AshaDii,
..nilikushauri usimuulize kuhusu nia yake ya kugombea Uraisi mwaka 2015. kwa mtizamo wangu hakuna jipya litakalopatikana kutoka ktk majibu yake.
..binafsi ningependa maswali yako yajikite ktk masuala yanayohusu CDM, sera zao, na utayari wao wa kushika madaraka ya nchi.
1. Zitto na Mbowe wamesikika kumsifia Raisi Kikwete kwa kutatua kero za wananchi. Kitendo hicho ni sawa na ku-endorse rekodi ya CCM na serikali yake. Je, ktk mazingira hayo CDM wana sababu gani za kuwashawishi wananchi wawatoe CCM madarakani na kuikabidhi nchi kwa CDM?
2. Elimu yetu imeporomoka kwa kiwango kikubwa sana. Wahitimu wa vyuo vyetu wanafanya vibaya wanaposhindanishwa na wahitimu wa nchi jirani. Je, anafikiri CCM imekosea wapi? Pia CDM ina mikakati gani ya muda mfupi na mrefu kutatua tatizo hilo ktk ngazi za elimu ya msingi, sekondari, vyuo vya ualimu, na vyuo vikuu, ikiwa itapewa madaraka? Je, mikakati hiyo inatekelezwa ktk jimbo lolote lile ambalo limeshikwa na wabunge wa CDM??
3.Tukiwa bado kwenye elimu; CDM walitoa ahadi kwamba elimu ya msingi na sekondari itakuwa bure. Je, CDM ikipewa madaraka utekelezaji wa ahadi hiyo utachukua muda gani? Pia serikali kuchukua mzigo wa kugharimia elimu ya msingi na sekondari 100% haoni kwamba utaikosesha serikali mapato ambayo yangetumika kuboresha viwango vya elimu??
4. Sera ya ubinafsishaji na soko huria imeshindwa kutatua tatizo la ajira kwa vijana. Je, CDM watarekebisha vipi tatizo hilo?
5.Uzalishaji ktk sekta za kilimo na ufugaji umeendelea kushuka nchini. Tunaomba atueleze sera na mkakati wa CDM kuinua kilimo nchini. Nini maoni yake kuhusu mpango wa CCM wa kilimo kwanza.
6.Sera ya mambo ya nje na mahusiano ya kimataifa ya CDM. Nini tofauti kati ya CCM na CDM ktk eneo hilo. Je, CDM ina msimamo gani kuhusu Tanzania kujiunga na OIC? CDM ina msimamo gani kuhusu ushiriki wetu ktk jumuiya za SADC na EAC? Je, ni nini hasara na faida za msimamo wa Tanzania kuhusu ARDHI ktk jumuiya ya EAC? Je, ni nini faida na hasara msimamo wa Tanzania kuhusu mkataba wa ulinzi wa EAC?
7.Uwekezaji wa serikali ktk miradi mikubwa. Nini faida na hasara za serikali kuwaachia wawekezaji jukumu la kujenga bandari, viwanja vya ndege, na miradi ya umeme? Ikiwa CDM watapewa madaraka serikali yao itawekeza ktk miradi ipi mikubwa?? Fedha za miradi hiyo zitatoka ktk vyanzo vipi??
8.Suala la michezo. Kwanini Tanzania tumeshindwa kufanya vizuri ktk mashindano ya kimataifa pamoja na kwamba mapesa mengi sana yametumika ktk vilabu vya mpira wa miguu?? Nini maoni yake kuhusu mtizamo kwamba Tanzania iachane na mpira wa miguu na badala yake ielekeze rasilimali na nguvu zake ktk riadha ambayo tuliwahi kuwa na rekodi nzuri??