Elimu ya bure Kuhusu umeme wa jua

Elimu ya bure Kuhusu umeme wa jua

Hahaha imebidi nicheki ila binafsi nachukia sana hii tabia ya akina Mohamed wao huwa wazuri sana kukosoa tu bila kutoa ushauri au kusaidia chochote.

Huo muda uliotumia kuandika kulasa nzima halafu hakuna cha msingi ulichosaidia, naona na wewe ni miongoni walipitia kwenye mitaala isiyo na tija
 
Mohamed Ngwasu nawe malizia hako kautam bas kuna kitu nilikuwa nasubir hapo lakn hujasema tunasubir
 
Last edited by a moderator:
HII ni hali ya "kitanzania ni mabingwa kukosoa" hapa tunaunganisha mawazo na wala hatulipwi humu kupitia hizo masters, na hilo litapunguza wachangiaji. Lazima tuelewe kuwa hata wataalamu wana wakati mgumu kwa sasa,

mfano vifaa vingi sokoni vinatofauti kubwa ya sifa ya nje, na hali halisi ya utendaji kazi {unaandikiwa 120w kumbe ni 80w, 10A kumbe ni 6A} hapa mtaalam huyu lazima atafeli kuleta matokeo mazuri. KENYA leo hawaangalii vyeti tu katika kuajili wanajikita zaidi katika uzoefu wako kazini.

USHAURI:bei ina uhusiano na ubora kwa seller mkweli, sola zinauzwa kwa wati moja kulingana na ubora-bongo. 1:1600,1:1800,1:2000,1:2500,.1:3000,1:4000,...hii kulingana na ujazo wa cells.(bei zidisha kwa wati unazozitaka).
 

Attachments

  • 1409116043300.jpg
    1409116043300.jpg
    46.3 KB · Views: 301
  • 1409116066387.jpg
    1409116066387.jpg
    26.9 KB · Views: 284
  • 1409116085031.jpg
    1409116085031.jpg
    37.3 KB · Views: 275
  • 1409116104910.jpg
    1409116104910.jpg
    40.6 KB · Views: 262
HII ni hali ya "kitanzania ni mabingwa kukosoa" hapa tunaunganisha mawazo na wala hatulipwi humu kupitia hizo masters, na hilo litapunguza wachangiaji. Lazima tuelewe kuwa hata wataalamu wana wakati mgumu kwa sasa,

Mfano vifaa vingi sokoni vinatofauti kubwa ya sifa ya nje, na hali halisi ya utendaji kazi {unaandikiwa 120w kumbe ni 80w, 10A kumbe ni 6A} hapa mtaalam huyu lazima atafeli kuleta matokeo mazuri.

KENYA leo hawaangalii vyeti tu katika kuajili wanajikita zaidi katika uzoefu wako kazini. USHAURI:bei ina uhusiano na ubora kwa seller mkweli, sola zinauzwa kwa wati moja kulingana na ubora-bongo.

1:1600,1:1800,1:2000,1:2500,.1:3000,1:4000,...hii kulingana na ujazo wa cells.(bei zidisha kwa wati unazozitaka).

Mkuu NAMKONG'O tunakuomba umalizie huo ufafanuzi wa hizo bei ingependeza kama ungetutajia kila kampuni
 
Sorry nilipata dharula ikabidi nitoke kwenye jamvi. sasa ndugu zangu iko hivi technically unapofanya estimate ya solar installation zingatia yafuatayo makadirio yanaanzia kwenye load kwenda kwenye source yaani cha kwanza kabisa unapaswa kujua utakuwa na load ratings ya watts ngapi e.g lamps TV radio etc mzigo wote unaconsume power kiasi gani.

Then unaangalia sasa mfumo wako utakuwa wa namna gani kama utahitaji invertor ili loads zote zitumie ac au utatumia moja kwa moja Dc.

tuanzie na dc baada ya kujua total load unakuja kwenye battery sasa unapaswa kujua ni battery ya size gani ikiwa full charge itaweza kudrive mzigo wako kwa masaa yasiyopungua 16 katika full load kwa kiwango cha 75% yaani mzigo wote ratings yake iwe ni 75% ya battery na uwashwe kwa masaa 16.

Baada ya hapo unaangalia solar panel lazima iwe ya ukubwa ambao itaweza kucharge battery na kujaza kwa masaa 4 ya jua kali likiwaka mfululizo yaani kuanzia saa tano hadi saa tisa alasiri.

Then solar regulator lazima iwe na ratings kulingana na ukubwa wa battery yako. then wiring system unatakiwa (recomended) kutumia cable ambazo ni flexible cable na hii ni shauri ya kuavoid skin effect na ratings zake ziko hivi kwa wiring unahitaji flexible cable ya 2.5mm sq minimum na maximum ni 4mm sq kutegemeana na urefu wa ruti ya wiring yako.

Cable kutoka solar panel via solar regulator to battery minimum ni flexible cable ya 6mm Sq kulingana na ukubwa na idadi ya panel na battery . taa ni dc lamp za watts kidogo lakini mwanga mkubwa. zingatia kuwa battery lazima iwe ni solar battery na siyo battery ya gari. mafundi wengi wana ignore waya ni jambo la kawaida kukuta mtu kafunga waya za speaker kwenye solar .

Na kwa ac ukitumia invertor formular ni ile ile unanza na load then invertor ya ukubwa gani inaweza ikawasha mzigo wako at list kwa masaa kumi na mbili bila kuchemka baadaye battery ya ukubwa gani inaweza kudrive invertor yako kwa mzigo ulionao kwa masaa kumi na mbili bila kuzima ikumbukwe kuwa invertor peke yake ukiiwasha tu bila ya mzigo inaconsume charge kwa hiyo unapaswa kutest invertor yako kabla haujaichukua.

Then solar panel kwa vigezo vile vile na regulator. cable kutoka solar panel hadi battery ni vile vile ila wiring taa ni 1.5mm sq pvc cable na socket ni 2.5 mm pvc cable. gharama ya vifaa inategemeana na product ila now days bei zimeshuka sana baada ya serikali kutoa rudhuku kwa waingizaji kwa sababu ya rea tofauti na miaka mitatu iliyopita gharama ilikuwa ni kubwa sana.

Kwa mikoa na wilaya za pembezoni nimeona bei bado haiwasaidii wananchi bidhaa ni feki na zinauzwa kiulanguzi bei hadi mara mbili ya sehemu zingine. naomba kuhitimisha maswali ruksa.
 
Mohamed Ngwasu

Mkuu umezungumzaukweli ila kuna vitu kadhaa naomba nikuongezee. Kwenye solar panel kuchaji battery masaa 4 hii sio recommended time.

Tunaita Peak Sun Hours(P.S.H) muda ambao miale ya mwanga wa jua hupiga ktk kioo cha solar kwa kiwango cha juu at 100% efficiency. Na hii haimaanishi masaa mengine yanayobakia solar panel haipati jua na kuzalisha umeme, hapana.

Hii ina maana jua linapochomoza asubui hadi linapozama jioni solar panel hunyonya miale ya mwanga wa jua na kuigeuza kuwa umeme na kuitunza kwwnye battery. Ila hayo masaa yanayozungumziwa ni kipindi solar huzalisha umeme kwa kiwango kikubwa kuliko masaa mengine.

Na hayo masaa hutodautiana kati ya eneo moja hadi lingine( mkoa na mkoa, nchi na nchi)

Halafu solar regulator SIO LAZIMA iwe na rating kutokana ukubwa wa battery. Solar regulator kwa sabab kazi yake ni kupitisha na kucontrol umeme unaotoka kwenye solar panel kwenda kwwnye battery na unaotoka kwenye battery kwenda kwenye vifaa vinavyotumia umeme wa DC,

hivyo kikubwa tunachokiangalia ni current(A) zinazotoka kwenye panel na voltage(V) zake. Kwa maana charge controller zipo za aina mbili 1.S.H.S( solar home system) 2. MPPT( maximum power point tracking).

Pia kwenye mifumo ya solar recommended cable ni DC Cable haijalishi iwe ni Flexible au PVC.

Asante.
 
Last edited by a moderator:
solar panel nyingi zimefungwa 'Diod' ambazo kazi yake ni kuruhusu chaji ya kupita kutoka kwenye solar kwenda kwenye betri na diod hizi haziruhusu chaji kuingia kwenye solar cells.

(Fahamu kuwa solar panel ikikosa/kuharibika diod) inanyonya umeme hata kama betri itakuwa imejaa chaji, inapungua sana. Hili linafanya watu wengi kuziona betri zao mbovu na kuzitupa.

JAMBO LA KUCHAJI BETRI ni solar ziwe na watt kubwa kuliko betri, hii itasaidia betri kupata kiwango kizuri cha chaji kuanzia asubuhi.
 
Mkuu umezungumzaukweli ila kuna vitu kadhaa naomba nikuongezee. Kwenye solar panel kuchaji battery masaa 4 hii sio recommended time. Tunaita Peak Sun Hours(P.S.H) muda ambao miale ya mwanga wa jua hupiga ktk kioo cha solar kwa kiwango cha juu at 100% efficiency.

Na hii haimaanishi masaa mengine yanayobakia solar panel haipati jua na kuzalisha umeme, hapana. Hii ina maana jua linapochomoza asubui hadi linapozama jioni solar panel hunyonya miale ya mwanga wa jua na kuigeuza kuwa umeme na kuitunza kwwnye battery.

Ila hayo masaa yanayozungumziwa ni kipindi solar huzalisha umeme kwa kiwango kikubwa kuliko masaa mengine. Na hayo masaa hutodautiana kati ya eneo moja hadi lingine( mkoa na mkoa, nchi na nchi)

Halafu solar regulator SIO LAZIMA iwe na rating kutokana ukubwa wa battery. Solar regulator kwa sabab kazi yake ni kupitisha na kucontrol umeme unaotoka kwenye solar panel kwenda kwwnye battery na unaotoka kwenye battery kwenda kwenye vifaa vinavyotumia umeme wa DC,

hivyo kikubwa tunachokiangalia ni current(A) zinazotoka kwenye panel na voltage(V) zake. Kwa maana charge controller zipo za aina mbili 1.S.H.S( solar home system) 2. MPPT( maximum power point tracking).

Pia kwenye mifumo ya solar recommended cable ni DC Cable haijalishi iwe ni Flexible au PVC.

Asante.

Regulator ina umuhm gan haswa...
 
Regulator ina umuhm gan haswa...

Umuhimu wa solar regulator ni kudhibiti umeme unaotoka kwenye solar panel kwenda kwenye battery na unaotoka kwenye battery kwenda kwenye vifaa vinavyotumia umeme wa DC( umeme wa battery),

yaani kwa tafsiri rahisi ni kuzuia battery kujazwa sana na solar na pia kuzuia kutumika sana na vifaa vinavyotumia umeme huo wa DC na pia hufanya kazi ya HVD( High Voltage Disconnect ) na LVD( Low Voltage Disconnect ).

Na pia kwenye Solar regulator ndipo kuna center connection point kati ya Solar, Battery na DC Appliance.
 
Regulator ina umuhm gan haswa...

Kumbuka Solar Regulator haihusiki na kucontrol umeme wa Inverter kwasababu Inverter hupokea umeme uliohifadhiwa tayari kwenye battery, na ndio maana connection ya kuunga Inverter huanzia kwenye battery na sio kwenye charge controller.
 
Kumbuka Solar Regulator haihusiki na kucontrol umeme wa Inverter kwasababu Inverter hupokea umeme uliohifadhiwa tayari kwenye battery, na ndio maana connection ya kuunga Inverter huanzia kwenye battery na sio kwenye charge controller.

Sawa sawa unamaanisha.....bila kuweka ile kuna ueezekano wa kujaza betri had kupasuka..?
 
Halafu... kuna uwezekano wa kuunga betri 2 za w100@ zitumike pamoja..? Na inveter ni ya w300?
 
Sawa sawa unamaanisha.....bila kuweka ile kuna ueezekano wa kujaza betri had kupasuka..?

Ndio mkuu, kwasabab Solar panel inapochaji battery huwa haijui km sasa ishajaa au haijajaa.....yenyewe inatiririsha umeme tu. Kitu pekee kinachojua sasa battery imejaa au imeishiwa chaji ni SOLAR CHARGE CONTROLLER AU SOLAR REGULATOR tu.
 
Ndio mkuu, kwasabab Solar panel inapochaji battery huwa haijui km sasa ishajaa au haijajaa.....yenyewe inatiririsha umeme tu. Kitu pekee kinachojua sasa battery imejaa au imeishiwa chaji ni SOLAR CHARGE CONTROLLER AU SOLAR REGULATOR tu.

Halafu... kuna uwezekano wa kuunga betri 2 za w100@ zitumike pamoja..? Na inveter ni ya w300?
 
Halafu... kuna uwezekano wa kuunga betri 2 za w100@ zitumike pamoja..? Na inveter ni ya w300?

Battery ziko rated interms of Ah au N na sio W km ulivyoandika. Jibu lako ni NDIO unaweza kuunga izo battery 2 za N100 na zikatumika pamoja kwa kuunga na Inverter ya 300W pia
 
Back
Top Bottom