Familia ya Neema aliyedai badilishiwa mtoto yakataa kata kata kupokea mwili wa Marehemu kuzika, Yadai yule si mtoto wao

Familia ya Neema aliyedai badilishiwa mtoto yakataa kata kata kupokea mwili wa Marehemu kuzika, Yadai yule si mtoto wao

Carlos The Jackal

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2017
Posts
28,749
Reaction score
91,814
Familia ya NEEMA inaendelea kusisitiza, Nurse Kwa mara ya Kwanza alimletea NEEMA mtoto akiwa kwenye Kanga nyingine ( Hapa Mtoto anaweza kua alikua ndie ila tu Kanga zilichanganywa).

Baada ya NEEMA kuhoji Kanga si zake, mtoto huyu Ndani ya kanga zisizo za NEEMA, akarudishwa Kwa Mzazi mwingine aitwaye Mariam Binti wa Miaka 18.

Kisha Mtoto aliyekua Kapewa Binti Mariam, ndio akaletwa Kwa NEEMA sasa akiwa Ndani ya Kanga za Neema.


Inasemekana, Binti Mariam mwenyewe anasema baada ya Kujifungua aliambiwa kua Mtoto wake ana shida za Upumuaji !!.


View: https://youtu.be/mZksznhQXXg?si=ufwtgOowAFhH7wfn


Kilichotokea katika Sakata hili ni sawa na CCM dhidi ya No Reforms No Elections.


Kwamba DNA Iseme mtoto wa Marehem kweli sio wa NEEMA?. Ili Jamii ianze kua na mashaka na kuleta mtafaruku?.


CHADEMA IMSAIDIE HUYU NEEMA, DNA irudiwe Upya Nje ya Nchi !! .
 
Dada anataka aambiwe mwanawe amepata shida akiwa yuko kwenye chumba cha upasuaji uelewa apa n shida na mama anaonekana ndo mwenye shida apa anamfundisha bint yake vitu ambavyo si sahihi
 
Dada anataka aambiwe mwanawe amepata shida akiwa yuko kwenye chumba cha upasuaji uelewa apa n shida na mama anaonekana ndo mwenye shida apa anamfundisha bint yake vitu ambavyo si sahihi
Acha kuchukulia mambo kimihemko!!, Kwahiyo hicho ndio kinafanya nessi abadili kanga ya mtoto!. Mount MERU wamekuwa na shida hizi sio leo.... Wanahusika sana kuuza na kupoteza watoto wa watu.
 
Acha kuchukulia mambo kimihemko!!, Kwahiyo hicho ndio kinafanya nessi abadili kanga ya mtoto!. Mount MERU wamekuwa na shida hizi sio leo.... Wanahusika sana kuuza na kupoteza watoto wa watu.
Mim na wew nan anaongea kimihemko majibu si walishapewa ya DNA na mkemia mkuu sasa shida yao bado nn nyie mnaomsapot uyu mama ndo mnamjaza ujinga mchanhien bas akafanye Dna south au kenya
 
Mim na wew nan anaongea kimihemko majibu si walishapewa ya DNA na mkemia mkuu sasa shida yao bado nn nyie mnaomsapot uyu mama ndo mnamjaza ujinga mchanhien bas akafanye Dna south au kenya
Mtoto wa kwanza aliyemzaa alikuwa na kilo tatu na gram 1 Kama sikosei ndivyo alivyodai huyu wa pili anayemkataa ana kilo mbili na gram kadhaa halafu ni dhaifu jumlisha na hiyo kanga yeyote asingempokea haki itendeke kwa huyu mama, Mount Meru wanajua mtoto alipo.
 
Dada anataka aambiwe mwanawe amepata shida akiwa yuko kwenye chumba cha upasuaji uelewa apa n shida na mama anaonekana ndo mwenye shida apa anamfundisha bint yake vitu ambavyo si sahihi
Kuna muda ni bora tu ukae kimya kuliko kubwabwaja ugoro ukaishusha hadhi yako.
 
Hapo kqenye kilo 3 na kilo 2 ndo kunaleta shida
 
Kwamba DNA Iseme mtoto wa Marehem kweli sio wa NEEMA?. Ili Jamii ianze kua na mashaka na kuleta mtafaruku?.
Reputation ya MOUNT MERU Hospital ndio inalindwa hapo, in the expense of Mtoto wa Neema.

Yaani ni bora Neema asipate mwanae, ila Hospital iendelee kuaminika(Watu wanalinda UGALI wao).

Nafikiri hawa wangedai mtoto nje ya vyombo vya habari, wangepewa mapema sana. Ila hapo sasa hivi majibu yakiwa alibadilishwa, UGALI wa wafanyakazi wengi hapo utamwagika.
 
nje ya media si hata wangeuliwa kabisa, media imewasaidia hata wapimwe dna.
Reputation ya MOUNT MERU Hospital ndio inalindwa hapo, in the expense of Mtoto wa Neema.

Yaani ni bora Neema asipate mwanae, ila Hospital iendelee kuaminika(Watu wanalinda UGALI wao).

Nafikiri hawa wangedai mtoto nje ya vyombo vya habari, wangepewa mapema sana. Ila hapo sasa hivi majibu yakiwa alibadilishwa, UGALI wa wafanyakazi wengi hapo utamwagika.
 
Shida ni ofisi ya mkemia mkuu wakati mwingine unawaza hivi wale wanaofanya kazi mule ndani Wana weledi kiasi Gani?
 
DNA ya kweli iko ulaya kwa watu serious huku afrika tunataniana tu!
 
nje ya media si hata wangeuliwa kabisa, media imewasaidia hata wapimwe dna.
Unalosema ni sahihi pia, endapo kama hilo jambo walikusudia. Kweli wangeweza kuwaua.

Ila kama ilikuwa ni bahati mbaya au uzembe mdogo, basi wangepewa tu mtoto bila shida yeyote nje ya MEDIA.

Kitendo cha kwenda kwenye MEDIA, kinaweza wanyima haki kwasababu ya attention. Matokeo yoyote yatayokuwa upande wa Neema, yataondoka na vibarua vya watu. Iwe walifanya Uzembe, bahati mbaya au Makusudi.

Serikalini mkuu kuna watu huwa wapo tayari kupoteza uhai ili kulinda tu vibarua vyao, watu wana akili za ajabu sana kwenye utumishi wa umma.

Kuna mpuuzi aliwahi leta uzito uhamisho ya ndugu yangu fulani, nilimpa namba yake katibu aliyenifanyia mchakato aongee nae yule afisa utumishi. Kitu alichomfanya ni cha hovyo hadi mimi nilikuja tena kuwa msuluhishi. VIBARUA watu wanavilinda kwa DAMU na JASHO.
 
Unalosema ni sahihi pia, endapo kama hilo jambo walikusudia. Kweli wangeweza kuwaua.

Ila kama ilikuwa ni bahati mbaya au uzembe mdogo, basi wangepewa tu mtoto bila shida yeyote nje ya MEDIA.

Kitendo cha kwenda kwenye MEDIA, kinaweza wanyima haki kwasababu ya attention. Matokeo yoyote yatayokuwa upande wa Neema, yataondoka na vibarua vya watu. Iwe walifanya Uzembe, bahati mbaya au Makusudi.

Serikalini mkuu kuna watu huwa wapo tayari kupoteza uhai ili kulinda tu vibarua vyao, watu wana akili za ajabu sana kwenye utumishi wa umma.

Kuna mpuuzi aliwahi leta uzito uhamisho ya ndugu yangu fulani, nilimpa namba yake katibu aliyenifanyia mchakato aongee nae yule afisa utumishi. Kitu alichomfanya ni cha hovyo hadi mimi nilikuja tena kuwa msuluhishi. VIBARUA watu wanavilinda kwa DAMU na JASHO.
Hawa wamekuja kwenye media baada ya kuona hawapati walichohitaji. Media siku hizi ni kimbilio na sio mahakamani au polisi.

Ukipata huruma ya jamii haki yako inawahishwa, akitokea mwanasiasa akaingilia hilo sakata watu vibarua vitaota nyasi mapema sana.
 
Hapa inawezekana manesi walijichanganya.

Inawezekana kabisa huyo mtoto waliopewa ndio wao.
 
Acha kuchukulia mambo kimihemko!!, Kwahiyo hicho ndio kinafanya nessi abadili kanga ya mtoto!. Mount MERU wamekuwa na shida hizi sio leo.... Wanahusika sana kuuza na kupoteza watoto wa watu.
Inabidi tukapime DNA za mababu zetu, wazazi wetu, watoto wetu, wajukuu wetu na vitukuu vyetu.

CCM hawataki hii itokee, utakuta Chid Benz ni mtoto wa Mheshimiwa fulani na mtoto aliyelelewa na huyo Mheshkmiwa ambaye sasa ni Meneja wa Benki fulani, nk sio mtoto wake.
 
Hizi nchi za kijamaa na kishoshalist anything can happen, usikute hapo watu wamebadirisha kweli na wanakomaa ili kulinda reputation na Hospital. Yaani hizi nchi za kijamaa serikali haipaswi kukosea..
Huyo Glory hua msala anao duuh!
Kama mtu anaweza kuuliwa mjini kabisa, serikali ikapiga kimya, ishindwe kupiga kimya mtu kubadirishiwa mtoto...??
Ndo shida ya kuua TRUST hii. ONCE TRUST IS BROKEN IT IS FINAL..na ndo kinachotokea kati ya serikali na wananchi wake, imagine huyo mama anasema kabisa waende nje ya nchi mwa ajili ya DNA..maana yake hapa chenga..
 
Mim na wew nan anaongea kimihemko majibu si walishapewa ya DNA na mkemia mkuu sasa shida yao bado nn nyie mnaomsapot uyu mama ndo mnamjaza ujinga mchanhien bas akafanye Dna south au kenya
Wana uwezo Sasa wa kusafir nje ya nchi kufanya hio DNA ?

Umaskin mbaya
 
Acha kuchukulia mambo kimihemko!!, Kwahiyo hicho ndio kinafanya nessi abadili kanga ya mtoto!. Mount MERU wamekuwa na shida hizi sio leo.... Wanahusika sana kuuza na kupoteza watoto wa watu.
Dna si imetoa majibu ?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom