Kaka acha kulinganisha international flight na local.. Mfundishe huyu
Tiba ajue kwamba international wanasaidia wanaochelewa but local airline haiwezekani maana wanakodisha madirisha ya check in
Binafsi ni mteja mzuri sana wa fast jet na nitaendelea kuwa mteja wao kwa sababu nimeyakubali mapungufu yao.. Na ukilinganisha Fast jet na precision fast jet wana mapungufu machache kuliko precision.. Muhimu ni kuelewa terms and condition zao vizuri...
Terms za fast jet reporting time ni 3 hours before departure na ukichelewa sana watakusaidia lakini mwisho wa kufanya check in ni 40 minutes before departure.. So kwa kigezo hicho mtoa mada alichelewa check in..
Na wanafanya hivyo sababu Fast jet hawana dirisha la check in kama qatar au emirates. Wao wanachofanya wanaazima dirisha kwa ajili ya check in na ndio maana wanasema dakika 40 before safari hawawezi kusaidia wacherewaji sababu muda wa kukodisha dirisha unakuwa umeshaisha...
Binafsi nilishachelewa Qatar airways nakumbuka ilikuwa tarehe 24/6/2012 pale JNIA na tulifika saa sita kama na nusu hivi wakati ndege inaondoka saa 7 lakini kwa huruma walikuja wafanyakazi wao wakawasha computer za check in, wakatuprintia sticker za bags.. Tukachekiwa airport fasta na tukaingia kwenye ndege na kuondoka na hii iliwezekana sababu wao wana dirisha lao maalumu pale airport hawakodishi na wana haki ya kuwasha computer muda wowote tofauti na fast jet wanaotegemea Swissport..
Ukichelewa local airline imekula kwako lakini ukichelewa international airline unaweza ukaeleweka na kuwashiwa computer for check in maana wanajua wao wanatembea kwa Connections kwenye hubs zao so wakikuacha wanajua utateseka sana kwenye connection maana kuna miji mingine hazina connection flights za kila siku so lazima upandishwe ndege tu ili wakuokoe ukaiwahi connection yako