongozi , pia alionesha kuwa
Ana madeni kwenye mabenki mbalimbali ndani nanje ya nchi , na hii ni
kwa mujibu wa sheria .

Sasa hapo nimeona nisaidie kutoa ufafanuzi huu, na kama mtu unataka
unaweza kwenda pale tume ya maadili ya viongozi wa umma na unalipia
kiasi cha shilingi 1,000 tu na unapewa fomu hizo ila huruhusiwi kuondoka
nazo wala kupiga picha au kutoa nakala ya fomu (photocopy) .

hivyo , jukwaa kuendelea na kujadiliana kuhusu nyumba moja ya DUBAI , ni
vyema jukwaa likarudi kwenye heshima yake ya siku za nyuma ya kuwa
mbele ya waandishi kwa kwenda hatua moja mbele katika kuutafuta ukweli
wenyewe na sio kuendelea kulifanya jukwaa kuwa kama sehemu ya udaku.

Hivyo, basi badala ya kusubiria wakina Ezekiel Kimwaga , kuandika
taarifa za upande mmoja wanaotaka wao kuwa ni Mbowe, Rostam Na Ngeleja
tu ndio ambao waliombwa kusaidia timu hiyo katika kutafuta ukweli wa
fedha za Uswisi, ni kuwa wabunge wote walioongea siku ya mjadala huo
walihojiwa akiwemo Zitto Kabwe ambaye alihojiwa kwa saa nane na timu
hiyo, pamoja na wabunge wengine wengi na wafanyabiashara wakiwemo
mameneja wa Benki mbalimbali na wamiliki wa maduka ya fedha .

Ni Imani yangu kuwa kwa hili nimeweza kulisaidia jukwaa kuwa na mjadala
ambao ni focused , na turejee historia yetu ya kubwa mbele ya media
nyingine na sio kama ambavyo leo tunakuwa .........

Asante sana ndugu kwa taarifa yako na jitihada zako za kuutafuta ukweli

Dhamira yako inaendana na jina lako. Sasa tunaomba mods wai-update main post ili kuiweka thread hii kwenye mizania yake
 
WanaJF,
Nilieleza hapa jukwaani kuwa hatuhitaji propaganda. Hatua ya kwanza ni 1) mtupatie taarifa ya ukaguzi mliyofanya kwa Eecretariat ya Maadili ya Umma. Gharama ya ukaguzi haizidi 1,500. lipeni hizo fedha, kagueni file lake, ndiyo muwe na uhalali wa kupiga propaganda hapa. Hili si swala la " nadhani", oh sijui nini. Fsnyeni homework yenu, ndipo watanzania watawaelewa. Vinginevyo, tutawaonya wachochezi, wazushi, watu wadioitakia nchi hii mema, kwa kujaribu kutuondoa kutoka kwa mapambano halisi ya ufisadi na kutuwekea mapambano feki.

2. Wameisha kusema wengi, kuwa na nyumba nje ya nchi, au akaunti siyo kosa, kosa ni ufisadi hasa wa kutumia fedha za umma au kuziiba na au kuhukumu na kuzificha kwenye benki za nje, na hasa Offshore Banks Kama walivyofanya Mafisadi wa ccm kwa fedha za EPA, Tangold, Meremeta ambazo mpaka CCM na Serikali yake wameshindwa kuzitolea Taarifa, siyo humu jamvini, lakini hata Bungeni ambapo Serikali inapaswa kuwajibika. Haya hapa ni propaganda tu, na Kama nilivyosema kwenye post nyingine, hizi propaganda zimefeli hata kabla hazijaanza. Upotoshwaji wowote, ni lazima ujibiwe, tena kwa hoja, na Kama hoja Great Thinkers msiingie kwenye mtego wa kishabiki, jibuni kwa hoja Kama wana nia njema watawaelewa, kama hawataki " hata ukimpigia Gitta Mbuzi haitasaidia".
mzee, unataka ukaguzi upi? wewe na genge lako ndio mkafanye huo ukaguzi mkanushe kwa ushahidi kuwa mbowe sio fisadi ila hadi sasa huna mamlaka ya kupinga wizi uliofanywa na mbowe then akaenda kununua jumba dubai badala ya hata kuwekeza hapa nchini ili angalau basi watz wanufaike na kile alichokiiba kilichotokana na kodi zao...ruzuku!!!
slaa, bora ukae kimya kuliko kutetea ufisadi.pole sana kwa kuumbuka kwenu
 
una ushahidi kuwa ni cash system.na umejiridhisha kama malipo yalikuwa bank kutumia kampuni zake za nje,labda we na tume yako ya kondefu mseme kuwa kwa nini mmeleta mambo yasiyoiusu fedha uswis tena kabla ya wakati

Kukaa kimya ingekuwa vyema zaidi kuliko ulichoandika hapa.
 
niliipenda chadema ya kipindi cha akina chacha wangwe lakini hii ya kikanda zaidi sina imani nayo maana iko kijasiliamali zaidi.

Kama mbowe, ananunua nyumba dubai halafu anaandamanisha watanzania ili kikinuka yeye fasta dubai.

haha laumu baba zako na wazazi wake wa nyuma vingine tumetengenezewa na wazee wetu na kama amevikuta siku ya mwisho anatakiwa kuulizwa uliongeza vipi na ndio hizoza dubai ,holland,na mauri...kama ulikuwa hujui infact ukienda moshi wana hotel nanyakaterentege
 
nampongeza Mbowe kwa kuwa na nyumba nzuri, sawa na JK na viongozi wengine... nasikitikia mangula wa watu, kachoka hadi aavaa suti na adidas sijui nae kama ana jumba au ndio anajenga
Mkuu.....kirahisi kabisa.
Mbowe ni mfanyabiashara sku nyingi kitambo. Ana kampuni nje ya nchi - Dubai, ana nyumba SA, Uingereza na US.

Tatizo ni kwamba, ana tuhuma za wizi wa mali ya umma? ana mashtaka ya ukwepaji kodi au kavunja sheria ya kodi? yeye au makampuni yake?

Kama hapana, basi tuwe na reserve ya maneno.
Watanzania tumezidi wivu na maneno maneno tu.
 
Chadema wanahangaika na wanahamasisha watu wajitolee halafu pesa ya ruzuku mnakwenda kujengea nyumba na hati ya nyumba unaandika jina la mchumba wako hivi kweli ni akili au matope mwakani mtarudisha nyumba na gari chama anayotumia slaa.

Kweli magamba mnakazi sana, kumbe inawauma mnapoona chadema kinachangiwa na wanachama na wapendamaendeleo. Na bado 2015 tunachangisha kura zetu zote kwenda chadema alafu tuone mtaongea nini
 
duu naadhani huyu jamaa analipwa kwa kazi anayofanya,sidhani kama ana kazi kutwa yumo humu kusaka habari za jamaa zake

Na wewe muda wote unapokua ukinifuatilia nadhani unalipwa kufuatilia habari zangu
 
Kweli magamba mnakazi sana, kumbe inawauma mnapoona chadema kinachangiwa na wanachama na wapendamaendeleo. Na bado 2015 tunachangisha kura zetu zote kwenda chadema alafu tuone mtaongea nini

Isitoshe kwani ni vbaya au aramu kumiliki nyumba nje ya nchi. ata mimi ningekuwa na uwezo mkubwa mbona ningewekeza kila nchi?
 
Back
Top Bottom