Edward Lowassa on ITV!-Dakika 45 Part II!.

..., ila kiukweli, kufuatia afya yake kuwa mgogoro, kwa jinsi nilivyomuona akizungumza, anatoa maneno makali kwa sauti yenye fire on hisi ayes, and fear is the weapon on his heart, hivyo body language isaonekana wazi, "he is a sick man"!, hivyo hawezi kuhimili mikiki mikiki ya 2015, ....
I subscribe to this conclusion! Jamaa kesha!
 
Pasco,
Haujanijibu hapo Namba 64. Au zilikuwa ni fitna na mizengwe ya Mwalimu tu? Au Lowasa wa mwaka 1995 sio huyu wa sasa? Au sisi waTz ni wepesi kusamehe na kusahau!
 
ipo siku atakuja kuelezea tuhuma zake za ufisadi na naomba aelezee kiundani zaidi ili watanzania wajue ukweli. Mi nikimfikiriaga jk huwa mawazo yanakuja mpaka napata dhambi maana ni zaidi ya mjinga kwa kweli
Mkuu Aleyn, huwezi kupata dhambi kwa kuwaza, kimtiacho mtu najisi, ni kile tuu kitokacho, chochote kilichomo, sio najisi, hivyo kuwaza chochote sio dhambi bali ukiwaza mabaya, ukayasema au kuyatenda ndipo hukeuka dhambi!.
 
Pasco,
Hivi zile sababu za mwaka 1995 zilizomwondoa kwenye kinyang'anyiro cha Urais mapema tu kabla hata kupigiwa kura zimefutwa? Kuna siku alisafishwa? Na nani? Na kikao gani? Utakumbuka sababu kama hizo zilimwandama JSM alipojaribu tena mwaka 2005.
Alikuwa makini jana alipojibu swali la Urais kwa kifupi tu kwamba "atavuka daraja" atakapolifikia. Na mimi naamini kwa CCM hii hata hilo daraja hataliona. WATANZANIA hatuko tayari tena kuiweka sokoni nafasi hii.
Mkuu WildCard, Nyerere alikuwa mjamaa wa ukweli, ugomvi wake na EL ni baada ya kusikia EL ndie landlord wa jengo la ubalozi wa Afrika Kusini pale Masaki, by then azimio la Zanzibar, halikuwepo, baada ya kuwepo kwa azimio la Zanzibar, kumemsafisha kabisa EL, kwa sasa sio kosa tena viongozi wa CCM kumiliki mali, ndio maana hata Chenge hajafanywa chochote licha ya kukutwa na vile vijisenti vyake kule UK na hata hizi kelele za mabilioni ya Uswisi, ni kelele tuu, nothing will be done to anyone!.

Enzi za CCM ya Nyerere, sifa kuu ya uongozi ilikuwa ni uwezo na uadilifu, enzi hizo, utajiri, ulikuwa unawapotezea sifa za uongozi!, baada ya Azimio la Zanzibar, sifa kuu ya uongozi wa CCM ya sasa ni pesa!. Haijalishi hizo fedha umezipataje, "the end justfies the means", the bottom line is money, Lowassa anayo sifa hii na hivyo ni very strong candidate ukiondoa afya tete!.
 
Kipindi kimeanza, anaanza na repeat ya hoja yake ya gesi kuwa vitalu vilivyoshagawiwa vinatosha, tusiendelee kugawa vitalu. Mtaniona mjinga, ' I'm not a fool"!.


Katika hili yuko sahihi lakini yeye kama Mbunge asiishie kusema tu, ana nafasi ya kuishauri na kuishawishi serikali mpaka likafanikiwa.
 
pasco heshima mbele!
Naomba unijuze kama kweli ccm watakuwa tayari kumsimamisha el kuwa mgombea wao wa nafasi ya urais!
wawe tayari mara ngapi mkuu ulimsikia walimuuliza akawajibu
wazungu wanasema uwezi kuongea kitu mpaka wakati ujavuka mto so subirini ukifika wakati basi tutavuka jamani
infact jamaa ni kichwa najiuliza alipokuwa waziri mkuu mbona akuyafanya haya?????
 
Pasco,
Haujanijibu hapo Namba 64. Au zilikuwa ni fitna na mizengwe ya Mwalimu tu? Au Lowasa wa mwaka 1995 sio huyu wa sasa? Au sisi waTz ni wepesi kusamehe na kusahau!
nimeshakujibu, ila pia kwani Watanzania huwa tunachagua nini?!. Sisi Watanzania sio kweli kuwa ni wepesi wa kusamehe na kusahau, bali hatunaga hata kumbukumbu tumetendwa nini, ndio maana kila siku CCM inakuja na ahadi mpya, hakuna kumbukumbu yoyote ya iliahidi nini zamani na nini kilitekelezwa, sisi tunaendelea kuichagua tuu na kuichagua na kuichagua!. 2005, CCM ilikuja na kauli mbiu ya " Maisha Bora Kwa Kila Mtanzania" kwa kutumia "Kasi mpya, Ari Mpya na Nguvu Mpya!", 2010, tukaletewa " Maisha Bora kwa Kila Mtanzania, Yanawezekana " kupitia kwa "Kasi Zaidi, Ari Zaidi na Nguvu Zaidi!" ila hakuna tathmini wala kumbukumbu ya tulichoahidiwa na kilichofanyika!, sisi ni watu wa kupokea tuu!.

Amini nakuambia, kama afya ya EL sio mgogoro, na CCM ikamsimamisha Lowassa, hakuna mpinzani yoyote atakaefurukuta kwenye Urais, ubunge yes!
 
Mkuu WildCard, Nyerere alikuwa mjamaa wa ukweli, ugomvi wake na EL ni baada ya kusikia EL ndie landlord wa jengo la ubalozi wa Afrika Kusini pale Masaki, by then azimio la Zanzibar, halikuwepo, baada ya kuwepo kwa azimio la Zanzibar, kumemsafisha kabisa EL, kwa sasa sio kosa tena viongozi wa CCM kumiliki mali, ndio maana hata Chenge hajafanywa chochote licha ya kukutwa na vile vijisenti vyake kule UK na hata hizi kelele za mabilioni ya Uswisi, ni kelele tuu, nothing will be done to anyone!.

Enzi za CCM ya Nyerere, sifa kuu ya uongozi ilikuwa ni uwezo na uadilifu, enzi hizo, utajiri, ulikuwa unawapotezea sifa za uongozi!, baada ya Azimio la Zanzibar, sifa kuu ya uongozi wa CCM ya sasa ni pesa!. Haijalishi hizo fedha umezipataje, "the end justfies the means", the bottom line is money, Lowassa anayo sifa hii na hivyo ni very strong candidate ukiondoa afya tete!.


Hata kamaunampenda sana Lowassa usijaribu kupotosha historia
Azimio la Zanzibar lilipitishwa mwaka 1992
Nyerere alimzuia Lowassa kwenye uchaguzi wa 1995...
Sasa usichanganye watu
 
WAJAMANI natamani ningemsikiliza lakini kama hathubutun kumtaja mmiliki wa RICHMOND iliyomzaa DOWANS,nayo DOWANS ikamzaa SYMBION basi hata ajichome moto,ajiwambe msalabani au ajilipue hana jipya!
 
Hata kamaunampenda sana Lowassa usijaribu kupotosha historia
Azimio la Zanzibar lilipitishwa mwaka 1992
Nyerere alimzuia Lowassa kwenye uchaguzi wa 1995...
Sasa usichanganye watu
Mkuu the Boss, nakiri kukosea contents, lakini context is still valid, kosa la Lowassa mbele ya Nyerere, ni utajiri, jee leo utajiri bado ni kosa kwa CCM?.

Kumuunga kwangu Lowassa sio suala la kumpenda, ni suala la kuukubali ukweli mtupu, no one matches him!, kama umenisoma in "in between the lines", JK mwenyewe, sii lolote, sii chochote mbele ya Lowassa!. Wale wapinzani wa Lowassa shukuruni Mungu, afya yake ni issue, vinginevyo hakuna yoyote wa kumshinda, ndani na nje ya CCM, mkubali mkatae!. Japo kufuatia afya yake kuwa issue, CCM itamsimamisha Membe, bila support ya kambi ya EL, Membe is nothing, ndani ya CCM, na nje ya CCM ndio kabisa, huyu ni unyoya tuu wa kuku, unapulizwa hata na kajiupepo ka kuzimia mshumaa!.
 
Lowasa anajichanganya kati ya elimu na kilimo.anasema kuna tatizo kubwa la ajira.linatatuliwa vipi,sio kwa kilimo?lakini yeye anasema kilimo si kipaumbele kwa sasa
 
Kaswali kengine kadogo ka nyongeza: Kwa nini yuko kimya sana mle mjengoni ambako angeyasema vizuri zaidi haya alooyasema pale ITV? Mzee JSM pamoja na kutopangilia vizuri hoja zake aliendelea kuongea Bungeni. Rafiki yako Lowasa ni jasiri sana. Pamoja na kutuibia koote bado anataka atutawale tena!
 
....[/QUOTE]
Mkuu Nguruvi3, ukipitia ile page 1 utaona amezungumza nini, nikitulia nita compile na kuiupdate 1st post!.
 
ipo siku watu wataelewa kuwa EL hausiki na richmond? sisi wachache ndio tunaojua fact za richmond, tunamlaumu sana EL kwa nini alijiuzuru. Wenye kumbukumbu siku EL alipojiuzuru Bungeni alihojiwa na Tido mhando wa TBC kwenye mazungumzo ambayo yalirekodiwa akiwa kwenye nyumba ya waziri mkuu ya Dodoma. yale mazungumzo yalikuwa yarushwe na TBC alhamisi usiku. Tido alitaka airushe kama ilivyo bila kuedit. wapambe wa JK walizipata taarifa very late kwamba EL anamwaga mboga, kipindi kilipotaka kwenda hewani tu yaani tido anamtambulisha EL, kikakatwa hapohapo. anayetaka kujua Ngoyayi aliongea nini amuulize Tido atamweleza vizuri, kwa kuwa Tido hayupo tena kifungoni(TBC) yupo huru (mwananchi).

Najua EL hawezi kuongea tena hii issue mpaka JK atakapomaliza uraisi wake, ila issue ya richmond itampa tabu sana katika harakati za uraisi. Haitoshi tu kusikia kuwa EL amemweleza JK kwenye vikao vya kamati kuu dodoma kwamba yeye JK ndio aliyekuwa anampa maelezo kuhusiana na Richmond, wananchi wanataka wamsikie yeye EL mwenyewe.


I WILL ALWAYS BE THE TRUTHFUL DISCIPLE OF NGOYAYI

hapo ndo ameshusha credit zake mkuu kwanini afiche hayupo tayali kufa kwa ajili ya kutetea maslahi ya nchi hii, MNAFIKI NA MPENDA URAISI TU HUYU!
 
Kaswali kengine kadogo ka nyongeza: Kwa nini yuko kimya sana mle mjengoni ambako angeyasema vizuri zaidi haya alooyasema pale ITV? Mzee JSM pamoja na kutopangilia vizuri hoja zake aliendelea kuongea Bungeni. Rafiki yako Lowasa ni jasiri sana. Pamoja na kutuibia koote bado anataka atutawale tena!
Mkuu WildCard, rekebisho kidogo, Lowassa sio rafiki yangu, bali ni mwana CCM pekee ambaye mimi namkubali sana kwa kusimamishwa kugombea urais 2015 kwa tiketi ya CCM!.

Kimya chake kule mjengoni ni msuso!, amesusa kuongea chochote, au kuchangia chochote kwa saba bado ana kinyongo cha u-PM, hivyo anajihesabu kuwa yeye sio mbunge wa kawaida wa kusema sema na kuchangia changia bungeni!, baada ya yeye kuwa PM, he is now a "president in waiting"!, hivyo kusema sema sana sio kuzuri!.

Nevertheless, bunge la mwaka 2015, ataunguruma sana kumbomoa JK na mtandao wake, atahakikisha walomtundika msalabani kwa Richmond, wanasulubiwa!, yeye atasafishwa, atatakatishwa, atakaswa, atapakwa mafuta tayari kwa 2015, kama ni kweli yuko fit, basi mkae mkijua, kama CCM watamsimamisha Lowassa, 2015, ni CCM Tena!.
 
wawe tayari mara ngapi mkuu ulimsikia walimuuliza akawajibu
wazungu wanasema uwezi kuongea kitu mpaka wakati ujavuka mto so subirini ukifika wakati basi tutavuka jamani
infact jamaa ni kichwa najiuliza alipokuwa waziri mkuu mbona akuyafanya haya?????

kajenga sekondari nchi nzima,kaondo tatizo la maji shy kwa kuuvunja mkataba wa mwaka 1922.kaifuta na baadae kuishinda mahakamani kampuni ya city water.alitia saini mkataba na makanisa ili yapate ruzuku kwa ajili ya kuhudumia jamii.HALAFU KUNA MTU ANASEMA HAKUFANYA KITU.KWELI WANA MACHO LAKINI HAWAONI
 
watz tuna hasira na "EL" huyu si ndiye aliyeunda mtandao wa kitapeli wa kumwingiza Rais "DHAIFU" madarakani. hana cha kutuambia anapoteza muda. alishakataliwa na MWALIMU.naye ni miongoni mwa genge la mafisadi ndani ya CCM, 2015 kiama chao
 
.....[/QUOTE]
Akina Nape, Sitta, Mwakyembe,..., wanakuelewa kweli? Nitamshangaa sana JK na CC yake atakayounda mwaka huu wakimwachia mtu huyu akapenya hadi kwenye ballot boxes za 2015. Hebu tuangaze macho na akili zetu nje ya CCM pia.
Historia ya NCHI hii haimpi nafasi Lowasa kuwa Rais wetu ajae. Hakuna WAZIRI MKUU amepata kuwa RAIS isipokuwa Mwalimu pekee.
 
Back
Top Bottom