Unaongelea nchi kama France ambayo population ni 69% irreligious na 29% ni atheists,ofcourse by default wataokamatwa wengi ni waislamu kwasababu pia France ndio nchi inayoongoza ulaya kwa kuwa na waarabu wengi,ambao wengi ni waislamu pia. Utamaduni wa kifaransa kwa muda mrefu sana haukubaliana na mambo ya dini,mfano mzuri ni swala la Charlie Hebdo,gazeti lilikuwa lina'attack dini zote kwenye matoleo yake but ilionekana kama waislamu ndo wanaonewa,waislamu wengi ndio waliokuwa wanalalamika,ingawa wakristo,papa,Yesu na Mungu alikuwa anachorwa mara kwa mara pia.
E.U ilituma wajumbe Belgium kuongea na Lissu,muda mrefu sana kabla ya issue za ushoga kuibuka Tanzania,hiki ni kisingizio ambacho wengi tunapenda kukitumia kwamba E.U wameibuka kwenye issue za ushoga tu.
Mambo mabovu kwenye hii nchi yameanza zamani na yalikuwa yanaangaliwa tu na mataifa mengine.
Uhuru hakushinda kesi Hague!!?baada ya kushinda kesi,umeona anavyoishi na wapinzani wake!!?..... Future za kidemokrasia ziko wapi kwa Uganda,Rwanda na Burundi!!?unataka kuishi kwenye nchi ambayo unakatwa mshahara ili kuchangia uchaguzi wa kiongozi ambaye hataki kutoka madarakani,anajibadilishia katiba tu,kila inapokaribia uchaguzi!!!?
Siamini E.U iko perfect wala Mataifa ya Magharibi yako perfect,mengi yana makosa yao pia but mengi pia yamekomaa kidemokrasia na issue za haki za binadamu,tofauti na mataifa yetu huku ambako asilimia kubwa bado tuna'cherish authoritarian over democratic rule,na kwa namna moja au nyingine tunahitaji kuwe na watchdog ili kunapotokea uminywaji wa kidemokrasia/uvunjaji wa haki za binadamu tuwe na sehemu za kwenda kulilia,nchi nyingi za Africa hazijakua kidemokrasia kuwe atleats na tume huru kama mahakama kuu Ile ya Kenya ilivyofanya kwenye uchaguzi uliyopita,so twende tukalilie wapi haki zetu!!?
Tukuwe kidemokrasia,umeona E.U au Mataifa ya Magharibi yanahangaika na Nchi kama Ghana,Namibia au Botswana!!?ni nchi zinazoendelea kukuza demokrasia ya kweli na husikii kelele wala Kiki za kijinga.
Swala la Mwisho,wakati wa JK hakukuwa na issue za mashoga!!?alipokuwa anaulizwa alikuwa anajibu nini!!?"Hili sio swala langu binafsi ni swala la Utamaduni wa Kitanzania,tukifikia wakati watanzania wanapenda kuliongelea tutaongea"....Finito,hakuna kukamata mashoga wala kuhangaika nao,nani alidhurika au kukosa chochote!!?Hii mihemko ya ushoga inatoka wapi kama sio cheap publicity stunts kuonekana kama viongozi wanafanya kazi kumbe hamna lolote,btw hizo cheap publicity stunts pia zinatumika na viongozi wa ulaya kwa wanachi wao kuonyesha wanafanya kazi na kusimamia haki za binadamu,so tusilaumu upande mmoja tu.