wenye JF yenu
Moderator msiunganishe hii na ile Special Thread ya Barca, hapa ni kwa ajili ya mechi ya leo tuu!
eebana leo mishale ya saa nne usiku, pale Camp Nou, Barcelona itakua Nyumbani dhidi ya Internationale milan, hii ni bonge moja ya mechi, kwani inter hii ya Antonio conte ni ya moto sana!!
Je, ernesto valverde atapata ushindi mbele ya muitaliano Antonio conte!?
Barcelona ikichagizwa na wachezaji machachari kama Left back Jord alba, beki kama Pique, na mamidlfild wakali kama Frankie de Jong, Busquets na Mbrazil Arthur, ikichagizwa na washambulia makini kama Suarez, Antoine Grizmann, kinda Ansu Fati na baba yao LM10.
je itashinda mbele ya kikosi cha inter kilichosheheni mastar kama Marcelo Brazovic, Alexis Sanchez, Skriniar, Central Midfild kama Sensi, D'ambrosio na mabek hatari Kama Stefan de vrij na diego godin?
Tukutane kibanda umiza!