Enyi mliooa, mlipataje wake?

Enyi mliooa, mlipataje wake?

Kumbe nanyi mnakuwaga desparate🙆🙆
Ila mnavyojikutaga miungu sasa😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Habari wakuu.

Poleni sana kwa majukumu, Hoja yangu ni kwamba imefika wakati nataka kuoa sasa, ila sasa imebidi niulize kwa mliooa. Mmepataje wake wakuoa? Maana toka nipate wazo la kuoa nimekua nazurula sana maeneo mbalimbali nikiamini nitakutana na anayenifaa, hii hali imenifanya hata nikiwa nyumba ya ibada nisiwe makini na ibada bali nakagua mke, hata nikiwa kwenye daladala yaani akipanda Dada nakuwa makini sana nikiamini labda ndo huyu..!
MSAADA WENU TAFADHARI...

Mkuu

Don't trust any woman you see kwenye daladala,sijui Mlimani City,sijui sokoni,sijui kanisani,sijui barabarani...

Ni too much of a risk mzee...

Easiest and safe ni uulizie kijiijini/mkoa unaotoka wakupe actual referrals!

Kwanini referrals zilizotoka kwenu ni more appropriate ni kwasababu hao wasichana unaopewa referral wanawajua tangu wakiwa wadogo na wanajua walipo now na wanafanya nini na walikua wana behave vipi wakiwa wadogo!

Kuna probability ya wakengeukaji ila ukichukua sample ya 10 girls,utapata mmoja hapo ambae ni perfect fit!

Don't trust any woman in Dar es Salaam unaemuona tu hivi!
 
Dah nimekuelewa saaana mkuu nashukuru sana
Mkuu

Don't trust any woman you see kwenye daladala,sijui Mlimani City,sijui sokoni,sijui kanisani,sijui barabarani...

Ni too much of a risk mzee...

Easiest and safe ni uulizie kijiijini/mkoa unaotoka wakupe actual referrals!

Kwanini referrals zilizotoka kwenu ni more appropriate ni kwasababu hao wasichana unaopewa referral wanawajua tangu wakiwa wadogo na wanajua walipo now na wanafanya nini na walikua wana behave vipi wakiwa wadogo!

Kuna probability ya wakengeukaji ila ukichukua sample ya 10 girls,utapata mmoja hapo ambae ni perfect fit!

Don't trust any woman in Dar es Salaam unaemuona tu hivi!
 
Hapa watu watakuambia *Sali Sana Mungu atakuonesha*
Wakati wao walikula na kuliwa mingo mpaka kuolewa.
99% ya wanandoa hakuna aliyekaa tu na kusali Mungu akamuonesha.
Tamaa za mwili ndio zilianza.
Hiyo moja nayo nimeiacha kwa kuwa huwa Sina uhakika na yanayoongelewa.!!

Tumejaa uongo uongo tu.
Mwambieni kijana atongoze wanawake!!
 
Kama huko Dar utapata taabu sana, kila demu unayeona anakufaa atakwambia anasoma chuo au anasubir kujiunga na chuo,kila demu mjuaji,kwao wamejenga, sasa wewe uje kumbahatisha anayelala kwenye kochi umri utakuwa umekuacha, ili kurahisisha mambo tembelea sehemu za clinic utapata single mother, hao hawana mizengwe.
 
Ukitaka mke mzuri mwangalie tabia za Mama wa Mke unae muoa,

Before ya mke wangu, nilikuwa na Binti mmoja tukienda kula tunaagiza Sato wawili na tulipo bakisha haangaiki kuomba afungiwe na mbaya zaidi alikuwa anaagiza vitu vyenye bei harafu vinamshinda.

Oohoo Mungu wangu... Nakumbuka first time nipo out na huyu ambae ni Mke wangu.. Alisema tuagize Sato mmoja na chip's Mbili... Na tulibakisha kwa sababu stori zilichukua nafasi kubwa.. Aliomba afungiwe kisha akaniambia chukua ukifika Home utakula... Nilimuona huyu vipi aoni noma hii sehemu tulivu hivi harafu mambo ya kufunga funga.. Ilikuwa saa nne usiku.

Nilivyo fika home nikavuta bangi kisha ndio nikazama kwenye tathimini juu yake... Ganja inaisha kichwani saa nane usiku njaa ya hatari.... Nikakumbuka ooohoo I have something. Mke mwema utamjua kwa Matendo na tabia zake.

Hahah
 
Habari wakuu.

Poleni sana kwa majukumu, Hoja yangu ni kwamba imefika wakati nataka kuoa sasa, ila sasa imebidi niulize kwa mliooa. Mmepataje wake wakuoa? Maana toka nipate wazo la kuoa nimekua nazurula sana maeneo mbalimbali nikiamini nitakutana na anayenifaa, hii hali imenifanya hata nikiwa nyumba ya ibada nisiwe makini na ibada bali nakagua mke, hata nikiwa kwenye daladala yaani akipanda Dada nakuwa makini sana nikiamini labda ndo huyu..!
MSAADA WENU TAFADHARI...
Aiseee kuwa makini sana mkuu katika hiyo sekta.
Unamuona mwenzio gwajima na skendo zake zote bado anatetewa na mkewe,si umemuona mkewe alivyokuwa na msimamo thaibiti Ndugu?

Alafu chonde chonde usiyafite mke wakati una genye zimekupanda,kila mke utamuona mzuri sana kwa sababu ya tamaa za mwili.

Mke ambae unaweza kudumu nae ni yule ambae ukimuona tu yanakujia mawqzo ya kumuoa zaidi ya kufanya nae mapenzi tu.maana yake ni kwamba kuna wanawake ukiwatazama tu mavazi yao basi wanakuvutia upate hamu ya kuzini nao.sasa mke akiwa hivyo tahadhari sana.

Nakumbuka wakati nipo kijana nasoma kabla sijaoa kulikuwa na dada falani anavaa hijabu vizuri sana ikawa namzimia sana kwa kweli mpaka nikimuona napata picha ameshakuwa mke wangu tayari na tunaishi vizuri sana,lakini kuna wadada wengine nikiwaona nawaza uchafu tu moja kwa moja.sasa wewe angalia sana sana sana.

Alafu angalia dini yako mkuu,kama ni mkristo basi pahala safi pa kupata mke ni kanisani.sasa kanisani NAKO UCHAGUE,SIO KWA KUWA NI KANISA BASI UNACHUKUA YEYOTE.utajuta na kuleta uzi hapa.kuwa makini kanisani uangalie na kuwashirikisha wazoefu wa sehemu hiyo.

Lakini pia naomba kama una mama basi mtumie kumuulizia akutafutie binti mwenye tabia njema sana anayemjua,wanamama wanajuana sana mtaani wanajua kabisa kwamba nyumba flani yule binti ametulia au hajatulia.kwa hiyo wanajua sehemu sahihi.
Alafu badala ya hapo sasa umwambie akutafutie mke,mama hawezi kukuimgiza chaka hata siku moja,ataeatumia wenzie wamtafutiee nyumba gni kuna binti mzuri.

Akipatikana unawaambie wasiambiwe hapo kwa binti kama una lengo fulani,wewe ufanye mipango kumuona huyo binti na kumtafakari nama alivyo,huku na wewe ukiulizia wadau mbali mbali juu ya mwenendo wake,ukiona umempenda namna alivyo na tabia ziko fressh basi hapo anza kutupa ndoana na kupeleka taarifa rasmi kwa huyo dada mdogo mdogo ili naye tuone kama atakuwa amekukubali.

Ila tu mkuu...

Ukitaka mke mwema basi kuwa wewe mwema kwanza.anza kutengenea mda huu tulie na kutuliza akili sio useme utatulia ukioowa shauri yako
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom