Kwanza kabisa naomba nitahadhalishe kuwa mimi sio expert wa hii kitu ila nahakika walau mtapata mawili au matatu lakini pia naamini wataalam zaidi watakuja kufafanua na pengine kujibu maswali.
Ni ukweli usiopingika kuwa watu wengi wana uelewa wa hii nguvu lakini pia nahakika kuwa kwa namna moja ama nyingine elimu ni bahari.
Kwangu nimefunga
1. Panel ya 160w (made in ujerumani).
2. Dry battery ya 500N (made in Ujerumani)
3. Inverter ya Victron/Phoenix) 12v, 350va (made in Philipine) ambayo ni auto na haina kelele
4. Dash board 15A/ solar power controller aina ya Steca/Solarix PRS 1515 ya (made in zhing zong)
Na vifaa tajwa hapo juu vinategemeana na matumizi yako ila mimi nina run
TAA
1Watt 5pcs...vyumbani na chooni
2Watt 6pcs...sebureni, corridor na store
3Watt 9pc...nje
Hizi zinauzwa pale Quality Centre moja 5000/ na zina mwanga wa kutosha kama nilivyoeleza hazitumii umeme mwingi tofauti na zamani kipindi nanunua niliuziwa taa zenye watt 10 mpaka 20 ziko kama tube light hizi za sasa ni bulb ambazo kimsingi ilikuwa hata TV kuangalia ni anasa maana taa tu hazikeshi usiku kucha.
(Nilizibadilisha kwa kununua kwanza chache ili nitest mwanga nikakuta zipo poa kabisa) so ikanilazimu nibadilishe zote.
Zinasambazwa na Step Entertaiment hawa jamaa wa Bongo movie.
Na kwa hakika hapa kwenye taa ndo wengi wetu tunaumia maana taa zinakuwa ni A kizamani wakati tech ime advance sana.
Nina Flat Tv 32"
Nina Laptop
Ambapo nimekuja kugundua laptop inakula umeme mwingi sana kuliko flat tv maana unaweza kuangalia tv siku nzima na ukawa safi tu kuliko tofauti na ukitumia laptop. Hapa siongelei TV zile za zamani zenye shape kama kisogo maana ninayo lakini nilishindwa kuitumia kwenye solar.
FAIDA
Haitatokea hata siku moja vifaa vyako kuungua
Pia gharama yake ni mwanzo tu wakati unanunua vifaa.
HASARA
Umeme wake hautoshi mahitaji yote mf pasi, jiko, fridge japo siku hiz zipo water pump, pasi, fridge na freezer za solar ila sijajua utendaji kazi wake.
Cha zaidi nashauri Panel yako iwe upande ambao jua ndo linaonekana kwa asilimia kubwa japo panel zingine zinahitaji mwanga tu then unatosha kuchaji betri yako.
Na fundi aifunge panel sambamba na bati ili kuisaidia uchafu ama vumbi kuwa linatoka lenyewe na hii itasaidia ufanisi wake pia, kuliko kuifunga horizontal maana itasababisha uchafu na vumbi vigande juu yake.
ANGALIZO
Vitu muhimu vya kuangalia wakati wa manunuzi ni Panel, Betri na Inveter ila kama utahitaji kuwa una chaji simu au radio au tv na kama ni taa tu hauhitaji inverter.
Wataalam munaweza kuongezea hapo.
Pamoja
alfred.kohi@kcd.co.tz