Ukitazama picha ya mabondia tunaosubiri wapambane, kwenye picha wameainisha kila kitu ikiwa ni pamoja na urefu wao isipokuwa uzito wao hauonyeshwi japo walipima, sasa jiulize kwa nini? Japo uzito ni kigezo muhimu kwenye ndondi lakini wanaonyesha urefu na uzito unawekwa kapuni! Si kwa bahati mbaya, wanajua wanachokifanya, wanajua kabisa kuwa wameiburuza dunia iamini kuwa huu ni mpambano wa karne! Sasa katika mazingira hayo ukionyesha uzito wa mabondia wako ni kilo ambazo ni pungufu ya 70, utamaliza utamu wote na wale waliokuwa wanaburuzwa watashtuka! Naomba nieleweke, sidharau pambano na nawaheshimu mabondia husika ila kudai kuwa ni mpambano wa karne huo ni uongo wa hali ya juu, na haustahili kabisa kutikisa dunia na kufanywa wa gharama kiasi hicho! Ila wajanja wametumia kwa ustadi vyombo vya habari na wamepiga pesa kuliko unavyoweza kufikiri!! Huu ni mpambano wa wavulana tu wa kilo 64---67! hata kama wavulana wenyewe na mafundi wa ndondi,! Kamwe hauwezi kuwa mpambano wa karne! Kama huu ukiitwa mpambano wa karne, ule wa Tyson na Lewis tungeuitaje?