Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,216
- 859,606
Ndio hivyo tena, tumeikosa.
Dangote ameiambia BBC, ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta katika mji wa Lamu nchini Kenya utaanza Oktoba 2026. Ujenzi utagharimu Dola za Kimarekani bilioni 15.5 badala ya bilioni 20 zilizotajwa awali. Upungufu wa gharama umetokana na uzoefu wa kujenga kiwanda kama hicho kule nchini Nigeria.
Sakata hili la 'Dangote refinery' katika ukanda wa Afrika Mashariki limeonesha matobo yaliyopo katika 'System' za utawala wa Tanzani, hasa katika idara za Usalama, madawati yanayoshughulikia siasa za kikanda, mipango mikakati na usalama wa kiuchumi (economic security) na maendeleo ya taifa kwa ujumla. TUMEZINGUA.
Baada ya Kampuni ya Dangote kutangaza ujenzi wa refinery huko Lamu, tumeshuhudia 'jitihada za zima moto' za kumshawishi Dangote abadili mawazo;
Kwanza tumeona Dangote akialikwa Ikulu ya Dar es Salaam na kupewa eneo Bagamoyo kwa ajili ya uwekezaji.
Pili tumeona tukio la kusaini hati ya Makubaliano (MoU) kati ya Tanzania na Uganda kuufanya mji wa Tanga kuwa kituo kikuu cha Nishati.
Tatu, wakati tukio hilo likiendelea Waziri wa Sera Mipamgo na Uwekezaji alikuwa Nigeria kukutana na Dangote. (Pengine kumshawishi abadili mawazo). Tuliona Waziri akibena zawadi ya 'kumtongoza' bilionea Dangote. Mbinu za kale!
Hayo mambo matatu yalitakiwa kufanyika punde tu Rais Ruto alipotangaza ujenzi wa refinery hiyo mjini Tanga. Lakini badala yake, watu wasio na uwezo waliopo madarakani, sio tu hawakujua lakufanya bali walifanya 'blunder' la kumzodoa Ruto kwa kauli zake. Ni 'Blunder' la mwaka.
Ruto aliitangaza Tanga kana kwamba ni utashi wa pamoja wa mataifa ya Afrika Mashariki yaliokwisha amua! Isingekuwa Rais kwa Kampuni ya Damgote kufikiria tofauti na maamuzi ya mataufa 6.
Baada ya kauli ya Ruto, ndipo tukio la kuitangaza Tanga kama Energy Hub lilipaswa kufanyika na zaidi kwenye bajeti ya mwaka 2026/27 liwepo. Hili lingehusisha Tanzania, Kenya, Rwanda, DRC, Uganda na wengine badala ya Tanzania na Uganda pekee. Ukisoma bajeti ya Wizara ya Nishati, hakuna mpamgo wa hiyo Energy Hub kwa Tanga, badala yake kuna mpango wa Energy Hub wa Dar es Salaam. Maana yake huo mpango ni mpya kabisa, na pengine lengo ni kumshawishi Dangote, lakini ni 'Too late'.
Jambo lingine ambalo lilipswa kufanyika ni Serikali ya Tanzania kutangaza kutenga kiasi cha fedha kwa ajili ya mradi huo wa refinery mjini Tanga.
Mbali na hapo, tungeweza kupenyeza ajenda hiyo kwenye vyombo vya habari vya kikanda na kimataifa.
Lengo la yote hayo ni kuinyima Kampuni ya Dangote muda wa kufikiria nje ya Tanga.
Lakini wapi?
Badala ya kuketi na kuumiza vichwa namna ya kutumia fursa, tukaruhusu akili za taarab zifanye kazi. Akili za Kuzodoa, kusuta na lugha za mafumbo zikachukua nafasi ya Akili ya kupanga mikakati ya kiuchumi kwenye mazingira ya siasa za kijiografia.
Aibu kwa wanojiita wanamikakati.
Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo.
Dangote ameiambia BBC, ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta katika mji wa Lamu nchini Kenya utaanza Oktoba 2026. Ujenzi utagharimu Dola za Kimarekani bilioni 15.5 badala ya bilioni 20 zilizotajwa awali. Upungufu wa gharama umetokana na uzoefu wa kujenga kiwanda kama hicho kule nchini Nigeria.
Sakata hili la 'Dangote refinery' katika ukanda wa Afrika Mashariki limeonesha matobo yaliyopo katika 'System' za utawala wa Tanzani, hasa katika idara za Usalama, madawati yanayoshughulikia siasa za kikanda, mipango mikakati na usalama wa kiuchumi (economic security) na maendeleo ya taifa kwa ujumla. TUMEZINGUA.
Baada ya Kampuni ya Dangote kutangaza ujenzi wa refinery huko Lamu, tumeshuhudia 'jitihada za zima moto' za kumshawishi Dangote abadili mawazo;
Kwanza tumeona Dangote akialikwa Ikulu ya Dar es Salaam na kupewa eneo Bagamoyo kwa ajili ya uwekezaji.
Pili tumeona tukio la kusaini hati ya Makubaliano (MoU) kati ya Tanzania na Uganda kuufanya mji wa Tanga kuwa kituo kikuu cha Nishati.
Tatu, wakati tukio hilo likiendelea Waziri wa Sera Mipamgo na Uwekezaji alikuwa Nigeria kukutana na Dangote. (Pengine kumshawishi abadili mawazo). Tuliona Waziri akibena zawadi ya 'kumtongoza' bilionea Dangote. Mbinu za kale!
Hayo mambo matatu yalitakiwa kufanyika punde tu Rais Ruto alipotangaza ujenzi wa refinery hiyo mjini Tanga. Lakini badala yake, watu wasio na uwezo waliopo madarakani, sio tu hawakujua lakufanya bali walifanya 'blunder' la kumzodoa Ruto kwa kauli zake. Ni 'Blunder' la mwaka.
Ruto aliitangaza Tanga kana kwamba ni utashi wa pamoja wa mataifa ya Afrika Mashariki yaliokwisha amua! Isingekuwa Rais kwa Kampuni ya Damgote kufikiria tofauti na maamuzi ya mataufa 6.
Baada ya kauli ya Ruto, ndipo tukio la kuitangaza Tanga kama Energy Hub lilipaswa kufanyika na zaidi kwenye bajeti ya mwaka 2026/27 liwepo. Hili lingehusisha Tanzania, Kenya, Rwanda, DRC, Uganda na wengine badala ya Tanzania na Uganda pekee. Ukisoma bajeti ya Wizara ya Nishati, hakuna mpamgo wa hiyo Energy Hub kwa Tanga, badala yake kuna mpango wa Energy Hub wa Dar es Salaam. Maana yake huo mpango ni mpya kabisa, na pengine lengo ni kumshawishi Dangote, lakini ni 'Too late'.
Jambo lingine ambalo lilipswa kufanyika ni Serikali ya Tanzania kutangaza kutenga kiasi cha fedha kwa ajili ya mradi huo wa refinery mjini Tanga.
Mbali na hapo, tungeweza kupenyeza ajenda hiyo kwenye vyombo vya habari vya kikanda na kimataifa.
Lengo la yote hayo ni kuinyima Kampuni ya Dangote muda wa kufikiria nje ya Tanga.
Lakini wapi?
Badala ya kuketi na kuumiza vichwa namna ya kutumia fursa, tukaruhusu akili za taarab zifanye kazi. Akili za Kuzodoa, kusuta na lugha za mafumbo zikachukua nafasi ya Akili ya kupanga mikakati ya kiuchumi kwenye mazingira ya siasa za kijiografia.
Aibu kwa wanojiita wanamikakati.
Nawasilisha!
Dr. Chris Cyrilo.