Finally: Hongereni Wana-CCM Online!!

Finally: Hongereni Wana-CCM Online!!

Status
Not open for further replies.
Duu!! Kaka uko sawa katika CIP yako kweli, maana sijui hata umejishutukia kitu gani kwani aliye-post wala hakusema wewe ni shoga sijui nini kimekusibu mpaka unahamaki...! Watch-out, this is JF bwana!!

- ha! ha! ha! ha! ha!ETi least wananchi hapa wana uhakika kwamba mimi kiongozi wao wa Taifa sio shoga, maana siku hizi Dunia imeharibika sana mnachagua kiongozi wa taifa kumbe shoga! ha! ha! ha!

- But in me what you see is what you get, kudadeki yaani Kiongozi Rijali! ha1 ha! ha! ha!

Le Mutuz!!
 
Mh: Nimegundua leo kuwa akili yako,umbo lako pamoja na umri ni tofauti sana, rudi nyumbani kavae
Omeona eeeh!!
I used to think the same.
Jamaa bado ni Premature kama sio mental retarded.

So sad kwa mzee Mallecela.
 
Hilo nalo neno mkuu. Nitake radhi, mimi ni CCM.....Ila unaniboa. William unammumiza mkeo na wanao. Grow up.... By the way, mkeo sasa hivi ni wifi yangu alafu wee pia ni shemeji...lol
MTOTO.jpg

like father like son.
 
Nikushauri tu kwamba jaribu kusoma na kutafakari ushauri wa Mchambuzi katika post #10 .
 
- Well, Brother nimekuwa ninakusoma kwa muda kidogo sasa, sina uhakika of what is your mission hapa JF maana wengine wote unaowaona humu wana mission, wengi wao ni wapambe wa Chadema wanaotaka kutuvuruga CCM at any cost. For you to say kwamba CCM imemeguka ni absolutely over reaching! mimi nilikuwepo Dodoma majuzi kwenye Mkutano wetu mkuu nimegombea NEC viti 10 na kupata kura 800 na kushika nafasi ya 12, kama kweli CCM ingekuwa imemeguka no way ningeweza kupata kura zote hizo!! kati ya kura 2,000!

Kwa hiyo woote wanaotetea vyama vyao hapa jamiiforums wana mission zao?kwa hiyo na wewe una mission zako hapa?kwa hiyo hauwapingi watu kwa hoja zenye ukweli bali una missio zako hapa jamiiforums?

- Sijui ni System gani unayoisema ambayo sio ya CCM, kwamba CCM tunaweza kusambaratishwa na Upinzani sijui ni Upinzani upi huo, maana nonaujua majuzi tu wamepigwa chini kwenye Udiwani na CCM, makundi ndani ya chama cha siasa ni kawaida sana, Tanzania tulichelewa sana kuwa nayo kwa sababu ya kutawaliwa na chama kimoja kwa muda mrefu sana, brother kumbuka maneno ya Mwenyekiti Mao, aliposema "Ukiona watu wawili wanakubaliana kwa kila kitu na kila wakati ujue kwamba mmoja wao ni mgonjwa au wote wawili ni wagonjwa" so it is ok kwa CCM kuwa na makundi kwa sababu hata Democrats kule US wanayo makundi so are Republicans!!

Kwa hiyo na hapa upo ktk mission zako?Yaani wapinzani wamepigwa chini?Willium ni ustaarabu gani unauonesha hapa?Penye matusi hapana hoja za msingi,ni kelele za mtu alieishiwa sera kichwani.Sio wewe ulikuja hapa jukwaani ukalalamikia rushwa imekithiri ndani ya chama chako?

- Sina uhakika na maelezo yako umefanyia wapi huo utafiiti, lakini binasfi ninaamini sana CCM, infact kama itaweza ku-maintain hii hype ya sasa, Wapinzani watakuwa na wakati mgumu sana 2015, infact ninasema hivi Wapinzani hawatashinda 2015, matokeo ni kwamba Chama cha wasi wasi kama Chadema kwa kukosa Urais, kitakufa kifo cha panzi!! Kwamba CCM ina kansa? hapana kumbe hujajua kwamba kansa ipo Chadema, kati ya Mbowe, Slaa na Zitto!

Si unaona mission zako hapa,uongo mtupu hapa.Hivi ni vita ipi ipo hapa kati ya hawa uliowataja?Vyama vya upinzani vipo vingi lakini ktk kichwa chako umeiona Chadema tu?Chadema inawaumiza vichwa sana ccm kila anaetaka kutoka lazima aimbe wimbo wa Chadema kama alivyofanya baba yenu Wasira.

- Halafu unapaswa kujua kwamba Chadema hawana mgomea imara wa Urais 2015, sasa watashindaje CCM iko vizuri sana wakorofi kina Mgeja umeona walivyoshugulikiwa na CC sasa hivi adabu mbele, waliotaka kupiga kura za maruhani ndio kabisaa yaani huzuni hata kusema, please brother naona na wewe unajaribu kuwa na mkono kwenye nyama na kwenye kunde CCM hatuhitaji wanachama kama wasio na msimamo kama wewe, kama umeona maji yamekushinda CCM nenda kwa usalama tu lakini wewe mtu mmoja huwaongelei wana CCM wote Millioni Tano!!

Hata katika masuala ya ya wizi wa pesa/wanyama wetu/madini yetu tunaona mnadili tu na dagaa,Chama kinachotekeleza ilani zake za uchaguzi huwa hakipotezi muda wa kupambana na wapinzani(wasiwasi-kama ulivyowaita).

- KIDUMU CCM!!

Le Mutuz!!

Ni lazima upigie debe kule unakula,tumeshashuhudia Lumumba namna mlipageuza uwanja wa mapambano kisa!!!!!!!!?
 
- Mimi nilidhani kwa elimu kubwa uliyonayo ungejali the Future of Chadema, kuliko a guaranteed Future ya CCM, ni majuzi tu nchi zote za Afrika Mashariki zimekubaliana kwamba kwa vile CCCM ni imara sana basi Chuo cha Kivukoni kifufuliwe na Mukama na kiwe kwa ajili ya Africa nzima, hivi hujasikia kwamba siku hizi vyama vyote vikongwe vya siasa Afrika vinakuja CCM kujifunza!

- I mean naomba ujali future ya Chadema maana upo kwenye njia panda sana!!

Le Mutuz!!

Sorry, nilikuwa namjibu Mchambuzina kwamba ieleweke mimi si mwanachama wa chama cho chote cha siasa kwa hoja zifuatazo.
  • Sitaki kushabikia rangi ya chama au bendera kama sina akili timamu
  • Sitaki kuwa pendera ya chama fulani
  • Uhuru wangu ndio ngao ya maisha yangu
  • Mimi ni mpenzi wa itikadi zenye kujenga wananchi kwa uadilifu na uaminifu si kwa hadaa.
  • Kujishikiza kwenye chama itakuwa mtumwa bila kutumia akili yangu ila kuitikia ndiyo ndiyo na kuwa mpiga vuvuzela
  • Uhuru wangu unanipa faraja kila sera nzuri zinapochipukia kuzikubali na mbovu zinapokosa soko siumii kukosa mshiko.
  • Kutofungamana na upande wo wote ila ubora ndiyo raha yangu, ndio maana kila kilicho bora kutoka chama cho chote siko na uchoyo ila kuwapa haki yao.
  • Kwa akili timamu na mwono mpana ni kujadili hoja si mtu ndivyo walio wapana wanavyofanya kama falsafa isemayo; "hajadiliwi mtu ila hoja." Kumjadili mtu binafsi ni dalili za kuishiwa nguvu ya hoja na hivyo kujiegemea kwenye hoja ya nguvu.
​
Mfano mimi nikianza kukuchambua ndugu William J Malecela kwa kuwa nakufahamu nitakuwa nimepungukiwa na kitu fulani kichwani kwani inanibidi nijijadili mwenyewe kwanza na dhana ya madhaifu yangu. Kinachotakiwa nijadili hoja yako na ndivyo ninavyofanya. Sawa nianze kuijadili familia ya Kikwete ni kosa kwa kuwa Urais ni mtu aliyechaguliwa si familia, na urais ni taasisi iliyo na misingi, sheria na taratibu zake ambayo kitakachojadiliwa ni system ya uongozi si Kikwete na familia yake, ndio maana Rais akishachaguliwa huunda jopo la viongozi mbalimbali ambao atasaidiana nao katika kuongoza nchi. Hivyo kianchojadiliwa kushindwa kwa CCM si Kikwete kama Kikwete, ila management system na ndicho kinachotakiwa kukfanyiwa kazi.
 
Mkuu naomba uendelee kutunza heshima yako mijadala kama hii ni too low for u. ur a GT
Unampamba bure! mijidala hii ni too low kwake? mbona ndiyo size yake hii! tena hata hivyo nadhani hapa amejitahidi angalau kuna vipoint kidogo japo vya kidarasa la saba hivi.

Labda kwa sababu anatumia jina halisi basi anaona inapendeza kuandika na kuongeaongea humu kwenye mitandao ili aonekane kwa wakubwa zake, pengine atafikiriwa kwenye nafasi ya Nape. Si unamjua mpenda madaraka huyu?

Ila mimi napendekeza tutoke huku kwenye key board tuende kwenye uwanja wa wazi kwenye media au tuwe na public talk, wanachadema na wanaCCM tuone nani anahoja. CCM yenyewe sasa hivi inakopi kila kitu kutoka CHADEMA, itakuwa na lipi jipya la kuwaambia wananchi? Hawa CCM walitakiwa wawe wanatulia tu ili kustiri aibu yao kuliko kukaa hapa na kuleta projo.
 
- Wewe wacha kuweweseka mimi ni bachelor sina mke so it is a fair game, so hata nikimuoa dada yako unakuwa rest assured kuwa ameolewa na Rijali! ha! ha! ha! ha!

Le Mutuz!!
Una miaka 51 bado hujaoa na bado unacheza na wasichana mtaani na unajiita kijana.
Tatizo ni nini hasa?
 
Hivi Kaka William,

Unajua kwamba chama chetu kimesha meguka ndani kwa ndani siku nyingi na tuna vyama zaidi ya viwili kimtazamo na kimalengo ndani ya CCM? Kinacho kosekana ni usajili wa tendwa; Isitoshe, viongozi wengi ndani ya CCM hawafanya kazi tena kwa mapenzi ya CCM, na hii ni hatari kwani wanasukumwa zaidi na UWOGA, UBINAFSI na UNAFIKI, masuala ambayo mwalimu aliyajadili sana jinsi gani ni tishio kwa uhai wa Chama;

Mimi ni Mwana CCM lakini kwa akili zangu timamu, naelewa kwamba kwa sasa CCM bado ni moja kwa sababu ya System tu, hakuna lingine; Chama kinacholindwa na system ni chama dhaifu;

Ni muhimu tukai sambaratisha CCM sasahivi kama nia yetu ni kuijenga upya, kuliko kusubiri kuja kusambaratishwa na Upinzani, kwani siku hiyo haipo mbali;

Hoja yako ya kutetea Chama chenye kansa ya kiungo ni hoja mfu kwani unachofanya ni kutetea na kuwa mtiifu kwa chama kwa mujibu wa katiba, sio kwa mujibu wa uhalisia wa soko la Siasa; Kaka, Kansa imesha sambaa, tukate tu hicho kiungo na tuanze maisha mapya;

Mkuu Mchambuzi,
Nakubaliana na pointi yako kuwa chama kimemeguka lakini pia sikubaliani na jinsi ulivyo generalise kuwa viongozi wote wanasukumwa na uwoga,ubinafsi na unafiki katika utendaji wa shughuli za chama. ninaamini ndani ya CCM kuna watu wanaofanya kazi bila kuwa na hayo na mmojawapo ni wewe. Hivi hujui kama wewe remotely ni kiongozi ndani ya CCM? Kwa yale unayoyaandika na kuyachangia hapa ukiikosoa CCM ni kazi tosha ndani ya chama kwa vile unakijenga chama

Hapo kwenye RED, nitafurahi ukinifafanulia vizuri unaposema kuisarambatisha CCM kwa sasa badala ya kusarambatishwa na upinzani
 
- Ahsante sana, ila ndugu yangu dalili za mvua huwa ni mawingu, uchaguzi wa udiwani majuzi ni ujumbe tosha kuhusu what to expect 2015 the budern is on the otherside sio kwetu CCM tena!!

Le Mutuz!!
Du mwalimu wako alipata shida kukufundisha, uchaguzi wa madiwani CDM hawakupoteza kata, ila nyie mmepoteza 2 kwenda chadema kama mlivyopoteza Arumeru Mashariki.
 
- Well, Brother nimekuwa ninakusoma kwa muda kidogo sasa, sina uhakika of what is your mission hapa JF
Nimekuwa mwanachama wa JF kwa miaka sita sasa na kabla ya hapo nilikuwa mwanachama wa Jamboforums; Na kote huku kuwili, wakati wa kujiunga, sikuwahi kukutana na kipengele kinachouliza MISSION YAKO KAMA MWANACHAMA NI NINI; Vinginevyo kwa uelewa wangu, huu ni uwanja wa kubadilishana mawazo na kupimana kwa hoja, kwa kujenga na kwa maslahi ya taifa letu, na ni hivyo ndivyo nimekuwa nafanya kwa miaka sita;

maana wengine wote unaowaona humu wana mission, wengi wao ni wapambe wa Chadema wanaotaka kutuvuruga CCM at any cost.
Kwa kauli hii, basi kumbe mission yako ni kuja kupambana na hoja za Chadema; Sasa nimekusoma; Naomba ujue kwamba mimi sio mwenzako katika hilo, badala yake nipo humu kubadilishana mawazo na wana chadema, wana ccm, wana CUF, NCCR n.k kwa manufaa ya taifa, na ikitokea tunapishana, mgongano wa mawazo ni suala la kawaida towards that end;

For you to say kwamba CCM imemeguka ni absolutely over reaching!
Kwa hili naishiwa hata nguvu ya kukujibu kwani hata mwenyekiti taifa amelizungumzia hili i.e. makundi; kama hauoni factions ndani ya CCM ya sasa na haukubaliani na mimi katika hili, basi mimi na wewe tunaishi dunia mbili tofauti kabisa; Vinginevyo unaweza kuwa sahihi na mtazamo wako, lakini nitaendelea kupingana na mtazamo huo;

mimi nilikuwepo Dodoma majuzi kwenye Mkutano wetu mkuu nimegombea NEC viti 10 na kupata kura 800 na kushika nafasi ya 12, kama kweli CCM ingekuwa imemeguka no way ningeweza kupata kura zote hizo!! kati ya kura 2,000!
Yani hiki ndio kipimo chako rasmi on whether CCM imemeguka au haijameguka? No wonder tunapishana mtazamo;

Sijui ni System gani unayoisema ambayo sio ya CCM
Ingekuwa sio ya CCM isingeisaidia CCM;

kwamba CCM tunaweza kusambaratishwa na Upinzani sijui ni Upinzani upi huo, maana nonaujua majuzi tu wamepigwa chini kwenye Udiwani na CCM,
Tuwe tuna chambua na matokeo, itatusaidia sana; Tumeshinda kata nyingi, pengine four times ya idadi ya kata walizoshinda Chadema lakini jumla ya idadi ya kura picha ni tofauti kabisa; hii inatuambia nini? Kura zetu CCM nyingi ni vijijini, Chadema ni Mijini; Na mwelekeo wa dunia ni urbanization ambapo ifikapo 2025, over 50% ya wakazi wa Africa, Tanzania ikiwemo watakuwa in urban areas; Are we investing for the future? Kwanini tunapoteza mvuto mijini? hazina yetu vijijini ni suala la muda tu;

makundi ndani ya chama cha siasa ni kawaida sana, Tanzania tulichelewa sana kuwa nayo kwa sababu ya kutawaliwa na chama kimoja kwa muda mrefu sana,
Ninachozungumzia mimi ni FACTIONS within the party ambazo mara kwa mara kumekuwa na jitihada za kuzikutanisha kama njia ya kuokoa chama kisipasuke; Factions sio jambo jema kwa uhai wa chama, whether kuna chama kimoja au vyama mia moja ndani ya demokrasia husika;

brother kumbuka maneno ya Mwenyekiti Mao, aliposema "Ukiona watu wawili wanakubaliana kwa kila kitu na kila wakati ujue kwamba mmoja wao ni mgonjwa au wote wawili ni wagonjwa" so it is ok kwa CCM kuwa na makundi kwa sababu hata Democrats kule US wanayo makundi so are Republicans!!

One British Conservative - Enoch Powell (1912) alipata nena kwamba: A Party... is not a faction or club of individuals who associate for mutual assistance in acquiring and retaining office; It is a body of persons who hold, advocate and desire to bring into effect certain political principles and policies".

Huyo Mao, na pia mifano yako juu ya Democrats na Republicans wanaongelea on the later, sio the former; Sisi tupo kwenye the former na ndio hoja yangu ya msingi katika hili;

Sina uhakika na maelezo yako umefanyia wapi huo utafiiti

Sijafanya any scientific research zaidi ya kuwa observant wa maendeleo mbalimbali hasa huku site; wewe je, kuna research umefanya?

lakini binasfi ninaamini sana CCM, infact kama itaweza ku-maintain hii hype ya sasa, Wapinzani watakuwa na wakati mgumu sana 2015
Ni vizuri kwamba umeweka a conditionality on this one i.e. kama itaweza..., na hii ni tofauti na hoja yako ya msingi kwenye bandiko namba moja; vinginevyo ushindi wetu sio straight forward tena kama zamani, na ndio maana Mwenyekiti ameona kuna utofauti kati ya Mukama na Kinana au Makamba na Kinana;

infact ninasema hivi Wapinzani hawatashinda 2015
Hii kauli kidogo inatoka so authoritative, kana kwamba ushindi wa CCM sio lazima upitie sanduku la kura;

matokeo ni kwamba Chama cha wasi wasi kama Chadema kwa kukosa Urais, kitakufa kifo cha panzi!! Kwamba CCM ina kansa? hapana kumbe hujajua kwamba kansa ipo Chadema, kati ya Mbowe, Slaa na Zitto!
Chadema ina kansa na sio CCM? Tukiendelea kulikataa hili, tutakuja aibika vibaya sana siku ya siku; Chadema is experiencing growth and increase in popularity kwa sababu ya madhaifu yetu CCM, na hata mwenyekiti kalisemea hilo; Wewe unaita hiyo ni Kansa?

Halafu unapaswa kujua kwamba Chadema hawana mgomea imara wa Urais 2015, sasa watashindaje
Kipimo cha Uimara ni nini? Sisi mgombea wetu ni yupi imara wa kuweza kukabiliana na nguvu ya Chadema ambayo sio ya dola bali ya UMMA? Tunamjua mgombea huyo? Tunamuandaa au tutampiga majungu hata kama ndiye angekuwa chaguo sahihi? I hope tutaachia nguvu za soko zitupatie mgombea imara kutoka CCM;

CCM iko vizuri sana wakorofi kina Mgeja umeona walivyoshugulikiwa na CC sasa hivi adabu mbele, waliotaka kupiga kura za maruhani ndio kabisaa yaani huzuni hata kusema
Mwenyewe unaanza kukubaliana na mimi kuhusu makundi ndani ya CCM ambayo hayana tija ingawa hapo awali ulileta hoja za Mao na Vyama vya marekani kwamba hivi ni vitu vya kawaida;

please brother naona na wewe unajaribu kuwa na mkono kwenye nyama na kwenye kunde CCM hatuhitaji wanachama kama wasio na msimamo kama wewe, kama umeona maji yamekushinda CCM nenda kwa usalama tu lakini wewe mtu mmoja huwaongelei wana CCM wote Millioni Tano!!
Hizi ndio kauli zenu CCM hata ngazi za juu, na mnajisahau kwamba milioni tano ilianza na moja; mtaendelea kupoteza watu wengi kwa kutokuwa tayari kusoma alama za nyakati; Vinginevyo hauna mamlaka ya kuniambia niende wapi kutumia haki yangu ya kikatiba katika masuala ya siasa; Lakini kama una mkono huko sijui wapi wa kuniondoa uanachama, na iwe hivyo; Mpaka muda huo ufike, rudi kwenye mwongozo wetu wa CCM (1982) ambao unasema hivi:

Ibara ya ( 5) Kujikosoa na kukosoana ni silaha ya Mapinduzi

58. Kuna mambo mawili tuliyojifunza ambayo ni muhimu pia kuyazingatia. La kwanza linahusu suala la kukosoa, kujikosoa na kukosoana kama njia ya kukijenga na kukiimarisha Chama na wanachama. Ni kweli kuwa katika TUJISAHIHISHE Mwalimu anasisitiza jambo hili na kwamba Katiba ya CCM inatamka waziwazi juu ya umuhimu wake. Lakini ni kweli pia kuwa hatujaijenga tabia hii ipasavyo. Mara nyingi tumependelea kuteteana, kufichiana makosa na hata kutafuta visingizio visivyo na msingi. Neno kuleana, kwetu sisi (ingawa kuna malezi mema na mabaya) limechukua nafasi ya kukosoana. Wanachama wenye upungufu husaidiwa kama wanakosolewa ili wajirekebishe...

59. Suala la kukosoa, kujikosoa na kukosoana lina sura kadhaa. Kwanza linataka wanachama na viongozi kuwa tayari kusema kweli katika vitendo vyao na kukubali kuambizana ukweli. Pili, linataka wanachama na hasa viongozi wawe tayari kukosolewa bila kuhamaki na inapobidi kukubali kujirekebisha. Tatu ni kuwa Chama chenyewe katika vikao vyake vya ngazi mbalimbali kuwa na utaratibu wa kujikosoa.

KIDUMU CCM!!
Matumaini yangu ni TUTADUMU unconditionally i.e. hata tukiwa chama cha upinzani bila ya kuwa na dola mikononi; in fact, kwa mtazamo wangu, tukianguka 2015 ndio tutajua ukweli kina nani wanakipenda chama kwa dhati na nani walikuwa wanatafuta tu maisha ya mkato mkato; Kaka, Je, ikitokea tumeanguka 2015 utaendelea kuwa mwanachama wa CCM? I hope jibu lako halitajirudia tena kwamba 'infact ninasema hivi Wapinzani hawatashinda 2015';
 
- Well, Brother nimekuwa ninakusoma kwa muda kidogo sasa, sina uhakika of what is your mission hapa JF maana wengine wote unaowaona humu wana mission, wengi wao ni wapambe wa Chadema wanaotaka kutuvuruga CCM at any cost.
...

- Sina uhakika na maelezo yako umefanyia wapi huo utafiiti, lakini binasfi ninaamini sana CCM, infact kama itaweza ku-maintain hii hype ya sasa, Wapinzani watakuwa na wakati mgumu sana 2015, infact ninasema hivi Wapinzani hawatashinda 2015, matokeo ni kwamba Chama cha wasi wasi kama Chadema kwa kukosa Urais, kitakufa kifo cha panzi!! Kwamba CCM ina kansa? hapana kumbe hujajua kwamba kansa ipo Chadema, kati ya Mbowe, Slaa na Zitto!

- Halafu unapaswa kujua kwamba Chadema hawana mgomea imara wa Urais 2015, sasa watashindaje CCM iko vizuri sana wakorofi kina Mgeja umeona walivyoshugulikiwa na CC sasa hivi adabu mbele, waliotaka kupiga kura za maruhani ndio kabisaa yaani huzuni hata kusema, please brother naona na wewe unajaribu kuwa na mkono kwenye nyama na kwenye kunde CCM hatuhitaji wanachama kama wasio na msimamo kama wewe, kama umeona maji yamekushinda CCM nenda kwa usalama tu lakini wewe mtu mmoja huwaongelei wana CCM wote Millioni Tano!!

- KIDUMU CCM!!

Le Mutuz!!

Mkuu,
Umeshasema makundi kwenye chama ni kitu cha kawaida, Kama mchambuzi ni mwana CCM lakini hakuvaliani Na baadhi ya mambo kwenye chama kama Ufisadi Au haungi mkono baadhi ya viongozi ndani ya chama asiseme?

Mkuu mbali Na mchambuzi kuna hata viongozi wakubwa au makada ndani ya chama hawakubaliani na vitendo vya kifisadi au kujihusisha na biashara ya nyara za taifa. Sasa hivi makundi ya urais ndani ya CCM ni dhahiri hata mwenyekiti wako anakiri na anajua ndio bomu litakalopasua CCM.

Kwa taarifa yako Mkuu huwezi ukaondoa tatizo lililopo kwa kulikataa tu kwamba halipo wakati hujalitatua.

Ni kweli na ni dhahiri kwamba CCM Ina makundi ambayo tayari ni nyufa na mpasuko ni lazima. Alichoshauri Mchanbuzi bora huo mpasuko utokee sasa hivi na huenda itanusuru chama kwa sababu itaondoa mafisadi au watu ambao hawafai Na chama kunusurika kuliko kusubiri kusambaratishwa na upinzani-great thinking.

Mkuu, Kwa mtazamo wako ni kwamba mwanachama mzuri ni anayekubali kila kitu kama kondoo-hii ni low thinking!

Mkuu Usitegemee kwamba kwa njia hii unayoifikiria itaimarisha chama chenu,

Sana sana chama chako kitaendelea kutegemea msaada wa vyombo vya dola. Lakini Mkuu, kwa taarika yako hata vyombo vya dola vimeshagawanyika. Watu wamechoka na Ufisadi wanataka Maendeleo.

Wewe uko huko CCM kwa sababu familia yako Na wewe binafsi mnafaidika na mfumo wa kifisadi uliopo. Lakini Mkuu, wafikirie ndugu watanzania zaidi ya asilimia 99 wanaoteseka na huu mfumo wenu.

Pamoja na kwamba mi si mwanachama wa CCM lakini najua kwamba kama ufisadi usingekuwepo na kuwa sera ya CCM, maendeleo yangetufaidisha wote kama watanzania.

Mkuu, hakuna utawala dhalimu usio na mwisho, Jisafisheni kwa matendo bila hadaa ya kudanganya wananchi la sivyo hatimaye NGUVU YA UMMA itawakumba
 
Nijuavyo mimi, Wanachama wa CCM wapo vijijini na ndiko CCM hupatia ushindi huko, lakini huko vijijini hakuna umeme wala computer, hili la kupongezana kwamba mpo online mbona sijalielewa?.
 
mpira si chenga bali magoli, na uchaguzi autizami tu ongezeko la kura bali viti, kati ya 29 mnashinda 5, halafu mnajisifia?

sema hivi . . . Kati ya 29 vya CCM, 5 vimechukuliwa na CDM!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom