Duble Chris
JF-Expert Member
- May 28, 2011
- 3,481
- 564
hakuna kitu hapo hawa pccb ndiyo walio wakamata wale walio toa rushwa iringa fikirieni nini kinaendelea sasa
Takukuru Leo wameamua kumgeuka Edward Lowasa na vibaraka wake katika marudiano ya uchaguzi wa Arumeru. Katika sakata Hilo katibu wa uvccm wilaya ya Monduli ndugu Ezekiel Mollel ametupwa rumande Mara baada ya kukamatwa na simu yake ilipo pekuliwa na kukutwa na mesej alizokuwa Akiwasiliana na Lowasa kuhusu kuchukua hela kwa askofu na mathius manga kwa Lengo la kwenda kuwahonga wajumbe wa arumeru Mashariki.
Katibu huyo amekiri kupewa maelekezo hayo na Lowasa na kuomba asamehewe kwa kuwa Lowasa ni kiongozi mkubwa yeye asingeweza Kuwa na ujasiri wa kumkatalia. Hadi wakati huu Ezekiel Mollel na Askofu wapo rumande.
Pia katika tukio lingine Fred Lowasa amethibitika kumhonga ticket ya ndege Elirehema kaaya ili amsaidie Sioi aweze kushinda. Kwenye simu ya elirehema Kaaya zimekutwa mesej Kuwa nakulipia ndege pamoja na kukupa lile fungu la kuwapelekea wajumbe. Kwa ushahidi huu hadi sasa elirehema Kaaya yupo rumande.
Wakati wowote mambo haya yatapelekea wahusika kupelekwa mahakamani.
Wana Arumeru mashariki wafanye uchaguzi kwa amani na utulivu na tena wasiwe na hofu yoyote.
Utasemaje hongera kumbe waliokamatwa ni ma capos tu. Godfather bado anatamba!Naam sasa kweli serikali ya jk imeamua kama noma na iwe noma,huyu alitaka kujifanya yeye ni mkubwa kuliko chama na serikali yake..kitu kingine inaonekana lowassa mambo mengi ya kimkakati alikua akimtegemea sana rostam aziz maana tokea rostam aziz ajiweke kando na siasa lowassa strategy zake mwenyewe karibu zote zimekuwa zikisambaratishwa mapema kabla hazijaanza..
Hongera takukuru arusha kwa utumishi uliotukuka na utii kwa amiri jeshi mkuu,mmeyashinda majaribu mkaitanguliza nchi,mzee manumba si mbaya ukichota busara hizi za takukuru arusha.
hii nchi utasema ni kaole sanaa group...sasa....
kwanini EL hajaumbuka hapo? yeye ni anaumezea urais mate? sasa mtu mwenyewe anahonga honga hivi unafikiri tukimpa urais si anaiuza nchi huyu
Sasa aliyeumbuka hapo ni EL au Kaaya?
Safari hii hakuna pa kupumulia!!!
Kwanza mi naombea EL ndio angewekwa lupango. Ila hapo waliowekwa lupango ni watu tofauti..
Sioi na EL wapo wanatanua mtaani, hata hawajahojiwa.
Utasemaje hongera kumbe waliokamatwa ni ma capos tu. Godfather bado anatamba!
hakuna mwenye huo ujasiri bado wa kumshika EL.
Waambie wajaribu kumkamata EL waone moto hao viwavi.
hii nchi utasema ni kaole sanaa group...sasa....
Iwapo yaliyosemwa ni kweli basi hali ya nchi ni tete. Askofu gani huyu anayetajwa? Kwa nini wasiwakamate watoa fedha sawa na wasambaza fedha? Hawa takukuru ni genge jingine la uhalifu nchini. Sina imani nao hata kidogo kwani baada ya mida mtasikia waliokamatwa wameachiliwa kwa uchunguzi au ushahidi wa takukuru haujitoshelezi. Wizi mtupi!
Utasemaje hongera kumbe waliokamatwa ni ma capos tu. Godfather bado anatamba!
Waambie wajaribu kumkamata EL waone moto hao viwavi.
Iliyoumbuka ni CCM wala si Lowassa.
Hii inaelekea ni kuoneshana ubabe ndani ya CCM. Tungojee kuona nani mbabe.
kwanini el hajaumbuka hapo? Yeye ni anaumezea urais mate? Sasa mtu mwenyewe anahonga honga hivi unafikiri tukimpa urais si anaiuza nchi huyu