Fahamu upande wa pili wa Dangote

Fahamu upande wa pili wa Dangote

Naona kampeni za kumchafua Dangote zimeanza kwa kasi.!
Hawatofanikiwa kabisa, mwisho wa siku tutawauliza bei ya cement ni shs sokoni ? Dangote shs 11500, wao ni shs 15000- 17000, sasa itakuaje tuwapende wao ?
 
Hii issue ya Dangote ni mbawaambia kuna siku ukweli utajulikana na mtu itaaibika vibaya!
 
Dangote labda abadilike ndio tutaweza kufaidi uwepo wake hapa Tanzania, ila kwa jinsi alivyo na ninavyomfahamu..kwa sasa kuondoka kwake ni nafuu kwa Watanzania na Taifa.

Yule bwana hawezi kufanya biashara bila utapeli hata mfanyakazi wake wa chini kabisa anajua. Jamaa anaingia mahali kwa lugha tamu sana na ahadi kibao, lakini si mtu yule.

Wapo wanaosema kuhusu ajira za watanzania walioko pale, ni hivi wafanyakazi wataalamu walioko pale ni wale waliokuwa kwenye viwanda vingine vya cement vilivyokuwa vinawalipa vizuri ila baada ya kusikia tishio la ujio wa likiwanda kubwa ambalo lingepewa gas, exemption ya kodi n.k likapunguza bei ya cement viwanda hivyo vingekufa kwa kushindwa kujiendesha,

Hatua mojawapo zilizochukuliwa na viwanda bora kama vile Twiga na vingine ni kupunguza wafanyakazi kwa kiasi kikubwa ambao wengi walienda Dangote kulipwa ujira mdogo sana maana yeye Dangote anatumia management ya Wahindi.

Kule Nigeria alianza biashara zake kwa style ya kuwahonga viongozi wakuu na wakampa excemption ya kodi, matumizi ya barabara hovyo na vitu vingine akashusha bei ya Cement, viwanda vingine vikafa akabaki yeye mwenyewe akishikilia kama 90% ya soko la cement na Lafarge kama chini ya 10% vingine vilikufa baada ya kuhakikisha kwamba ameviua akapandisha bei ikarudi kama zamani.

Hivyo ndivyo alitaka kufanya Tanzania, JK alimpa maeneo makubwa sana, mpaka na eneo la kujenga bandari yake binafsi, jambo ambalo kwa maoni yangu naona ilikuwa hatari hata kwa usalama wa nchi.

Eneo lililojengwa kiwanda na mining lilikuwa la vijiji vitano, ni eneo kubwa ambalo lilikuwa mali ya wananchi, Dangote kwa kushirikiana na viongozi wa serikali ya awamu ya nne waliwatapeli wale wazee kwa kuwapa vitu vidogo vidogo na ziara ya kwenda kuhiji kwa wazee wachache pamoja na laki tano tano na ahadi kibao wakabariki kuiacha ile ardhi na wale wazee wakatumika kuwashawishi wengine wakaingia kingi.

Mara kadhaa nilikuwa nikiwaona hawa wazee wanaojiita wenyeviti wa vijiji vile wakiambaa ambaa pale nje ya kiwanda cha Dangote wakitapeli watu kwa ahadi ya kuwaunganishia vibarua kiwandani wakati hata wao hawana ruhusa ya kuingia ndani ya kiwanda, wazee wamepigika wanajuta tu kimoyo moyo.

Niliwahi kujaribu kuongea na mmoja wao ambaye alikuwa mwenyekiti wa wenyeviti wakati huo nikiwa kiongozi wa chama cha wafanyakazi hapo Kiwandani, nilipomuuliza sababu ya wao wazee kugawa ardhi bure kwa Dangote aliniambia kwamba wao waliamini Dangote si mfanyabiashara ni Alhaji kwa hiyo walitoa ardhi kwa Alhaji ili ajenge kiwanda kiwasaidie watu..

Nilishangaa sana, lakini kilichonifurahisha ni kwamba wanajuta maana zaidi ya laki tano na ziara ya Mecca hawajafaidika tena kwa namna walivyotarajia.
Mtindo wa ufanyaji kazi wa Dangote ni wa kitapeli tapeli tu, anatapeliwa kuanzia mfanyakazi wake wa chini mpaka Rais na mawaziri wakiingia kingi wanatapeliwa.

Kule Nigeria, ana kiwanda kikubwa Four kiln lines kwenye state ya Obajana na kingine Ibese, wafanyakazi zaidi ya 60% ni wahindi, wanaishi vizuri kila kitu wanachotumia ni tofauti na weusi, magari, nyumba za kuishi n.k ni tofauti kabisa.

Wahindi wanaletwa wakiwa hawajui kitu kabisa wanafundishwa na weusi (wanigeria) halafu wakishajua wanawasimamia weusi, wanawanyanyasa sana waafrika, pale ndipo nilipojua kwamba Tanzania ni nchi nzuri sana na siku zote nawambia ukitaka kujua uzuri wa nchi yetu Tanzania nenda Nigeria. Hususanu kufanye kazi kwa Dangote.

Wakati Dangote anafungua kiwanda Tanzania, alikuwa anaahidi kuajiri watanzania lakini ukweli ni kwamba alikuwa ameandaa makontena ya wahindi kuja Tanzania kama ilivyo Nigeria, thanks to God Magufuli akaingia Madarakani.

Wale wahindi wachache waliokuwepo walichukia sana wakaanza hata kukuza mambo au kutunga uongo wakiilaumu Serikali ati kwa kuweka vikwazo vingi, wakati mwingine wanamdanganya Dangote kuhusu Serikali yetu na Watanzania ili wao wapate faida. Ninao ushahidi wa mambo baadhi ambayo kwa makusudi kabisa management ya kihindi ilikuwa ikimdanganya Dangote kwa faida yao.

Mojawapo ilikuwa ni ubora wa makaa ya Mawe ya Tanzania, tulikuwa na vijana wetu maabara pale, hata mimi niliposikia kwamba makaa yetu ya mawe yana quality ya chini niliumia sana niliwauliza wahandisi wetu waliokuwa maabara wakasema ni uongo.

Hiyo ilikuwa mbinu ya wahindi kufanya biashara na makampuni ya South Afrika kwa faida yao huku wakichafua bidhaa zetu.

Lingekuwa jambo la ajabu sana kama serikali ingekubali uhuni huo, nawapongeza sana Mawaziri hawa wa awamu ya tano kwa kutumia elimu yao vizuri kuchunguza hilo kwa sababu hata enzi zile tulikuwa tuwaeleza serikali kila tunapopata nafasi lakini enzi ya awamu ya nne ilikuwa enzi ya aina yake. tulionekana wapuuzi au maskini wanoko.

Watanzania tunapopinga au kutetea ni vema tukatafuta ukweli kwanza, Dangote industries ukiisikia kwenye vyombo vya habari utaona ni mkombozi kwa watanzania, lakini kwa namna ilivyo na inavyotaka ifanyiwe ni hatari sana kwa taifa.

Tumshukuru sana Rais na serikali kwa msimamo wake. Dangote hana tofauti na akina Carl peters wa zamani labda abadilike.........

Itaendelea wiki ijayo

Kuna wakati nawaza kama inawezekana hiki kiwanda kinunuliwe na watz
 
Dangote labda abadilike ndio tutaweza kufaidi uwepo wake hapa Tanzania, ila kwa jinsi alivyo na ninavyomfahamu..kwa sasa kuondoka kwake ni nafuu kwa Watanzania na Taifa.

Yule bwana hawezi kufanya biashara bila utapeli hata mfanyakazi wake wa chini kabisa anajua. Jamaa anaingia mahali kwa lugha tamu sana na ahadi kibao, lakini si mtu yule.

Wapo wanaosema kuhusu ajira za watanzania walioko pale, ni hivi wafanyakazi wataalamu walioko pale ni wale waliokuwa kwenye viwanda vingine vya cement vilivyokuwa vinawalipa vizuri ila baada ya kusikia tishio la ujio wa likiwanda kubwa ambalo lingepewa gas, exemption ya kodi n.k likapunguza bei ya cement viwanda hivyo vingekufa kwa kushindwa kujiendesha,

Hatua mojawapo zilizochukuliwa na viwanda bora kama vile Twiga na vingine ni kupunguza wafanyakazi kwa kiasi kikubwa ambao wengi walienda Dangote kulipwa ujira mdogo sana maana yeye Dangote anatumia management ya Wahindi.

Kule Nigeria alianza biashara zake kwa style ya kuwahonga viongozi wakuu na wakampa excemption ya kodi, matumizi ya barabara hovyo na vitu vingine akashusha bei ya Cement, viwanda vingine vikafa akabaki yeye mwenyewe akishikilia kama 90% ya soko la cement na Lafarge kama chini ya 10% vingine vilikufa baada ya kuhakikisha kwamba ameviua akapandisha bei ikarudi kama zamani.

Hivyo ndivyo alitaka kufanya Tanzania, JK alimpa maeneo makubwa sana, mpaka na eneo la kujenga bandari yake binafsi, jambo ambalo kwa maoni yangu naona ilikuwa hatari hata kwa usalama wa nchi.

Eneo lililojengwa kiwanda na mining lilikuwa la vijiji vitano, ni eneo kubwa ambalo lilikuwa mali ya wananchi, Dangote kwa kushirikiana na viongozi wa serikali ya awamu ya nne waliwatapeli wale wazee kwa kuwapa vitu vidogo vidogo na ziara ya kwenda kuhiji kwa wazee wachache pamoja na laki tano tano na ahadi kibao wakabariki kuiacha ile ardhi na wale wazee wakatumika kuwashawishi wengine wakaingia kingi.

Mara kadhaa nilikuwa nikiwaona hawa wazee wanaojiita wenyeviti wa vijiji vile wakiambaa ambaa pale nje ya kiwanda cha Dangote wakitapeli watu kwa ahadi ya kuwaunganishia vibarua kiwandani wakati hata wao hawana ruhusa ya kuingia ndani ya kiwanda, wazee wamepigika wanajuta tu kimoyo moyo.

Niliwahi kujaribu kuongea na mmoja wao ambaye alikuwa mwenyekiti wa wenyeviti wakati huo nikiwa kiongozi wa chama cha wafanyakazi hapo Kiwandani, nilipomuuliza sababu ya wao wazee kugawa ardhi bure kwa Dangote aliniambia kwamba wao waliamini Dangote si mfanyabiashara ni Alhaji kwa hiyo walitoa ardhi kwa Alhaji ili ajenge kiwanda kiwasaidie watu..

Nilishangaa sana, lakini kilichonifurahisha ni kwamba wanajuta maana zaidi ya laki tano na ziara ya Mecca hawajafaidika tena kwa namna walivyotarajia.
Mtindo wa ufanyaji kazi wa Dangote ni wa kitapeli tapeli tu, anatapeliwa kuanzia mfanyakazi wake wa chini mpaka Rais na mawaziri wakiingia kingi wanatapeliwa.

Kule Nigeria, ana kiwanda kikubwa Four kiln lines kwenye state ya Obajana na kingine Ibese, wafanyakazi zaidi ya 60% ni wahindi, wanaishi vizuri kila kitu wanachotumia ni tofauti na weusi, magari, nyumba za kuishi n.k ni tofauti kabisa.

Wahindi wanaletwa wakiwa hawajui kitu kabisa wanafundishwa na weusi (wanigeria) halafu wakishajua wanawasimamia weusi, wanawanyanyasa sana waafrika, pale ndipo nilipojua kwamba Tanzania ni nchi nzuri sana na siku zote nawambia ukitaka kujua uzuri wa nchi yetu Tanzania nenda Nigeria. Hususanu kufanye kazi kwa Dangote.

Wakati Dangote anafungua kiwanda Tanzania, alikuwa anaahidi kuajiri watanzania lakini ukweli ni kwamba alikuwa ameandaa makontena ya wahindi kuja Tanzania kama ilivyo Nigeria, thanks to God Magufuli akaingia Madarakani.

Wale wahindi wachache waliokuwepo walichukia sana wakaanza hata kukuza mambo au kutunga uongo wakiilaumu Serikali ati kwa kuweka vikwazo vingi, wakati mwingine wanamdanganya Dangote kuhusu Serikali yetu na Watanzania ili wao wapate faida. Ninao ushahidi wa mambo baadhi ambayo kwa makusudi kabisa management ya kihindi ilikuwa ikimdanganya Dangote kwa faida yao.

Mojawapo ilikuwa ni ubora wa makaa ya Mawe ya Tanzania, tulikuwa na vijana wetu maabara pale, hata mimi niliposikia kwamba makaa yetu ya mawe yana quality ya chini niliumia sana niliwauliza wahandisi wetu waliokuwa maabara wakasema ni uongo.

Hiyo ilikuwa mbinu ya wahindi kufanya biashara na makampuni ya South Afrika kwa faida yao huku wakichafua bidhaa zetu.

Lingekuwa jambo la ajabu sana kama serikali ingekubali uhuni huo, nawapongeza sana Mawaziri hawa wa awamu ya tano kwa kutumia elimu yao vizuri kuchunguza hilo kwa sababu hata enzi zile tulikuwa tuwaeleza serikali kila tunapopata nafasi lakini enzi ya awamu ya nne ilikuwa enzi ya aina yake. tulionekana wapuuzi au maskini wanoko.

Watanzania tunapopinga au kutetea ni vema tukatafuta ukweli kwanza, Dangote industries ukiisikia kwenye vyombo vya habari utaona ni mkombozi kwa watanzania, lakini kwa namna ilivyo na inavyotaka ifanyiwe ni hatari sana kwa taifa.

Tumshukuru sana Rais na serikali kwa msimamo wake. Dangote hana tofauti na akina Carl peters wa zamani labda abadilike.........

Itaendelea wiki ijayo
nyie maccm ndo mmeleta shida yote hii si mwachie dola waje wengine, nnagangania kwa nini??? alafu bila aibu mnajifanya wazalendo, leo ndo mmegundua ubaya wa dangote je mikataba mingine ya kipuuzi mliyosaini huko nyuma, mtaisitisha???
 
Namkumbusha Rais Tu Kule Kanda Ya Ziwa Pongezi Ni Nyingi Sana Namna Ulivyorudisha Wapiga Kura Wako
Kwenye Maeneo Yao Ya Kazi Na Wako Imara

Ila Wanasema Bado Hawajapewa "Magwangala" Hadi Leo Hivi Yule Mwekezaji Naye Afutiwe Hati Yake Tu
 
Ulikuwa wapi muda wote kueleza haya?Yaani baada ya msosi kuingia mchanga ndio unasema ooh ulikuwa na chumvi nyingi!
 
makubwa haya aseeee, kama hii ya kwako ni sawa basi naamini mzee wangu magufuli atakuita ikulu ukamuelezee kwa undani zaidi
 
Ujinga wa hawa maccm yanadhani dangote anatuhitaj sisi wakat sisi ndo tunamhtaj dongote kupitiliza
Kama hatuhitaji sisi kwa alileta kiwanda huku? Akajenge baharini au angani then auze hiyo cement. Dangote ni mjanjamjanja tu. Kila nchi ina taratibu na sheria zake. Kama anaona ameonewa bora awahi mahakamani na sio kulia lia kwenye media. Hapa kazi tu. Binafsi kwa mambo ambayo amewafanyia watanzania hasa waliokuwa wanampelekea mawe kutoka pale Kilwa (Kiranjeranje) na kuwalazimisha awape cement badala ya kuwalipa hela na jamaa wamefilisika sasa. Sina hamu nae. Acha aisome namba tu. Hata Bill Gates anafata sheria itakuwa Dangote?
 
Dangote labda abadilike ndio tutaweza kufaidi uwepo wake hapa Tanzania, ila kwa jinsi alivyo na ninavyomfahamu..kwa sasa kuondoka kwake ni nafuu kwa Watanzania na Taifa.

Yule bwana hawezi kufanya biashara bila utapeli hata mfanyakazi wake wa chini kabisa anajua. Jamaa anaingia mahali kwa lugha tamu sana na ahadi kibao, lakini si mtu yule.

Wapo wanaosema kuhusu ajira za watanzania walioko pale, ni hivi wafanyakazi wataalamu walioko pale ni wale waliokuwa kwenye viwanda vingine vya cement vilivyokuwa vinawalipa vizuri ila baada ya kusikia tishio la ujio wa likiwanda kubwa ambalo lingepewa gas, exemption ya kodi n.k likapunguza bei ya cement viwanda hivyo vingekufa kwa kushindwa kujiendesha,

Hatua mojawapo zilizochukuliwa na viwanda bora kama vile Twiga na vingine ni kupunguza wafanyakazi kwa kiasi kikubwa ambao wengi walienda Dangote kulipwa ujira mdogo sana maana yeye Dangote anatumia management ya Wahindi.

Kule Nigeria alianza biashara zake kwa style ya kuwahonga viongozi wakuu na wakampa excemption ya kodi, matumizi ya barabara hovyo na vitu vingine akashusha bei ya Cement, viwanda vingine vikafa akabaki yeye mwenyewe akishikilia kama 90% ya soko la cement na Lafarge kama chini ya 10% vingine vilikufa baada ya kuhakikisha kwamba ameviua akapandisha bei ikarudi kama zamani.

Hivyo ndivyo alitaka kufanya Tanzania, JK alimpa maeneo makubwa sana, mpaka na eneo la kujenga bandari yake binafsi, jambo ambalo kwa maoni yangu naona ilikuwa hatari hata kwa usalama wa nchi.

Eneo lililojengwa kiwanda na mining lilikuwa la vijiji vitano, ni eneo kubwa ambalo lilikuwa mali ya wananchi, Dangote kwa kushirikiana na viongozi wa serikali ya awamu ya nne waliwatapeli wale wazee kwa kuwapa vitu vidogo vidogo na ziara ya kwenda kuhiji kwa wazee wachache pamoja na laki tano tano na ahadi kibao wakabariki kuiacha ile ardhi na wale wazee wakatumika kuwashawishi wengine wakaingia kingi.

Mara kadhaa nilikuwa nikiwaona hawa wazee wanaojiita wenyeviti wa vijiji vile wakiambaa ambaa pale nje ya kiwanda cha Dangote wakitapeli watu kwa ahadi ya kuwaunganishia vibarua kiwandani wakati hata wao hawana ruhusa ya kuingia ndani ya kiwanda, wazee wamepigika wanajuta tu kimoyo moyo.

Niliwahi kujaribu kuongea na mmoja wao ambaye alikuwa mwenyekiti wa wenyeviti wakati huo nikiwa kiongozi wa chama cha wafanyakazi hapo Kiwandani, nilipomuuliza sababu ya wao wazee kugawa ardhi bure kwa Dangote aliniambia kwamba wao waliamini Dangote si mfanyabiashara ni Alhaji kwa hiyo walitoa ardhi kwa Alhaji ili ajenge kiwanda kiwasaidie watu..

Nilishangaa sana, lakini kilichonifurahisha ni kwamba wanajuta maana zaidi ya laki tano na ziara ya Mecca hawajafaidika tena kwa namna walivyotarajia.
Mtindo wa ufanyaji kazi wa Dangote ni wa kitapeli tapeli tu, anatapeliwa kuanzia mfanyakazi wake wa chini mpaka Rais na mawaziri wakiingia kingi wanatapeliwa.

Kule Nigeria, ana kiwanda kikubwa Four kiln lines kwenye state ya Obajana na kingine Ibese, wafanyakazi zaidi ya 60% ni wahindi, wanaishi vizuri kila kitu wanachotumia ni tofauti na weusi, magari, nyumba za kuishi n.k ni tofauti kabisa.

Wahindi wanaletwa wakiwa hawajui kitu kabisa wanafundishwa na weusi (wanigeria) halafu wakishajua wanawasimamia weusi, wanawanyanyasa sana waafrika, pale ndipo nilipojua kwamba Tanzania ni nchi nzuri sana na siku zote nawambia ukitaka kujua uzuri wa nchi yetu Tanzania nenda Nigeria. Hususanu kufanye kazi kwa Dangote.

Wakati Dangote anafungua kiwanda Tanzania, alikuwa anaahidi kuajiri watanzania lakini ukweli ni kwamba alikuwa ameandaa makontena ya wahindi kuja Tanzania kama ilivyo Nigeria, thanks to God Magufuli akaingia Madarakani.

Wale wahindi wachache waliokuwepo walichukia sana wakaanza hata kukuza mambo au kutunga uongo wakiilaumu Serikali ati kwa kuweka vikwazo vingi, wakati mwingine wanamdanganya Dangote kuhusu Serikali yetu na Watanzania ili wao wapate faida. Ninao ushahidi wa mambo baadhi ambayo kwa makusudi kabisa management ya kihindi ilikuwa ikimdanganya Dangote kwa faida yao.

Mojawapo ilikuwa ni ubora wa makaa ya Mawe ya Tanzania, tulikuwa na vijana wetu maabara pale, hata mimi niliposikia kwamba makaa yetu ya mawe yana quality ya chini niliumia sana niliwauliza wahandisi wetu waliokuwa maabara wakasema ni uongo.

Hiyo ilikuwa mbinu ya wahindi kufanya biashara na makampuni ya South Afrika kwa faida yao huku wakichafua bidhaa zetu.

Lingekuwa jambo la ajabu sana kama serikali ingekubali uhuni huo, nawapongeza sana Mawaziri hawa wa awamu ya tano kwa kutumia elimu yao vizuri kuchunguza hilo kwa sababu hata enzi zile tulikuwa tuwaeleza serikali kila tunapopata nafasi lakini enzi ya awamu ya nne ilikuwa enzi ya aina yake. tulionekana wapuuzi au maskini wanoko.

Watanzania tunapopinga au kutetea ni vema tukatafuta ukweli kwanza, Dangote industries ukiisikia kwenye vyombo vya habari utaona ni mkombozi kwa watanzania, lakini kwa namna ilivyo na inavyotaka ifanyiwe ni hatari sana kwa taifa.

Tumshukuru sana Rais na serikali kwa msimamo wake. Dangote hana tofauti na akina Carl peters wa zamani labda abadilike.........

Itaendelea wiki ijayo
Asante umemaliza hadithi yako.
sasa!
tunataka utushushie bei ya sementi ilee ya elf 11. Bei ya
Tajiri yako Dangote.
Mana mnamzingua.. amefunga kiwanda sementi sasa imeruka elf 15.
 
Kuja kwa viwanda vya wageni Tanzania ni neema pia kwa bidhaa za ndani na ajira kwa ujumla, nitashangaa sana kama dangote ataajiri zaidi ya watu 50 wahindi akaacha watanzania na serikali ipo, pia nitashangaa sana kama baadhi ya materials kama makaa ya mawe nayo yaagizwe kutoka nje ya nchi nawakati yanapatikana Tz, kuhusu gesi anunue sio kwa kupewa bure, maana in returns sisi tutanunua bidhaa zake iweje tumbembeleze wakati huo kiwanda kimeshajengwa nchini? hataki basi afunge, mfanyabiashara yeyote anae fanya kazi kwa karibu na wahindi unatakiwa kumuangalia very close,maana wahindi ni corrupted people in the world, hivyo dangote pia lazima tukae nae chonjo tukizubaa atashangaza.
Plus mkopo wa TIB....YAANI KIULAINI KABISA . ...
 
Walioingia naye mikataba ni ccm ....

Wanaovunja mkataba ni Ccm.....

Waliompokea ni Ccm......

Wanaotaka aondoke ni Ccm.....

Tafakari chukua hatua.........
Imepanda bei mpaka elfu 15 toka elfu 11
 
Hii ni kweli, Dangote huviua Viwanda vya nchi husika kwa kushusha bei kisha upandisha bei.
Halafu tujiulize kama angepewa gas bure au kwa bei ya chini je, Viwanda vingine vingene navyo vingepewa?
Mbona baresa hamumsemi...
Boti zooote pale feri zinazopiga kazi ni yeye peke yake kajenga mpaka gati yake. Zile boti za kampuni nyingine zipo hoi zimepaki.
 
Ujinga wa hawa maccm yanadhani dangote anatuhitaj sisi wakat sisi ndo tunamhtaj dongote kupitiliza
Wewe ndio mjinga kujifanya unajua kumbe nyumbu tu. Ebu tufafanulie hoja yako tukuelewe.

Kama anataka tax exemption, cheap prices on gas and coal supply ili apunguze bei, hata viwanda viwanda vingine vinaweza. Umesikia nyumbu!?
 
Daah, sasa hv nadhan hta mke akikuzingua inabidi uilaumu serikali ya awamu ya 4. Inasemwa vby na kila mtu aisee...!!

Sifahamu ukweli ni upi katika hili, ila wewe ni MNAFIKI kwa kuendelea kuwepo kwa Dangote wkt unajua sio watu wazuri. Wakati mlipokuwa mnapinga, ungeonesha uzalendo wa hali ya juu kma ungeacha kazi ili usiwe part ya udhalimu huo.

Kama Magufuli asingewakazia Dangote, TUNGEYAJUA YOTE HAYA...??? Au unatueleza ubaya wake huu kwa kuwa tayar uwezekano wa kazi kuwepo ni mdogo?? Mbn yote haya hayakujulikana kabla..??

Ulikuwa unawaeleza serikali. Nani ulimwambia..?? Au ulikuw unadiscuss na mkeo ambaye ni serikali ya nyumban kwako..? Unataka kutuaminisha kwmb serikali ya awamu ya 4 ilikuwa na wajinga wengi kiasi cha kutokukusikiliza hta kma ni kwa maslahi ya taifa..??

Nway, siku zote maskin huwa tunawaona matajiri ni watu wabaya sn. Na ukweli ni kwamba bila kuwa na kaukatili fulani ni ngumu sn kuwa tajiri.
Alikuwa anadiscuss na mume wake.
 
Dangote labda abadilike ndio tutaweza kufaidi uwepo wake hapa Tanzania, ila kwa jinsi alivyo na ninavyomfahamu..kwa sasa kuondoka kwake ni nafuu kwa Watanzania na Taifa.

Yule bwana hawezi kufanya biashara bila utapeli hata mfanyakazi wake wa chini kabisa anajua. Jamaa anaingia mahali kwa lugha tamu sana na ahadi kibao, lakini si mtu yule.

Wapo wanaosema kuhusu ajira za watanzania walioko pale, ni hivi wafanyakazi wataalamu walioko pale ni wale waliokuwa kwenye viwanda vingine vya cement vilivyokuwa vinawalipa vizuri ila baada ya kusikia tishio la ujio wa likiwanda kubwa ambalo lingepewa gas, exemption ya kodi n.k likapunguza bei ya cement viwanda hivyo vingekufa kwa kushindwa kujiendesha,

Hatua mojawapo zilizochukuliwa na viwanda bora kama vile Twiga na vingine ni kupunguza wafanyakazi kwa kiasi kikubwa ambao wengi walienda Dangote kulipwa ujira mdogo sana maana yeye Dangote anatumia management ya Wahindi.

Kule Nigeria alianza biashara zake kwa style ya kuwahonga viongozi wakuu na wakampa excemption ya kodi, matumizi ya barabara hovyo na vitu vingine akashusha bei ya Cement, viwanda vingine vikafa akabaki yeye mwenyewe akishikilia kama 90% ya soko la cement na Lafarge kama chini ya 10% vingine vilikufa baada ya kuhakikisha kwamba ameviua akapandisha bei ikarudi kama zamani.

Hivyo ndivyo alitaka kufanya Tanzania, JK alimpa maeneo makubwa sana, mpaka na eneo la kujenga bandari yake binafsi, jambo ambalo kwa maoni yangu naona ilikuwa hatari hata kwa usalama wa nchi.

Eneo lililojengwa kiwanda na mining lilikuwa la vijiji vitano, ni eneo kubwa ambalo lilikuwa mali ya wananchi, Dangote kwa kushirikiana na viongozi wa serikali ya awamu ya nne waliwatapeli wale wazee kwa kuwapa vitu vidogo vidogo na ziara ya kwenda kuhiji kwa wazee wachache pamoja na laki tano tano na ahadi kibao wakabariki kuiacha ile ardhi na wale wazee wakatumika kuwashawishi wengine wakaingia kingi.

Mara kadhaa nilikuwa nikiwaona hawa wazee wanaojiita wenyeviti wa vijiji vile wakiambaa ambaa pale nje ya kiwanda cha Dangote wakitapeli watu kwa ahadi ya kuwaunganishia vibarua kiwandani wakati hata wao hawana ruhusa ya kuingia ndani ya kiwanda, wazee wamepigika wanajuta tu kimoyo moyo.

Niliwahi kujaribu kuongea na mmoja wao ambaye alikuwa mwenyekiti wa wenyeviti wakati huo nikiwa kiongozi wa chama cha wafanyakazi hapo Kiwandani, nilipomuuliza sababu ya wao wazee kugawa ardhi bure kwa Dangote aliniambia kwamba wao waliamini Dangote si mfanyabiashara ni Alhaji kwa hiyo walitoa ardhi kwa Alhaji ili ajenge kiwanda kiwasaidie watu..

Nilishangaa sana, lakini kilichonifurahisha ni kwamba wanajuta maana zaidi ya laki tano na ziara ya Mecca hawajafaidika tena kwa namna walivyotarajia.
Mtindo wa ufanyaji kazi wa Dangote ni wa kitapeli tapeli tu, anatapeliwa kuanzia mfanyakazi wake wa chini mpaka Rais na mawaziri wakiingia kingi wanatapeliwa.

Kule Nigeria, ana kiwanda kikubwa Four kiln lines kwenye state ya Obajana na kingine Ibese, wafanyakazi zaidi ya 60% ni wahindi, wanaishi vizuri kila kitu wanachotumia ni tofauti na weusi, magari, nyumba za kuishi n.k ni tofauti kabisa.

Wahindi wanaletwa wakiwa hawajui kitu kabisa wanafundishwa na weusi (wanigeria) halafu wakishajua wanawasimamia weusi, wanawanyanyasa sana waafrika, pale ndipo nilipojua kwamba Tanzania ni nchi nzuri sana na siku zote nawambia ukitaka kujua uzuri wa nchi yetu Tanzania nenda Nigeria. Hususanu kufanye kazi kwa Dangote.

Wakati Dangote anafungua kiwanda Tanzania, alikuwa anaahidi kuajiri watanzania lakini ukweli ni kwamba alikuwa ameandaa makontena ya wahindi kuja Tanzania kama ilivyo Nigeria, thanks to God Magufuli akaingia Madarakani.

Wale wahindi wachache waliokuwepo walichukia sana wakaanza hata kukuza mambo au kutunga uongo wakiilaumu Serikali ati kwa kuweka vikwazo vingi, wakati mwingine wanamdanganya Dangote kuhusu Serikali yetu na Watanzania ili wao wapate faida. Ninao ushahidi wa mambo baadhi ambayo kwa makusudi kabisa management ya kihindi ilikuwa ikimdanganya Dangote kwa faida yao.

Mojawapo ilikuwa ni ubora wa makaa ya Mawe ya Tanzania, tulikuwa na vijana wetu maabara pale, hata mimi niliposikia kwamba makaa yetu ya mawe yana quality ya chini niliumia sana niliwauliza wahandisi wetu waliokuwa maabara wakasema ni uongo.

Hiyo ilikuwa mbinu ya wahindi kufanya biashara na makampuni ya South Afrika kwa faida yao huku wakichafua bidhaa zetu.

Lingekuwa jambo la ajabu sana kama serikali ingekubali uhuni huo, nawapongeza sana Mawaziri hawa wa awamu ya tano kwa kutumia elimu yao vizuri kuchunguza hilo kwa sababu hata enzi zile tulikuwa tuwaeleza serikali kila tunapopata nafasi lakini enzi ya awamu ya nne ilikuwa enzi ya aina yake. tulionekana wapuuzi au maskini wanoko.

Watanzania tunapopinga au kutetea ni vema tukatafuta ukweli kwanza, Dangote industries ukiisikia kwenye vyombo vya habari utaona ni mkombozi kwa watanzania, lakini kwa namna ilivyo na inavyotaka ifanyiwe ni hatari sana kwa taifa.

Tumshukuru sana Rais na serikali kwa msimamo wake. Dangote hana tofauti na akina Carl peters wa zamani labda abadilike.........

Itaendelea wiki ijayo
aisee' mkuu ungekua karibu ningekupa mkono kwa jinsi ulivyoelezea juu ya hizi management za kihindi kuna kampuni pia ya ESTIM construction tena inajiita still ya mzawa wanaletana wenyewe kwa wenyewe kutoka India na wanalipana mishahara mikubwa ya kuanzia USD $700 tena wanaingiziwa moja kwa moja kwenye akaunti zao za India naona ni kama mbinu ya kukwepa Kodi kwenye mishahara yao kwa huku Tanzania na bado huku Snapdeal posho ya zaidi ya t' sh 50'000/= kwa Kila mwisho wa wiki analaana bure amekupata bure na wanakunywa maziwa mara mbili kwa siku kwa sababu ya afya zao huku mtanzania mweusi anayetimkiwa na vumbi kwa ajili ya shughuli za ujenzi tena ni fundi ambae anamzidi hata kiwango cha ujuzi wa kazi huyo muhindi unakuta anaambuliaa sh elfu 9 au 10 jioni na wamejazana kibao' unaumwa sana aisee' sasa nashindwa hata kuelewa uzalendo wa kampuni ya kitanzania mtu mweusi ambae ni mzalendo kulipwa alipwe sh elfu 9 na ambae sio sio mzalendo alipwe zaidi ya USD$ 700na kuendelea tena wahusika wajaribu kuchunguza hili swala' ahsante
 
Huyu jamaa kaja na povu la wahindi. Usha jiuliza kwanini aliwapa wahindi wasimamie wakati wa erection na commissioning?. Ni watanzania wangapi wenye uwezo wa kusimamia project kubwa ya cement na wasiibe. Kuna thread humu ya dangote akilalamika wizi mkubwa unao fanywa na wazawa wenzutu huko mtwara. Mbali na hiyo hao wahindi hawahusiki ata kidogo kwenye kuensesha kiwanda. Kiwanda kinaendeshwa na wachina " sinoma" ambao wako kwenye guarantee period na baada ya miaka miwili watafanya hand over kwa wazawa. Na hao wahindi unao wasema walio kwenye mgt ni mageneral managers walio kuwa wanasimamia project. Na na soon baada ya project kuisha na ku hand over wanasepa zao. Swala la coal; akati Dangote inaingia kwenye operation bara bara ya mtwara- mbinga ilikuwa bado inashida kubwa hivo transport cost per ton of material ilikuwa kubwa ukilinganisha na ku import. Hali hii ilisababisha kiasi cha makaa ya mawe kuagizwa toka nje ya nchi ambapo soon bara bara itakapo isha inasemekana kuna lory 600 zinakuja kwa ajili ya kubeba raw material pamoja na cement.


Swala la kuua viwanda pengine hauja elewa kinacho fanyika. Kwanza dangote anajenga viwanda kwa gharama ndoko akiwatumia wachina ambao wako kama cheap labor hivo kufanya return on investment kuwa kubwa na kufanya payback period kuwa ndogo huku akiwa na most competitive technology. Swala ambalo viwanda vingi vya Tanzania havina. Inasemkena kila kitu ni automated kiasi kwamba hata idadi ya man power I apungua hivo wachache wenye uelewa mkubwa ndio wanao patiwa nafasi . Hayo ndio minayo yajua kihusu dangote hayo mengine ndo nimesikia kwako ngojea niyafanyie utafiti
 
Back
Top Bottom