Kumekuwa na mashinikizo kutoka EU na US kuwa twaweza kuwekewa vikwazo kwa sababu zaidi ya 15 walizoziona kuwa serikali yetu haiheshimu. Sababu hizo zilianza kupigiwa kelele humu ndani na sasa wakubwa wa dunia wameona waingilie kati.
Nafahamu wapo watu kama Mugabe ambao walikataa kukubali masharti ya EU na US na raia wakaendelea kuvumilia taabu kwa vile waliheshimu historia ya Mugabe katika upiganiaji uhuru wa nchi yao na jinsi alivyo teseka kwa kukaa hata gerezani muda mrefu kwa ajili ya nchi yake.
Jee ni halali kwetu mtu asiye na historia yeyote na nchi hii ambaye mwenyewe anasema "alisukumiziwa" madaraka hayo makubwa tukavumilia mateso yatakayo tokana na vikwazo kwa ajili ya maamuzi yake ya kiburi?
Nadhani kama uzalendo ausemao kila siku upo kwake, basi aamue kukaa pembeni kuepusha mateso kwa raia maana yeye haonyeshi kuyakubali masharti hayo kwani atageuka jiwe la chumvi.
Tunamshukuru kwa aliyo fanya hadi sasa na wengine wataendelea, ila kumvumilia kama Mugabe itakuwa ngumu kwani hana kabisa historia inayo stahili hilo