Elimu ya bure Kuhusu umeme wa jua

Elimu ya bure Kuhusu umeme wa jua

Watts sijajua ila wameandika 100volts-240volts.

42 inches TV ni 300watts na hiyo ni ac TV. Natamani sana kama tungewasiliana Kabla ya kuinunua ningekushauri kwa uzuri zaidi. Maelezo ni marefu nipm nikupe namba yangu unipigie tuongee
 
Kwanza kabisa naomba nitahadhalishe kuwa mimi sio expert wa hii kitu ila nahakika walau mutapata mawili au matatu lakin pia naamini wataalam zaidi watakuja kufafanua na pengine kujibu maswali.

Ni ukweli usipingika kuwa watu wengie wanauelewa wa hii nguvu lakin pia nahakika kuwa kwa namna moja ama nyingine elimu ni bahari.

Kwangu nimefunga

1. Panel ya 160w (made in ujerumani).

2. Dry battery ya 500N (made in Ujerumani)

3. Inverter ya Victron/Phoenix) 12v, 350va (made in Philipine) ambayo ni auto na hina kelele

4. Dash board 15A/ solar power controller aina ya Steca/Solarix PRS 1515 ya (made in zhing zong)

Na vifaa tajwa hapo juu vinategemeana na matumizi yako ila mimi nina run

TAA

1Watt 5pcs...vyumbani na chooni
2Watt 6pcs...sebureni, corridor na store
3Watt 9pc...nje

Hizi zinauzwa pale Quality Centre moja 5000/ na zinamwanga wa kutosha kama nilivyoeleza hazili umeme mwingi tofauti na zamani kipindi nanunua niliuziwa taa zenye watt 10 mpaka 20 ziko kama tube light hizi za sasa ni bulb ambazo kimsingi ilikuwa hata TV kuangalia ni anasa maana taa tu hazikeshi usiku kucha.

(Nilizibadirisha kwa kununua kwanza chache ili nitest mwanga nikakuta zipo poa kabisa) so ikanilazim nibadiriahe zote.
Zinasambazwa na Step Entertaiment hawa jamaa wa Bongo movie.

Na kwa hakika hapa kwenye taa ndo wengi wetu tunaumia maana taa zinakuwa ni A kizamani wakati tech ime advance sana

Nina Flat Tv 32"
Nina Laptop

Ambapo nimekuja kugundua laptop inakula umeme mwingi sana kuliko flat tv maana unaweza kuangalia tv siku nzima na ukawa safi tu kuliko tofauti na ukitumia laptop. Hapa siongelei tv zile za zamani zenye shape kama kisogo maana ninayo lakin nilishindwa kuitumia kwenye solar.

FAIDA

Haitatokea hata siku moja vifaa vyako kuungua
Pia gharama yake ni mwanzo tu wakat unanunua vifaa.

HASARA

Umeme wake hautoshi mahitaji yote mf pasi, jiko, fridge japo siku hiz zipo water pump, pasi, fridge na freezer za solar ila sijajua utendaji kaz wake.

Cha zaidi nashauri Panel yako iwe upande ambao jua ndo linaonekana kwa asilimia kubwa japo panel zingine zinahitaji mwanga tu then unatosha kuchaji betri yako.

Na fundi aifunge panel sambamba na bati ili kuisaidia uchafu ama vumbi kuwa linatoka lenyewe na hii itasaidia ufanisi wake pia, kuliko kuifunga horizontal maana itasababisha uchafu na vumbi vigande juu yake.

ANGALIZO

Vitu muhimu vya kuangalia wakati wa manunuzi ni Panel, Betri na Inveter ila kama utahitaji kuwa una chaji simu au radio au tv na kama ni taa tu hauhitaji inverter.

Wataalam munaweza kuongezea hapo.

Pamoja
alfred.kohi@kcd.co.tz

samahani ndugu,ninatumia invertor imeandikwa H-160,12v Dc to 230V Ac,ss nilikuwa nahitaji kununua dryer lenye 230v naomba msaada naweza nikatumia?
 
Molembi TV yako. Uliyonunua ni watts ngapi? Ni DC TV au no ac TV ?

samahani,ninahitaji kununua dryer ya mkono yenye 230v na invertor yangu imeandikwa h-160..12v Dc to 230v Ac..je nitaweza kuitumia vizuri tu?
 
samahani,ninahitaji kununua dryer ya mkono yenye 230v na invertor yangu imeandikwa h-160..12v Dc to 230v Ac..je nitaweza kuitumia vizuri tu?

Betri ya ukubwa gan na panel..?
 
Nashukru sana kwa darasa nimemnunulia mama solar panel watts 100 ana tumia taa 2 tv flat inch 42 na deki betry N100 lakini akiwasha tv akiangalia kwa muda wa saa 1 inazima tatizo ni nini?mkuu ikohi jubilant.
Molembe pole nimechelewa kuona swali lako naomba unipm nikupe namba yangu unipigie nikusaidie
 
Last edited by a moderator:
Ukiwekeza kwenye solar utapata faida ya muda mrefu. Kuna jamaa tumemfungia solar, system yake ina uwezo wa kuwasha jiko la umee burner 1, fridge 2 za wtt 180, deepfreezer kubwa 1, washing machine si ya kati 1, fan panga boy 3. Hivi vifaa vyote vinaweza kutumika kwa pamoja wakati wa mchana kuanzia saa 4 am hadi saa 9pm vinazimwa kwa ajili ya matumizi ya baadaye usiku.
 
Ni kweli, umeme mionzi ni mkombozi. Nimemua kutokununua UPS sasa Ninatumia Mionzi Jua ni raha mustarehe ofisini.
 
Unatakiwa kuongeza uwezo wa system yako.

Pengine ungemuuliza anataka iyo system ikae kwa mda gani wakati wa usiku? Ukishajua ndo umwambie aongeze ni na nini ili kukuza mfumo wake. Lkn ukimwambia aongeze uwezo wa mfumo wake kwa asie na taaluma na hayo mambo unamuweka njia panda.
Ni hayo tu..
 
Pengine ungemuuliza anataka iyo system ikae kwa mda gani wakati wa usiku? Ukishajua ndo umwambie aongeze ni na nini ili kukuza mfumo wake. Lkn ukimwambia aongeze uwezo wa mfumo wake kwa asie na taaluma na hayo mambo unamuweka njia panda.
Ni hayo tu..

kweli angenipa elimu zaidi,maana sielewi niongeze nn
 
By Professional mie ni electronics engineer. Ninaishi dar ninaweza kumsaidia yeyote kuhusu hii system bila malipo yoyote, nitakushauri kabla ya kunua na kufunga..online

Nimefunga Solar System nyumbani 2008 baada ya serekali kubadili mfumo na kuleta LUKU service Charge
Nina 2 Panels 90Watts @ = (180Watts)
Batery 7 sealed za 150Ah@ = 1050Ah

Matumizi
Nina Desktop Computer 1
Nina Laptop 1
Nina Solar Frige kubwa 290Lrs
Nina 500Watts Power invetor
Nina 32 Inch TV flat screen
Nina taa 3watts 11 ndani
nina taa 5watts 7 nje
Nina Brender 400Watts
Nina Music system 2000Watts PMPO ikipiga just kama uko disco
Mafundi wanakujaga na machine zao za kukata chuma na mbao wanatumia bila shida yoyote.

Sijutii kufunga solar system sio kwamba niko sehemu ambayo Tanesco hawajapita hapana nguzo ya umeme iko 1 meter kutoka nyumba yangu ila utumwa sitaki, kila siku bei ya umeme inapanda utasiki watu wanalia na kulalamika. 2008 elfu kumi nilikuwa napata 112 units sasa hivi 10,000 hata 38 units hupati
Mabadiliko ya kweli hutokea kwenye fikra na unayoyaona kwa nje ni matokeo tu...

Watanzania Tubadili jinsi tunavyo fikiria life is good
hivi vyote ilikughalimu shilingi ngapi na kwa sasa inaweza kufikia bei gani
 
Kwanza kabisa naomba nitahadhalishe kuwa mimi sio expert wa hii kitu ila nahakika walau mutapata mawili au matatu lakin pia naamini wataalam zaidi watakuja kufafanua na pengine kujibu maswali.

Pamoja
alfred.kohi@kcd.co.tz

Asante sana mtaalamu kwa ushauri mnono.

Nimeshindwa hesabu za matumizi.

Naomba Msaada: Nina 200Wpanel na 12V DC battery. Inveter matching size

Nimeweka inveter kwendaAC. Sasa kwa maasa 10 usiku niweke bulb za 40 W energy saver ngap?? Thanks
 
Asante sana mtaalamu kwa ushauri mnono.

Nimeshindwa hesabu za matumizi.

Naomba Msaada: Nina 200Wpanel na 12V DC battery. Inveter matching size

Nimeweka inveter kwendaAC. Sasa kwa maasa 10 usiku niweke bulb za 40 W energy saver ngap?? Thanks
Battery yako ina Ah. ngapi?
 
Betri ya N500 unatumia muda gani kuicharge mpaka ijae maana umesema panel yako ni watts 160 ambayo nazani current yake ni ndogo sana kuweza kuchaji battery ya N500 ukilinganisha na maxmum peak sun hours kwa tropical countries ni 4 hours per day pia wakati jua linachaji battery kunauwezekano kwamba kukawa na some runing loads ambazo pia zitakua zinafanya battry lizidi kuchelewa kujaaa,,je kuna formula yoyote umetumia kupata size ya battery na panel yako??je kuna formula umetumia kupata size ya inverter
 
Back
Top Bottom