EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

EXCLUSIVE Interview with Zitto Zuberi Kabwe at Jamii Forums [Coming Soon]

Status
Not open for further replies.
AshaDii haya maswali Mheshimiwa Zitto atayajibu lini na ktk thread ipi? hii au utafungua nyingine? Ni hayo tu
 
Last edited by a moderator:
Swali
  1. Msimamo wako ni upi kuhusiana na madai ya waislamu? hususani kina Ponda na taasisi za kislamu
  2. Ni upi msimamo wako kuhusiana na madai ya kikundi cha UAMSHO kule znz?
  3. Una msimamo gani kuhusu madai ya malawi juu ya ziwa nyasa
  4. Kama nipo sahihi nishawai kukusikia ukitamka hautagombea nafasi yeyote ndani ya chama chako mwakani (2013) bali ikifika mwaka 2015 utaomba ridhaa kwa chama chako kikusimamishe kugombea Uraisi; swali kwanini mwakani (2013) umeamua kutogombea nafasi yeyote ndani ya chama chako?

Asante sana Mheshimiwa.
 
Swali
  1. Msimamo wako ni upi kuhusiana na madai ya waislamu? ususani kina Ponda na taasisi za kislamu
  2. Ni upi msimamo wako kuhusiana na madai ya kikundi cha UAMSHO kule znz?
  3. Una msimamo gani kuhusu madai ya malawi juu ya ziwa nyasa
  4. Kama nipo sahihi nishawai kukusikia ukitamka hautagombea nafasi yeyote ndani ya chama chako mwakani (2013) bali ikifika mwaka 2015 utaomba ridhaa kwa chama chako kikusimamishe kugombea Uraisi; swali kwanini mwakani (2013) umeamua kutogombea nafasi yeyote ndani ya chama chako?

Asante sana Mheshimiwa.

Swali namba 1 na 2 yanamhusuje Zitto. Acha chokochoko.
 
Swali langu ni Kama ifuatavyo:
Nini kipaumbele chake katika kuhakikisha taifa linasonga mbele kama atakabaziwa madaraka ya kuliongoza taifa? Na je amejiandaa vipi kukabaliana na changamoto ambazo atakumbana nazo pindi atakapo shika taifa Kama kiongozi? Na changamoto kubwa hapa kwetu ni ufisadi uliopitiliza , atahakikisha wanawajibika vipi hao watu. Na je, asipo fanikisha azma yake ya urais, anatalisaidi vipi taifa kutoka na vipaumbele vyake vya kulisaidia taifa lisonge mbele?
 
mimi sio fan sana wa zitto,lakini kuna vitu vichache huwa anasema ningependa kuvijua...
  • kwenye ajali iliyomuua mama Mbatia,ulikua wa kwanza kufika,je ni kweli ulihisi ilikua planned kwa ajili yako?
  • Je ni kweli una vyanzo vingi ndani ya System(TISS)
 
Mheshimiwa Zitto, hongera kwa kukubalika. Maswali yangu ni matatu tuuu1. Ni kiongozi gani unaemkubali zaidi Tanzania? Na unampa nafasi gani ya uongozi mwaka 2015?2. Ni nani anaefaa kuwa raisi wa Tanzania mwaka 2015? Kwa nini? Yaani ana sifa zipi hadi ukadhani ndiye anaefaa?3. Ni siri gani hasa iliyokupa mafanikio wewe? "Kiuchumi zaidi" coz wewe ni tajiri mkubwa bila shaka.
 
CCm wanadai kuwa Chadema hawana figures (watu) wa dhati katika jopo la viongozi au wanachama kuweza kupata nafasi ya uongozi wa nchi hii. sasa Mheshimiwa Zito ana maoni gani kuhusu hili na pia anatathimini vipi hali ya CDM kuelekea uchaguzi wa 2015. ana maoni gani namna CCM walivojipanga hasa kwa kuchagua viongozi wapya na je, hali hii haathiriri uungwaji mkono wa wanachi kwa CDM? wanatupa matumaini gani sisi wapenda mabadiliko?
 
  1. Maswali Yangu,Zito Kabwe ulikuwa mmoja wa wanachama muhimu sana hapa Jamiiforums tena ukitumia jina lako halisi na kuchangia mijadala mbalimbali,Ni muda mrefu sana michango yako haionekani Je nini kimekukimbiza hapa Jamiiforums?



  2. Kumekuwa na shutuma nyingi sana kuhusu wewekutoka miongoni mwa wanachama/mashabiki wa CHADEMA ,wanasema wewe ni mamluki wa CCM je una maoni gani kuhusu hizi shutuma?
 
AshaDii haya maswali Mheshimiwa Zitto atayajibu lini na ktk thread ipi? hii au utafungua nyingine? Ni hayo tu


Godlisten sema tu mambo yaabana ni mengi.. Ukisoma ndani ya hii thread yoote hayo yamelezwa. Hata hivo kwa manufaa na urahisi kwako narudia kuwa siku na mda wa interview itatangazwa - Ila Inshallah itakuwa wiki hii hii. Itakuwa na thread yake ambayo itaurushwa Jukwaa la Great Thinkers na itahusisha tu members wawili (AshaDii na Ziito).

Hata hivyo ili kuwezesha wale members wanaofuatilia kuweza comment yale ambayo wanaona yanaendelea kutakuwa na thread nyingine (side thread) ambayo itatumika kama mahala pa members wote kurusha mabandiko yao.
 
  1. Maswali Yangu,Zito Kabwe ulikuwa mmoja wa wanachama muhimu sana hapa Jamiiforums tena ukitumia jina lako halisi na kuchangia mijadala mbalimbali,Ni muda mrefu sana michango yako haionekani Je nini kimekukimbiza hapa Jamiiforums?

  2. Kumekuwa na shutuma nyingi sana kuhusu wewekutoka miongoni mwa wanachama/mashabiki wa CHADEMA ,wanasema wewe ni mamluki wa CCM je una maoni gani kuhusu hizi shutuma?

Belo niombe samahani kwako na niwe wazi kuwa hilo swali lako la kwanza sitawakilisha... Naweza jibu kwa niaba. Mkuu Zitto yupo hapa Jamiiforums na huwa anatokeza mara moja moja ingawa sio consistently. Mwezi huu tu mmoja karusha threads sio chini ya 5 ambazo utazipata kwa kupitia hii Link... Zitto's Latest Threads.
 
Mheshimiwa zitto naomba kuuliza je kwanin unatka kuwa rais 2015 ?pia kwanin wewe na dr slaa hamna ndoa ila mnataka kuingia ikulu?pia uliwahi kutuhumiwa kuwa na mahusiano ya karibu na usalama wa taifa. vp unasemje juu. ya hilo?
 
@Ashadii ,nakubaliana na wewe nilikuwa sijaona hizo thread zake lakini still ukichunguza utagundua kuwa baada ya kupotea kwa muda mrefu sana alirudi tena mwezi September na sio mwezi huu kama ulivyosema
 
@Ashadii ,nakubaliana na wewe nilikuwa sijaona hizo thread zake lakini still ukichunguza utagundua kuwa baada ya kupotea kwa muda mrefu sana alirudi tena mwezi September na sio mwezi huu kama ulivyosema

Belo hio ilikuwa ni link ya threads alizo post... Ukitaka kujua HASA ushiriki wake inatakiwa uangalie post zake. Ukiangalia hizi post zake kwa mwaka tu huu 2012 utaona kuwa toka mwezi January (na huko nyuma) yupo hapa na pale na karibu kila mwenzi wa mwaka huu kachangia, na mwaka jana pia. Naomba pitia linki hii... Zitto's latest Posts.

Nafanya hili ili walau uelewe ni kwanini sitawakilisha hilo swali... Pamoja saana.
 
@Ashadii ,nakubaliana na wewe nilikuwa sijaona hizo thread zake lakini still ukichunguza utagundua kuwa baada ya kupotea kwa muda mrefu sana alirudi tena mwezi September na sio mwezi huu kama ulivyosema
Kwani ni lazima akija JF kwamba alog in? haiwezekani yeye kuja hapa kama Guest tu kama anaona hana cha kuchangia kwenye mjadala husika?

Halafu ni possibly akawa ana ID yake ya ziada hapa JF ambayo anaweza kuitumia kuingilia jukwaa la wakubwa na MMU, maana Mwanasiasa ni agharabu kumkuta majukwaa hayo lakini si kama hawashiriki bali kuna ID za kulinda Privacy zao.
 
Mh Zito,

CCM ina reform kwa kasi, inaonekana ikawa kwenye nuru mpya kabisa hadi kufikia 2015.

1. Unaona tofauti ya msingi kati ya CCM na CHADEMA ni IPI?

2. Nini kinakuvutia ndani ya CCM amabcho hakipo CHADEMA?

3. Bado unafikiri wewe kuwa CHADEMA ni tija kwa jamii kuliko kuwa Chame kingine say CCM?

Mkuu, CCM haijafanya reform yoyote, Au wewe reform maana yake nini? mfumo ule ule, Ufisadi ule ule, rushwa zile zile, sera zile zile, porojo zile zile zilizojaa usanii bila vitendo, etc Au Mkuu kubadili nyuso ndio reform!
 
Kwakweli ni either sina swali,au nimechoshwa na SIASA NA WANA SIASA!!!
 
Mh Zitto naamini wewe ni mchumi.Umekuwa ukibadili magari ya bei mbaya na umekuwa ukigundua kuwa yana gharama kubwa kuyamiliki:=

-Je unahitaji mara ngapi ili uweze jua kuwa choice zako ni wrong?
-Je unawezaje kuwahakikishia watanzania hutafanya these kinds of wrong choices economically na kuwapa gharama km ulivyofanya ktk maisha yako mara nyingi?

- Mh Zitto mimi binafsi sijaona wapi umewajibika vya kutosha ktk kuthibitisha kuwa hutumii karata ya udini, ukanda na pretence ya umasikini kupitia watu baki.Naomba kauli yako inayoweza nishawishi kuwa umefanya jitihada za kuwaondosha watu wanaokuona upo kundi lako waamini vinginevyo.Pia ,Je una lengo la kuweka hadharani ni yako ya kupinga hizi hisia?

-Zitto unajithaminishaje mbele ya wana CDM ktk kuleta umoja wa chama na kujeng chama kuliko ubinafsi?

-Je unadhnai ulishika mujibu wako vyema,ulipoamua tangaza nia ya kugombea uraisi ktk chama kipindi ambao chama kilikuwa kikipambana kujijenga na kujipanua?naomba uwe mkweli na uelezee vyema.
 
Zitto huwa anashauriwa/anashauriana na nani katika mikakati yake ya kisiasa?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom